TUTARAJIE MAANDAMANO YA AMANI KUDAI KATIBAMPYA


Pichani ni Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la Katiba nchini, (JUKATA) Hebron Mwakagenda  akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam kuhusu  maandamano ya kudai katiba mpya.

Wakati Sintofahamu kuhusu katiba Mpya nchini Tanzania ikiendelea kuzidi huku Utawala wa awamu ya Tano ukiwa Kimya kuhusu swala hilo,Harakati zilizoanzishwa majuma kadhaa yaliyopita hatimaye yameanza kuzua mambo baada ya Jukwaa la Katiba Tanzania JUKATA kutangaza maandamano makubwa kudai kurejeshwa mchakato wa Katiba mpya.

Mchakato wa Katiba nchini ulisimama kupisha uchaguzi mkuu mwaka 2015 na Tangu kuingia kwa serikali ya awamu ya Tano kumekuwa kimya huku wanaharakati wakinongona chinichini kuhusu hatma ya mchakato huo ambao unatajwa kuligharimu taifa pesa nyingi kipindi cha ukusanywaji wa maoni yake.

Wakati hayo yakitokea Leo Jukwaa la Katiba Tanzania limetangaza Rasmi azma yake ya kufanya maandamano ya nchi nzima kuishinikiza serikali Kurejesha mchakato wa Katiba mpya.

Akitangaza Maandamano hayo Leo jijini Dar es salaam wakati Wa mkutano na waandishi Wa Habari,Mkurugenzi Mtendaji Wa (JUKATA),Hebron Mwakagenda amesema baada ya mkutano Mkuu Jukwaa hilo uliofanyika mkoani Dodoma mwisho Wa wiki iliyopita wamezimia kifanya maandamano nchi mzima yenye lengo la kudai katiba mpya.

 "Tumeazimia kufanya maandamano katika ngazi ya  kitaifa yatafanyika Jijini Dar es Salaam,yakianzia ofisi za JUKUTA  hapa Mwenge Tarehe 31 mwezi huu wa kumi Saa nne asubuhi na yatahitimishwa katika viwanja vya mnazi mmoja" amesema Mwakagenda.

Mwakagenda amesema Jukwaa la hilo ni teyari limeshaliandikia barua Jeshi la Polisi kanda Maalum ya Dar es Salaam kutoa taarifa juu ya kusudia kufanya maandamano hayo 

"Maandamano haya  ni ya amani ili kurudisha hamasa ya wananchi kuendelea kushiriki kwenye michakato ya kidemokrasia  hapa nchini"

"Kwa upekee na heshima kubwa sana JUKATA pia tumemwandikia barua Rais Magufuli kumwomba ayapokee maandamano yetu ya amani katika viwanja vya Mnazi Mmoja" Amongeza Kusema Mwakagenda.

Hata hivyo,Mwakagenda amesema kuwa maandamano hayo kwa upande Wa Mikoa  mingine nje ya Dar Maandamano ambapo yatafanyika kila wilaya.

Pamoja na hayo JUKATA wamesema wanaamini watapata ushiriano Wa kutosha Wa Jeshi la Polisi ili maandamano hayo yafanyike kwa amani.

JPM ABADILI BARAZA LA MAWAZIRI



Image result for MAGUFULIRais John Magufuli amefanya mabadiliko ya baraza la mawaziri kwa kuwatema mawaziri wanne waliokuwepo kwenye baraza la awali.

Mawaziri walioachwa ni aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe na nafasi yake kuchukuliwa na Hamis Kigwangwala aliyekuwa Naibu Waziri Wizara ya Afya.

Mwingine aliyeachwa ni aliyekuwa Waziri Maji na Umwagiliaji,  Mhandisi Gerson Lwenge ambaye nafasi yake imechukuliwa na Mbunge wa Katavi,  Mhandisi Issack Kamwele aliyekuwa naibu waziri wa wizara hiyo.

Panga hilo limempitia pia aliyekuwa Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura ambaye nafasi yake imechukuliwa na Mbunge wa Viti Maalum CCM, Juliana Shonza.

