Waziri mkuu mgeni rasmi upokeaji saruji kwa njia ya reli -Moshi




Safari za treni ya mizigo kwenda mikoa ya kaskazini zilizokuwa zimesimama kwa zaidi ya miaka 13, zitaanza tena Jumamosi hii ya Julai 20, 2019 ambapo Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa ataipokea treni hiyo mjini Moshi Mkoa wa Kilimanjaro
ADVERTISEMENT

Moshi. Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuzindua treni ya mizigo Jumamosi ya Julai 20, 2019 Mkoani Kilimanjaro.
Treni hiyo itapokelewa Mjini Moshi Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa na mabehewa 20 iliyobeba mifuko 20 ya saruji.
Kwa zaidi ya miaka 13 safari za treni hizo zilisimama kufanya kazi katika mikoa ya Tanga na Kilimanjaro kutokana na sababu mbalimbali.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu Julai 15, 2019 amesema Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo.
Hata hivyo Mwananchi limepita katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo na kushuhudia usafi ukifanyika katika barabara za reli  huku baadhi ya wananchi wakishangaa kuona kichwa cha treni kikipita maeneo mbalimbali.
Jana usiku kichwa cha treni kilipoonekana kikipita katika baadhi ya maeneo Mjini Moshi wananchi mkoani humo walianza kushangilia kwa furaha huku wengine wakipiga kelele za furaha.
PIA SOMA

FUNGUA LINK HII UONE MAAJABU

http://MyWorkingHour.com/?userid=512046
Je!unapenda kutengeneza pesa basi link hii ni free unajiunga ukishamaliza subiri majibu ndani ya masaa 24

BILIONI MOJA YAWAPONZA POLISI SABA



1. E.4948 CPL Dani Isack Kasala
2. F.1331 CPL Matete Maiga Misana
3. G.1876 PC Japhet Emmanuel Lukiko
4. G.5080 PC Maingu Baithaman Sorrah
5. G.6885 PC Alex Elias Nkali
6. G.7244 PC Timoth Nzumbi Paul
7. H.4060 PC David Kadama Ngelela.

Aidha, kuhusu Afisa SSP: Moris Okinda ambaye alikuwa kiongozi wa askari hao walioomba na kupokea rushwa ya kiasi hicho cha fedha, mamlaka yake ya kinidhamu tayari imemsimamisha kazi na tayari amefikishwa mahakamani pamoja na askari hao.
Pamoja na askari hao, pia wamefikishwa mahakamani watuhumiwa wengine wa nne waliokamatwa huko Kigongo feri Wilayani Misungwi wakitorosha madini hayo ya dhahabu kutoka Tanzania kwenda Nchi jirani ya Rwanda.

Watuhumiwa waliokamatwa wakitorosha madini hayo ya dhahabu ni;
1. Sajid Abadalah Hassan, miaka 28, mfanyabiashara wa dhahabu, mkazi wa Ilala Dar es Salaam na Mwanza mtaa wa pamba ‘A’.
2. Kisabo Kija  Mkinda , miaka 55, mfanyabiashara wa dhahabu, mkazi wa mwatulole –Geita
3.Emmanuel Ntemi, miaka 63, dereva, mkazi wa kijiji cha mwatulole –Geita
4. Hassan Sadiq Hassan, miaka 28, Mhindi, Raia wa Pakistani, mkazi wa Mwanza mtaa wa Pamba ‘A’, Mfanyakazi wa duka la kuuza vito.
Kufuatia sakata hili, Jeshi la Polisi Tanzania kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na wanaendelea na uchunguzi wa kina ili tuweze kuwakamata watuhumiwa wote waliohusika kwa namna moja au nyingine katika sakata hili.

WAZIRI MHAGAMA ATINGA KIWANDA CHA VIATU.............ATOA AGIZO KWA VITENDAJI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama amewataka watendaji wa kiwanda cha Viatu na bidhaa za ngozi cha Karanga Wilaya ya Moshi kuzalisha bidhaa zenye ubora na kuendana na Soko lililopo nchini.
Ametoa kauli hiyo alipotembelea kiwanda hicho mwishoni mwa wiki ili kukagua shughuli za uendeshaji wa kiwanda hicho na kujiridhisha na ubora wa bidhaa zinazozalishwa.

“Niwatake watendaji kuweka mikakati madhubuti ya kuendelea kutengeneza bidhaa zenye ubora kwa kuzingatia viwango vinavyotatiwa”, Mhagama
Aidha Waziri aliwaasa watendaji wa kiwanda hicho kuendelea kutatua changamoto zinazowazunguka za kimfumo kwa kuzingatia sheria na taratibu za uendeshaji wa kiwanda hicho ili kuendana na ukuaji wa teknolojia na ushindani ulipo.