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani naye ametupwa nje na nafasi yake kuchukuliwa na Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga.

Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Magufuli kufanya mabadiliko ya baraza lake la mawaziri tangu aingie madarakani.

MANJI ANAWEZA POTEZA MAISHA MUDA WOWOTE-DAKTARI



Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Hospitali ya Aga Khan, Mustapha Bapumia (62) ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa anashangaa mtu mwenye umri mdogo kama Yusuf Manji (41) kuwa na vyuma vinne kwenye moyo.

Alieleza kuwa na vyuma vinne kwenye moyo ni hatari na kwamba anatembea katika kamba nyembamba.

“Kitaaluma huyu ni lazima ajiangalie sana yupo katika hatari anaweza kupoteza maisha muda wowote.”

Dk Bapumia ambaye ni shahidi wa tatu wa upande wa utetezi alimeeleza hayo jana Jumatatu mbele ya Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha wakati akitoa ushahidi katika kesi inayomkabili Manji ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroine.

Akiongozwa na Wakili Hajra Mungula kutoa ushahidi, Dk Bapumia alisema yeye kwa siku huwa anawaona wagonjwa 50 hadi 60 na kwamba Februari 21, 2017 ilikuwa ni mara ya kwanza Manji kupelekwa kwao akiwa na maumivu ya moyo.

Ameeleza kuwa wana utaratibu wa wagonjwa tete kuwapeleka katika kitengo cha dharura na kwamba Manji walimpokea, wakamlaza, wakamchunguza na kuona ana tatizo sugu la moyo pamoja na kuwa na umri mdogo.

"Nikatafuatilia historia na kubaini licha ya kuzibuliwa kwa mishipa yake mitatu India, Dubai na Marekani, ilikuwa bado haijaziba lakini alikuwa bado anapata maumivu ya moyo," ameeleza shahidi huyo.

Ameeleza kuwa walimfanyia vipimo na vilionyesha tatizo lipo na kuna sehemu ya nne inahitaji kuzibuliwa na kwamba mgonjwa alikuwa wazi kuwa anatumia sigara na pombe.

Kutokana na hali hiyo ameeleza walimshauri mgonjwa ili waweze kuzibuliwa lakini akawaambia waache na akaomba dawa kwa kuwa familia yake ipo Marekani na matibabu yake mengi yanafanyika huko.

Shahidi huyo alieleza kuwa wao kama hospitali hawezi kufanya chochote bila ridhaa ya mgonjwa hivyo wakampatia dawa na akaruhusiwa Februari 24, 2017.

Alieleza kuwa siku hiyo hiyo alirejeshwa tena hospitalini hapo nyakati za saa mbili usiku akisumbuliwa na maumivu kwenye moyo, wakamlaza mpaka tarehe Machi 14, 2017 ambapo aliruhusiwa.

“Katika kipindi hicho Manji aliridhia na kuzibuliwa vyuma kwenye moyo.”

Ameeleza kuwa walimpatia dawa ikiwamo za kupunguza kolestro (mafuta) kupunguza maumivu sugu ya mgongo pamoja na kupunguza hofu ambazo zimo ndani ya Morphine na Benzodiazepines.

Kwa upande wake Manji akijitetea aliiomba Mahakama imuachie huru.

Akitoa ushahidi wake alieleza kuwa yeye ana matatizo ya moyo ya kurithi kutoka kwa babu zake ambao walikwishafariki kwa ugonjwa huo.

Ameeleza kuwa ugonjwa wa moyo ulimuanza akiwa na umri wa miaka 26 na kwamba mara nyingi amekuwa akitibiwa nje ya nchi ikiwamo India na Marekani na ana vyuma vitano kwenye moyo.

Akitoa ushahidi mahakamani hapo, Manji ameeleza kuwa kila baada ya miaka miwili anavibadilisha na kufanya uchunguzi vinafanya kazi vipi.

Akiongozwa na wakili wake, Hajra Mungula, Manji ameeleza kuwa katika ripoti zake za kati ya 2009 na 2016 haijawahi kutokea akaonekana kama anatumia dawa za kulevya.