“Nisingependa kuona kiwanda kinakwama kuzalisha bidhaa zenye ubora, hivyo ni vyema kuzingatia sheria na kanuni za uendeshaji wa kiwanda katika ufanisi wa hali ya juu”,alisisitiza mhagama.
Kiwanda cha viatu cha Gereza Kuu Karanga, Moshi kilizinduliwa rasmi Juni 3, 1977 na Rais wa awamu ya kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Baba wa Taifa Mwalimu, Julius Kambarage Nyerere.Awali kilikuwa na ubia na Mfuko wa hifadhi ya jamii wa PPF ambapo baada ya mabadiliko ya kuunganishwa kwa mifuko hiyo , kwa sasa kina ubia na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF.

UHABA WA MADARASA TATIZO WANAFUNZI 1266 WAKOSA MASOMO



Wanafunzi 1266 waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2018/2019 mkoani Lindi wameshindwa kujiunga na kuanza masomo kutokana na ukosefu wa vyumba vya madarasa.
Hayo yalibainishwa jana na katibu tawala(RAS) wa  mkoa wa Lindi, Rehema Madenge alipozungumza kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa(RCC) kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa,iliyopo katika manispaa ya Lindi.
Madenge alisema katika zoezi la uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2019, wanafunzi 11808 walichaguliwa na kupangiwa shule watakazo jiunganazo kwa ajili ya masomo.Ambapo kati ya wanafunzi hao waliochaguliwa ni wasichana 6124 na wavulana 5684.
Alisema kati ya wanafunzi hao waliochaguliwa,bado wanafunzi 1266 hawajajiunga kwenye shule walizopangiwa kutokana na kukosekana kwa vyumba vya madarasa.Huku akibainisha kwamba wanafunzi hao ni wasichana 602 na wavulana 664.

Madenge alizitaja halmashauri ambazo baadhi ya wanafunzi waliochaguliwa wameshindwa kuanza masomo kutokana na tatizo hilo kuwa ni,majina na idadi ya wanafunzi kwenye mabano ni Kilwa(434),Lindi(443),Nachingwea(127) na Ruangwa wanafunzi 262.

Katibu tawala huyo wa mkoa wa Lindi alisema kushindwa kujiunga kwa wanafunzi hao mapema kumesababishwa na upungufu wa vyumba vya madarasa 39 ambavyo vingeweza kukidhi mahitaji.

"Wilaya inayoongoza kwakuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa ni Kilwa ambayo inaupungufu wa vyumba kumi nanne hadi sasa.Ruangwa vyumba kumi na moja,Lindi vyumba kumi na wilaya ya Nachingwea ni vyumba vinne,"alisema Madenge.

Alisema kufuatia hali hiyo,mkuu wa mkoa wa Lindi,Godfrey Zambi ameziagiza halmashauri ambazo wanafunzi waliochaguliwa wameshindwa kuanza masomo zikamilishe ujenzi wa vyumba vya madarasa.Ambapo amezitaka ifikapo tarehe 15,mwezi Februari,mwaka huu ziwe zimekamilisha ujenzi huo.

Kufuatia hali hiyo baadhi ya wadau wa elimu mkoani humu walitoa maoni yao yanini kifanyike.Miongoni mwa wadau hao ni Mohammed Mussa anaeishi katika manispaa ya Lindi.Ambae alisema wazazi na walezi hawanabudi kuungana ili kutatua changamoto zilizopo kwenye sekta ya elimu.Badala ya jukumu hilo kuachiwa serikali peke yake.

Mohammed alisema alitoa ushauri huo wa jumla kutokana na mkoa wa Lindi kuendelea kupata matokeo mabovu ya kiwanga cha ufaulu.Ambao matokeo ya mtihani wa kidato cha pili umeshika nafasi ya 24 kati ya 26 iliyopo Tanzania bara.

TUNDAMAN:NILIKUWA KIMYA KWA SABABU...............



Msanii wa muziki wa kizazi kipya Tunda Man, amesema sababu iliyomfanya awe kimya baada ya kuoa ni kutafuta heshima ya ndoa, ambayo alihisi asingeipata kwa mapema angedhalilika.

Akizungumza na eNewz ya East Africa Television, Tunda Man amesema kwamba kitendo cha kutokuwa na mtoto baada ya kuoa kilikuwa kinamnyima raha, hivyo aliamua aache vingine vyote ili kutafuta heshima ya ndoa, lakini sasa anarudi kwenye game rasmi kwani ameshapata alichokuwa akikitafuta.

“Kitu kikubwa ni kwamba sasa niko huru, mwanzo ilikuwa heshima ya ndoa lazima mtoto, kitu kama hiko kilikuwa kinanitia stress kinoma yani, kwa hiyo nimeoa kama miaka miwili iliyopita, na nilikuwa nimekaa kimya ka muda mrefu kutafuta heshima ya ndoa, mnielewe wananchi, nafikiri heshima imekuja tayari, nina mtoto anaitwa Itsal, kwa hiyo kitu kikubwa sasa hvi nadeal na ngoma zangu”, amesema Tunda Man.

Msanii huyo amesema wiki ijayo anatarajia kuachia kazi mpya tatu kwa pamoja, ikiwemo ambayo ametunga baada ya kushuhudia machungu aliyopitia mke wake wakati wa ujauzito.

HOJA 15 ZA MWAKYEMBE



KAMBI Rasmi ya Upinzani Bungeni imesema imejipanga kumbana kwa hoja 15 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, atakapowasilisha bungeni mjini Dodoma leo hotuba ya makadirio ya wizara yake kwa mwaka ujao wa fedha.

Mambo hayo ni pamoja na kutotungwa kwa kanuni za sheria mpya ya habari iliyotungwa mwaka 2016, kupotea kitatanishi kwa waandishi wa habari, kusajili magazeti kila mwaka, waandishi wa habari kulipia vitambulisho vya kitaifa kila mwaka na ufujaji wa mapato ya mechi za soka zinazochezwa nchini.

Zingine ni serikali kutotenga bajeti kusaidia maendeleo ya michezo, madai ya wasanii kutengenezewa matabaka na wenye ving'amuzi kutoza huduma hadi kwa vituo vya televisheni (TV) visivyopaswa kulipiwa.

Pia wasanii kuimba nyimbo zisizo na maadili na kuvaa mavazi yasiyoendana na utamaduni wa Kitanzania, kuvamiwa kwa viwanja vya michezo nchini na changamoto katika upatikanaji wa washindi wa shindano la Miss Tanzania.

Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya Bunge la Bajeti iliyotolewa na Idara ya Habari na Elimu ya Bunge leo, Bunge litajadili kwa siku moja hotuba ya makadirio ya wizara hiyo kwa mwaka ujao wa fedha.

Akizungumza na Nipashe mjini hapa jana, Naibu Waziri Kivuli wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Devotha Minja, alisema wamepanga kuutumia mjadala huo kuibana serikali ili izitatue changamoto hizo.

Alisema hoja ya kwanza ni kile alichokiita kuvifunga midomo kwa vyombo vya habari vinavyomilikiwa na watu binafsi kwa kuvifungia na kuvitoza faini pale zinapochapisha au kutangaza habari kukosoa mwenendo wa utendaji wa serikali.

Alisema hali hiyo inarudisha nyuma maendeleo ya tasnia ya habari na kuminya uhuru wa kujieleza na haki ya kupata habari.

Minja ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), alisema hoja yao ya pili ambayo Dk. Mwakyembe watamtaka awape majibu bungeni leo ni kutotungwa kwa Kanuni za Sheria mpya ya Habari nchini.

Alisema licha ya Bunge kuipitisha muswada wa sheria hiyo na kutiwa saini na Rais takriban miaka miwili sasa, kanuni hazijatungwa ili ianze kutumika.

"Kwa sheria ile ambayo tuliipitisha, bado hazitengenezwa zile kanuni za kuunda mabaraza ya kushughulikia kesi za mwandishi mmoja mmoja," alisema Minja.

"Na hapa tunaona kuna ucheleweshaji wa makusudi ili sheria ya zamani iendelee kutumika kwa sababu inampa mamlaka waziri kufungia magazeti. Sheria ya sasa haina kitu kama hicho, inataka mwandishi aliyekosea ndiyo awajibike na si kufungia gazeti zima."

Minja ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari, pia alisema upinzani umejipanga kuutumia mjadala wa leo kumbana Dk. Mwakyembe ili wizara yake iachane na utaratibu wa waandishi wa habari kulipia kila mwaka Sh. 30,000 kupata vitambulisho vya kitaifa (press cards) badala yake wawe wanalipa kila baada ya miaka kuanzia mitatu hadi 10 kama ilivyo kwa leseni ya udereva na hati ya kusafiria.

Minja alisema malipo ya aina hiyo yako pia katika usajili wa magazeti, akieleza kuwa kuna utaratibu mpya umeanzishwa na wizara hiyo wa kusajili gazeti kila mwaka ambao hawauungi mkono.