Manji akiendelea kujitetea ameeleza kuwa anatumia vidonge 30 hadi 35 kwa siku.

Manji ameeleza kuwa polisi walikuwa wastaarabu wanampatia dawa na kwa upande wa Magereza vidonge vilikuwa katika kabati wanampatia.

Manji ameeleza kuwa Februari 8, 2017 alipata taarifa ya kutuhumiwa utumiaji wa dawa za kulevya na kuripoti kwa Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalum (ZCO).

Baada ya kuipata taarifa hiyo ameeleza aliitisha mkutano na waandishi wa habari kukanusha taarifa hiyo na Februari 9, 2017 alikwenda polisi kwa sababu anaheshimu jamuhuri na alitaka kazi ifanyike kwa haraka.

Ameeleza alivyokwenda alichukuliwa na kupelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ambapo alikutana na Gwajima(Askofu Josephat) na akatoa sampuli ya mkojo.

Ameeleza kuwa baada ya hapo walikwenda kukagua nyumbani kwake walichukua kompyuta, credit card na visa card.


Amesema kuwa anashangaa kwanini walichukua hivyo vitu wakati havihusiani na kesi ya dawa za kulevya na kuliacha sanduku lililokuwa na sindano na vifaa tiba.


Aliongeza kuwa inajulikana kuwa kuna ugomvi wa kibiashara ambapo wanagombea kampuni ya Tigo na kwamba hiyo kesi ni propaganda na ni mchezo mchafu.


Amesema hiyo kesi imemuathiri yeye binafsi na baba yake alimuachia vitu viwili jina zuri na maadili kwa jamii.


Pia imemuaribia jina kwa jamii yake, msikitini anashindwa kwenda kusali, biashara pia na imeumiza watoto na imemfanya aachie Uenyekiti wa Klabu ya Yanga.


Amesema kuwa kutokana na kesi hiyo anaona aibu kukaa na viongozi ambao anafahamiana nao akiwamo Raila Odinga na rais mstaafu Benjamin Mkapa


Kesi hiyo imeahirishwa hadi leo itakapoendelea kwa ushahidi wa upande wa utetezi.



Awali Manji alidai kuwa yeye ni mshauri wa kampuni za familia na kwamba alikataa tuhuma za dawa za kulevya ili mahakama imsikilize na kutenda haki na kwamba dawa aina ya Morphine na Benzodiazepines ni sehemu ya dawa zake ambazo anatumia.

Watanzania watakiwa kufuta sheria na taratibu za jenzi kuepusha bomoabomoa


Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo ya makazi Mhe. Angelina Mabula akihutubia katika hafla ya maadhimisho ya 32 ya makazi duniani kutoka kulia ni mkurugenzi wa nyumba Bw.Pius Tesha na wa pili kulia ni mkurugenzi wa mipangomiji profesa John Lupala maadhimisho yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
PICHA 1
Mwakilishi wa makamu mkuu wa chuo cha ushirika moshi Dkt.Lucas Mataba kulia akitoa salam kwa Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo ya makazi Mhe. Angelina Mabula wa kushoto  katika maadhimisho ya makazi duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano karimjee Jijini Dar es Salaam leo wa kwanza kushoto ni mkurugenzi wa mipangomiji profesa John Lupala.
PICHA 2
mkurugenzi wa mipangomiji profesa John Lupala kushoto akitoa maelezo kwa wadau wa nyumba na makazi katika maadhimisho ya 32 ya makazi duniania yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam kutoka kulia ni Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo ya makazi Mhe. Angelina Mabula na wa pili kushoto ni Mwakilishi wa makamu mkuu wa chuo cha ushirika moshi Dkt.Lucas Mataba.