Alisema utaratibu huo aliodai upo katika nchi mbili tu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaona si rafiki kwa uhai wa tasnia ya habari kwa kuwa umelenga kuyazima usajili magazeti yanayoandika habari zisizoifurahisha serikali.

Pia alisema watautumia mjadala wa leo kumbana Dk. Mwakyembe na serikali kwa ujumla kuhusu kile alichodai wasanii nchini wamegawanyika.

"Kuna wasanii wanapata upendeleo mkubwa wa serikali, na hili sasa limetengeneza matabaka kwa wasanii wetu. Yaani sasa tumefikia hatua wasanii wanakuwa wa chama fulani ilhali wanapaswa kuwa pamoja na kufanya kazi kwa kushirikiana," Devotha alisema.

Naibu waziri kivuli huyo pia alisema bado kuna changamoto ya ufujaji wa mapato ya milangoni kwenye mechi za soka nchini, akidai kuna Sh. milioni mbili zinadaiwa zinalipwa kwa wanaojiita wawezeshaji wa uwanja kwa kila mechi inayochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Sambamba na hayo, alisema watahoji bungeni sababu za uongozi wa Shirikisho la Soka (TFF) kuteua mtu mwenye tuhuma za rushwa kushika nafasi ya mtu aliyeondolewa madarakani kwa tuhuma zenye mwelekeo huo.

Aliongeza kuwa upinzani umejipanga kuibana serikali leo ichukue hatua stahiki dhidi ya watoa huduma za ving'amuzi ambao wamekuwa wakikata huduma hadi kwenye Tv zisizoruhusiwa kulipiwa nchini.

Wakati Minja akieleza hayo, Mbunge wa Wawi, Ahmed Juma Ngwali (CUF), alisema upinzani pia umejipanga kumbana Waziri Mwakyembe ili wizara yake iwe inatenga bajeti ya kusaidia maendeleo ya sekta ya michezo nchini.

Ngwali alidai kuwa kwa takribani miaka mitatu sasa, TFF haijawahi kupokea kiasi chochote cha fedha kutoka serikalini kusaidia maendeleo ya mpira wa miguu nchini.

Naye Mbunge wa Kaliua, Magdalena Sakaya (CUF), aliiambia Nipashe mjini hapa jana kuwa kama atapata nafasi ya kuchangia mjadala huo leo, ataitaka serikali kudhibiti maudhui ya nyimbo za wasanii na uvaaji wao.

"Nyimbo za wasanii wetu zinapaswa kuzingatia maadili. Mavazi yao pia ni lazima yazingatie utamaduni wetu ili kutunza heshima ya nchi," Sakaya alisema huku akisisitiza Baraza la Sanaa (Basata) linapaswa kuwajibishwa kwa kile alichodai limeshindwa kudhibiti wizi wa kazi za wasanii.

Mbunge huyo pia alisema atautumia mjadala wa leo kumshauri Dk. Mwakyembe na wizara yake kudhibiti udanganyifu katika upatikanaji wa washindi wa Miss Tanzania, akidai kuwa katika miaka ya karibuni shindano hilo limetawaliwa na udanganyifu.

"Miaka ya nyuma, nilifuatilia miaka mitatu ya mwanzo, mshindi ulikuwa unamwona kuanzia hatua ya mwisho kuwa huyu atashinda na kweli inakuwa hivyo. Lakini miaka ya karibuni kumekuwa na udanganyifu mkubwa ambao unaashiria ama rushwa au kujuana," alisema.

"Baadhi ya ma-Miss wenyewe wanaishi maisha ya ajabu ya kubadilisha wanaume. Hivi kweli hii ndiyo maana ya shindano hili? Kulikoni kuendelea kuiabisha nchi, ni heri lifutwe tu."

Sakaya pia alisema atautumia mjadala wa leo kuibana serikali ivirejeshe viwanja vya michezo na maeneo ya wazi yaliyovamiwa na kuendelezwa kwa kuwa uvamizi huo unakwamisha maendeleo yua watoto kimichezo.

"Ni aibu viwanja vya michezo vimevamiwa kujengwa majumba na serikali ipo inaangalia tu," alisema Sakaya na kuongeza:

"Ni lazima kama serikali inayojali maendeleo ya watoto na michezo tuvirejeshe viwanja na maeneo ya wazi yaliyovamiwa. Kama kuna mtu kajenga nyumba kwenye eneo la wazi tubomoe ili watoto wapate mahali pa kucheza.

"Lazima kama taifa tuwekeze katika michezo kwa sababu michezo ni ajira, ni afya na burudani. Rais mstaafu (Jakaya) Kikwete alikuwa analipa hadi mishahara ya makocha lakini sasa serikali inaonekana imejiweka kando kuendeleza michezo. Shuleni hakuna vifaa vya michezo.

"Tunategemea nini huko mbele kama hatuwekezi kwa watoto kwa sasa? Kina (Cristiano) Ronaldo hawakutengenezwa ukubwani, tuwekeze kwa watoto."

HAWA HAPA WATEJA WATAKAOHUDUMIWA NA NSSF



SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limetaja aina ya wanachama litakaohudumia baada ya Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kusainiwa na Rais John Magufuli hivi karibuni.

Meneja Kiongozi wa NSSF Mkoa wa Temeke, James Oigo, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waajiri kuhusu sheria hiyo mpya na wajibu wao katika kulinda haki za wanachama.

Watu watakaokuwa wanachama wa NSSF, alisema, ni waajiriwa wote wa sekta binafsi, wageni ambao wameajiriwa Tanzania Bara, waajiriwa katika taasisi za kimataifa zinazofanya kazi Tanzania Bara na watu wote waliojiajiri wenyewe na wale wa sekta isiyo rasmi.

Kwa mujibu wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya mwaka jana, mifuko ya sekta hiyo imeunganishwa na kubaki miwili - NSSF na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).

Mifuko iliyounganishwa kwa sheria mpya ni PPF, GEPF, LAPF na PSPF.

Oigo alisema NSSF inawatembelea wanachama wake nchi nzima kuwaelimisha juu ya sheria hiyo, ili kuondoa hofu iliyopo miongoni mwao baada ya mifuko kuunganishwa na kubaki miwili.

Katika ziara hizo, alisema, NSSF itahimiza waajiri kuwasilisha michango ya wafanyakazi kwa wakati ili kuliwezesha shirika kulipa mafao ya wanachama kwa ufanisi, kuzijua changamoto zinazowakumba waajiri.

"Waajiriwa wote ambao wataajiriwa baada ya sheria hii kuanza ndio watakuwa katika mfuko ama wa PSSSF endapo wanaajiriwa katika sekta ya umma na NSSF endapo wanaajiriwa katika sekta binafsi," alifafanua.

Aidha, alisema waliokwishaajiriwa wakati sheria hiyo inaanza ambao walikuwa katika mifuko iliyounganishwa watakuwa wanachama wa mfuko wa PSSSF bila kujali wapo setka binafsi au ya umma.

Aidha, watumishi ambao walikuwa wanachama wa NSSF watabakia kuwa wanachama wa NSSF bila kujali sekta wanayotoka, alisema Oigo.

Alizidi kufafanua kuwa kanuni ya ulipaji mafao na idadi ya mafao yatakuwa ya aina moja kwa mifuko yote miwili.

Akifungua mkutano huo, Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF, Bathow Mmuni, alisema sheria mpya ya hifadhi ya jamii imeshasainiwa na Rais na sasa zimebakia taratibu za kiuendeshaji.

Naye Meneja wa NSSF Kinondoni, Marco Magheke, alisema shirika limejipanga kuendelea kutoa huduma bora zaidi kwa wanachama wake.

DUA ZA MZEE AKILIMALI JUU YA SIMBA



Katibu wa Baraza la Wazee wa klabu ya Yanga, Ibrahimu Akilimali amesema kuwa kuelekea mchezo wao dhidi ya watani zao Simba SC kunahaja ya kutupilia mbali tofauti zao na kumuomba Mungu katika kuhakikisha wanachomoza na ushindi siku hiyo ya Aprili 29.

Wakati zimesalia siku mbili pekee kabla ya kukutana kwa watani hao wajadi Simba SC dhidi ya Yanga SC kwenye dimba la Taifa siku ya Jumapili hii, Mzee Akilimali ametumia muda wake kuiyombea timu yake kuhakikisha inachomoza na ushindi siku hiyo.

Tunalengo la kuwashinda wapinzani wetu, siyo rahisi lakini lazima ujiandae kwa hayo wazee tunatoa baraka zote kwa vijana kwakuwa hatuna kinyongo.

Isipokuwa mimi naomba tu Yaarabbi Yaarabbi nakuomba turudishie hali yetu ileile ya umoja na mshikamano wetu kwa kila hali, tushikamane kwaajili ya kuwasapato vijana wetu na tumuombe Mwenyezi Mungu kila mmoja kwa dua yake na imani yake ili tupate ushindi siku hiyo ya Jumapili.