PICHA 4
Mkurugenzi msaidizi wa urasimishaji makazi Bi.Beritha Mlonda akiwasilisha makala ya urasimishaji makazi katika maeneo yaliyoko kwenye mkakati wa mpango wa makazi bora kwa Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo ya makazi Mhe. Angelina Mabula katika maadhimisho ya 32 ya makazi duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano karimjee Jijini Dar es Salaam hivi leo.
PICHA 5
Wadau wa nyumba na makazi wakifuatilia mkutano wa maadhimisho ya 32 ya makazi yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano karimjee Jijini Dar es Salaam leo ambapo kauli mbiu ya mwaka  huu ni “sera za nyumba ,nyumba za gharama nafuu”.
PICHA 6
Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo ya makazi Mhe. Angelina Mabula, kulia ni mkurugenzi wa mipangomiji profesa John Lupala na kushoto ni Mwakilishi wa makamu mkuu wa chuo cha ushirika moshi Dkt.Lucas Mataba wakiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa nyumba na makazi wa bodi ya mwenge Jijini Dar es Salaam katika madhimisho ya 32 ya makazi duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano karimjee Jijini Dar es Salaam leo.(picha na paschal dotto- MAELEZO).
………………
Na.Paschal Dotto-MAELEZO  .

Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imewataka wananchi kuzingatia Sheria wakati wa ujenzi wa makazi yao ili kuepuka kujenga kwenye maeneo yasiyoruhusiwa jambo linalosababisha bomoa bomoa isiyo ya lazima.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe.Angelina Mabula aliyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam katika Maadhimisho ya Siku ya Makazi duniani ambayo yalifanyika katika ukumbi wa Karimjee.

Mhe.Mabula alisema kuwa ni vyema wananchi wazingatie sheria kabla hawajaanza kujenga makazi yao husika kwa kutoa taarifa kwenye ofisi husika ili kuepuka ukiukwaji wa Sheria za nchi katika ujenzi wa makazi.
“Watanzania tunakumbushwa kuzingatia Sheria na taratibu za nchi kwa sababu ubomoaji unaofanyika siyo kwa makusudi bali ni kwasababu tu watu wamekiuka Sheria zilizopo na pengine watumishi wasio waaminifu ndani ya Serikali ambao wanawapa watu maeneo pasiporuhusiwa”, alisisitiza Mhe. Mabula

Akizungumuzia mpango mkakati wa Wizara hiyo Mhe. Mabula alisema kuwa zaidi ya Miji 26 nchini ikiwemo Mtwara, Singida Mwanza na Dar es Salaam iko kwenye mchakato wa kupangilia makazi yake na kuwawezesha wananchi kuondokana na adha ya msongamano wa makazi.

Aidha Mhe. Mabula alisema kuwa katika maadhimisho hayo ya 32 yenye kauli mbiu isemayo ‘Sera za Nyumba :Nyumba za Gharama Nafuu’ ambayo inalenga zaidi kuimarisha sera za nyumba na makazi kwa kufuata sheria na taratibu kwa ujenzi wa makazi ya jamii             yenye ubora zaidi.

Mhe.Mabula aliongeza kuwa kwa Sera hii ina madhumuni makubwa katika kuhakikisha nyumba na makazi bora yenye huduma za msingi kwa jamii toshelezi ,kuwa na mazingira salama ya kuishi kwa wananchi wote hususani wenye mahitaji maalum wakiwemo watoto, vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu pamoja na upatikanaji wa usafiri na nishati endelevu zenye gharama nafuu ,ili kuwezesha yote haya ni lazima kujua Sheria inasemaje katika kupangilia miji iliyosalama kwa manufaa ya wote.

Alibainisha kuwa huduma nyingine ambazo zinapatikana kwenye makazi yaliyo katika mpangilio mzuri ni upatikanaji wa maji safi na salama na mfumo mzuri wa uondoshaji maji taka kwa ajili ya afya ya binadamu pamoja na uwepo wa hewa safi na ya kutosha.

“Ukienda kwenye eneo ambalo haliruhusiwi kujengwa lazima wakati ukifika kwa wenyewe kulitumia watakuondoa tu kwa sababu si eneo sahihi la makazi kwa hiyo mimi niseme ili kuepuka hii bomoabomoa tusijenge bila kuwa na kibali maalumu kutoka kwenye taasisi inayohusika ili kuweza kukidhi matakwa ya sheria na taratibu za makazi salama”,alisema Mhe. Mabula.