Nawaomba wana Yanga wenzangu tuwe wamoja tuwache tofauti zetu twende katika mchezo maana ni mgumu sana.

Kocha mpya ameingia na viongozi wetu wamefanya mambo haraka haraka sasa hivi yupo kazini, Msimbazi ubingwa bado isipokuwa tu mtu hawezi kukata tamaa ila hali bado. Amenitambuka mechi chache tu na yeye atarajie kufanya vibaya kwenye mechi hizo alizo nazo.

Wazee hatuna ahadi yoyote kwa vijana kwakuwa hayo yanatamkwa na viongozi.

Simba ambayo inaongoza kwenye msimamo wa ligi kwakuwa na jumla ya pointi 59 nyuma ya hasimu wake Yanga wenye alama 48 zinatarajia kukutana siku ya Jumapili ya Aprili 29 kwenye dimba la Taifa Jijini Dar es salaam.

MKURUGENZI KUCHUNGUZWA UKEREWE



Baraza la Madiwani la Halmashauri la Mji wa Ukerewe hawana imani na utendaji kazi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Mji huo Frank Bahati.

Akizungumza na KWANGULEO Blog baada kuvurugika kwa Kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo George Nyamaha alisema Mkurugenzi anapaswa kuchunguzwa.

"Siku tatu kabla ya kikao tulishuhudia stakabadhi feki walizopewa wafanyabiashara zikiwa na zina mhuri wa halmashauri, baada ya kuhoji kuhusu hizo stakabadhi Mkurugenzi akawa hataki tuhoji na kujadili suala hilo, jambo lililopelekea madiwani kuanza mvutano na mkurugenzi katika kikao na kutoka nje," alisema Nyamaha.

Nyamaha alisema kwa muda mrefu wamekuwa na shaka naye juu ya utendaji kazi wake, ambapo walimfikishia taarifa Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya na walikuwa wanasubiri majibu.

Aidha ameiomba Serikali kupitia  Mamlaka husika kufuatilia suala hilo kwa haraka kwani wafanyabiashara wamekuwa wakiilalamikia halmashauri wanavyonyanyaswa na watozaji ushuru pamoja na wanaopiga doria ya utokomezaji uvuvi haramu.

HII HAPA KAULI YA KAMANDA MAMBOSASA JUU YA UVAAJI VIMINI DAR


Tokeo la picha la KAMANDA MAMBOSASA
Hatua hiyo inakuja baada ya gazeti la kila siku la Nipashe January 17 (leo) kutoka na kichwa cha habari; Polisi yakamata wavaa vimini, kunyoa viduku.
Akizungumza Dar es Salaam Kamanda wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema taarifa hiyo haina ukweli wowote kwani mwandishi ameandika kitu ambacho hakukisema.
“Nilitaka nitoe ufafanuzi nikikanusha haya ambayo yameandikwa hayakusemwa na Jeshi la Polisi, anayasema mwenyewe mwandishi kwa interest yake na sana alichokuwa anatafuta ni umaarufu wa stori,” amesema.
“Ninamtaka sasa arudi kwa watanzania aombe radhi ili kuondosha usumbufu uliojitokeza, nimepigiwa simu kuanzia jana toka maeneo mbali mbali kwa jambo ambalo kimsingi halijafanywa na Jeshi la Polisi,” amesisitiza.

WCF YAWANOA WAAMUZI,WASULUHISHI NA MAKATIBU KUTOKA TUME YA USULUHISHI NA UAMUZU(CMA)


 Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala, Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw.Peter Kalonga, (kushboto), akijadiliana jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, (wkawanza kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bw.Shanes Nungu, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa Waamuzi, Wasuluhishi na Makatibu Muhtasi kutoka Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) mjini Morogoro leo Januari 17, 2018. Bw. Kalonga alimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw. Eric Shitindi.
Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala, Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw.Peter Kalonga,kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Eric Shitindi, akifungua mafunzo hayo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, akitoa hotuba yake.

MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), umejipanga vema kuendelea kutoa huduma bora kwa wadau, hususan katika kipindi hiki ambacho Mfuko unategemea ongezeko kubwa la waajiri na wafanyakazi, kutokana na mkakati wa Serikali ya awamu ya tano wa kujenga uchumi wa viwanda, ambao utaongeza ajira.
Hayo yamesemwa leo Januari 17, 2018 mjini Morogoro na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa Waamuzi, Wasuluhishi na Makatibu Muhtasi kutoka Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), ili kuongeza ujuzi kwenye utekelezaji wa majukumu ya Tume.

“Katika jambo hili la kujenga uchumi wa viwanda,  makampuni mengi yataanzishwa, kutakuwa na waajiri wengi, ongezeko la wafanyakazi, kwa hivyo unategemea kwamba hitajio la utoaji huduma za Mfuko kwa wadau  litaongezeka na Mfuko umekuja wakati muafaka na tupo kwa ajili ya kuwahudumia wale wote watakaopatwa na majanga mahala pa kazi lakini pia kuelimisha.” Alisema Bw. Mshomba.

Bw. Mshomba  alisema, kuanzia Julai, 2016 Mfuko ulianza kupokea madai ya Fidia yanayotokana na kuumia au kuugua mahali pa kazi.

“Jambo hili si rahisi kwa sababu ndio linaanza kwa hivyo tunahitaji ushirikiano wa karibu sana kutoka kwa wadau mbalimbali mkiwemo ninyi CMA, na katika hilo ushirikiano tu hautoshi Mfuko umekuwa ukitoa elimu ili kuwawezesha watu  wajue Mfuko umeanzishwa kwa sababu gani, kazi zake, lakini pia kujua taratibu za kudai fidia pale mfanyakazi anapopatwa na majanga ya kuumia au kuugua wakati akitekeleza wajibu wake wa kikazi.” Aliongeza Bw. Mshomba.

“Ndio maana leo hii tunao wataalamu wetu watakaotoa mada mbalimbali zikiwemo, Sheria za Fidia, Namna Fidia inavyolipwa lakini shughuli za Mfuko.” Alibainisha Mkurugenzi Mkuu Bw. Mshomba.

Aidha aliishukuru Tume kwa kuwashirikisha WCF ili kuwaelimisha wafanyakazi wake kutoka mikoa yote ya Tanzania bara.

“Ni muhimu kwetu sisi kuwaelimisha wadau kuhusu shughulim zetu na ndio maana huwa tuko tayari wadau wetu wanapotualika ili kutoa elimu hiyo.” Alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa ……..kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira, na Wenye Ulemavu, Bw. Eric F. Shitindi amewahimiza washiriki wa kuzingatia elimu watakayoipata kwenye mafunzo hayo ili hatimaye watekeleze ipasavyo malengo ya serikali ya awamu ya nne ya kujenga uchumi wa kati ifikapo mwak 2025.

“Ni matarajio yetu kwamba Tume na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, mnao wajibu mkubwa sana katika kufanikisha azma hiyo ya serikali kama nyinyi mtatekeleza wajibu wenu.” Alisema.
Baadhi ya washiriki.
Baadhi ya washiriki.
Mwenyekiti wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bw.Edrisa Mavura, akitoa hotuba yake.
Maafisa wa CMA wakiteta jambo.
Bw. Mshomba, (kulia), na Bw.Nungu, wakijadili jambo.
Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala, Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw.Peter Kalonga, akikaribishwa na Wakurugenzi wa WCF, Bw. Masha Mshomba, (kulia) na wa CMA, Bw.Shanes Nungu, alipofika kufungua mafunzo hayo
 Bw. Mshomba akijibu baadhi ya maswali ya washiriki kuhusu shughuli za Mfuko.
Baadhi ya washirtiki wakifuatilia mafunzo.
Kamishna wa Tume, Bi.Suzanne Ndomba, (kulia), akizungumza kwenye mafunzo hayo. Wengine ni Makamishna wenzake, kutoka kushoto, Bw.Kibwana Njaa, Bw.Jones Majura na Bw.Jaffary Ally Omar.
Picha ya pamoja.
Bw. Mashomba akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Sheria wa WCF, Bw. Abraham Siyovelwa, (katikati) na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Dkt. Abdulsalam Omar.
Washiriki wakipitia vipeperushi vya WCF.

GAIRO:YATIMA WASAIDIWA VIFAA VYA SHULE


Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe akiwaasa watoto yatima wa kituo cha Bethel Wilayani Gairo. Kulia kwake ni baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama walioambatana naye. Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Gairo, Mhe. Andrea Sendeha akitoa salamu kwa watoto yatima.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe akigawa zawadi kwa watoto yatima wa kituo cha Bethel kilichopo wilayani humo.
Watoto wa kituo cha Bethel Wilayani Gairo wakiwa wamejipanga mstari kupokea zawadi.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe (mwenye nguo ya njano), Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Gairo, Mhe. Andrea Sendeha (wa tatu toka kulia) pamoja na kamati ya ulinzi na usalama wakiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima wa kituo cha Bethel wa Gairo.


Katika kujali makundi yenye changamoto za maisha hasa watoto wadogo, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Shaidi Mchembe amegawa sare za shule na madaftari kwa watoto yatima 150 kituo cha Bethel Wilayani Gairo kinachosimamiwa na Mchungaji Chacha.

Hafla hiyo ya ugawaji wa vifaa ulifanyika mapema wiki hii, ambapo Mhe. Mchembe amesema kuwa huo ni utamaduni aliojiwekea kila mwanzo  wa mwaka wa kuwakumbuka watoto yatima na wale waishi katika mazingira magumu.

"Nawakumbusha wananchi kujenga utamaduni wa kusaidiana watu wasiojiweza ili muweze kupata baraka kutoka kwa mwenyezi Mungu, unajua unapokuwa nacho ukatoa kidogo unabarikiwa zaidi," alisema Mhe. Mchembe.

Mhe.  Mchembe aliwakumbusha watoto hao kuzingatia masomo kwani Serikali ya awamu ya tano ya Dr. John Magufuli inatoa elimu bure hivyo hakuna mtoto wa masikini atakayeshindwa kusoma. 

Katika kukua kwao wamtangulize Mungu naye ataendelea kuwabariki na kuwatoa katika hali ya kuhisi unyonge wa kukosa wazazi.

Mwisho aliwaasa waalimu kuwa na moyo wa upendo kwa watoto yatima. Pia kuweka karibu hasa watoto wa kike kuwaepusha na mimba za utotoni.

ELIMU YATOLEWA KWA VIONGOZI WA DINI DHIDI YA KUPINGA NDOA ZA UTOTONI


Mwenyekiti wa Mtandao wa kutokomeza Ndoa za Utotoni Bi. Valeria Msoka akisisitiza jambo katika mkutano uliowakutanisha viongozi wa dini zote lengo likiwa ni kujadili nafasi yao katika kupinga ndoa za utotoni.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia kwa umakini mkutano mapema leo jijini Dar es salaam.

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Al Hadi Mussa Salim akitoa ufafanuzi wa jambo fulani mapema leo katika mkutano uliowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali na kimila katika kujadili nafasi yao katika kupinga ndoa za utotoni.
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Al Hadi Mussa Salim akichangia mada mbele ya wageni walioudhuria mkutano huo mapema leo jijini Dar es salaam.

 Mkurugenzi mtendaji wa RICPT ambaye pia ni muwakilishi wa dini ya kikristo Rev. Canon Thomas Godda akitoa ufafanuzi juu ya siku hiyo, na nini nafasi yao kama viongozi wa dini katika kupinga ndoa za utotoni na ushiriki wao katika kuleta mabadiliko ya sheria ya ndoa inayotumika hivi sasa.
Mwanasheria kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Bw. Godfrey Mpandikizi akitoa presentetion mbele ya wageni waliudhuria mkutano wa kujadili kushinikiza viongozi wa dini na wakimila kupambana ili kuweza kubadilishwa kwa sheria ya ndoa iliyopo hivi sasa.

  • Viongozi wa dini zote hapa nchini wametakiwa kuwa mstari wa mbele kuishinikiza serikali kukubali kubadilisha sheria ndoa ya mwaka 1971.

  • Hayo yamesemwa mapema leo jijini Dar es salaam katika semina iliyoandaliwa na Mtandao wa Kutokomeza Ndoa za Utotoni(TECMN) iliyowakutanisha viongozi wa dini zote mbili pamoja na viongozi wa kimila kutoka mikoa mbalimbali.

  • Akiongea katika semina hiyo Bi. Valeria Msoka alisema kuwa viongozi wa dini ni watu walio karibu sana na jamii, hivyo wanazijua vizuri changamoto wanazokutana nazo wananchi ikiwemo ndoa za utotoni na wanatakiwa wasikae kimya kwani wao ndio msaada pekee kwa jamii yao.

  • Lakini pia viongozi wa dini ni watu wanaopewa nafasi nzuri na kuheshimiwa kwa kiasi kikubwa na serikali hivyo watumie muda huo kuiamba serikali kuwa sheria hii ya mwaka 1971 inayotoa ruhusa kwa mtoto wa kike kuolewa akiwa na miaka 14 haifai na inatakiwa kubadilishwa.

  • Mwenyekiti huyo aliendelea kusema kuwa lengo la kukutana na viongozi wa dini ni kujaribu kushauriana na kuona nini watakifanya kushinikiza kubadilishwa kwa sheria hiyo inayomnyima haki za zake za msingi mtoto wa kike.

  • Akiongea kwa niaba ya dini ya kiislamu Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Al Hadi Mussa Salim alisema kuwa dini zetu zimekuja kwa lengo kuu la kuwasaidia wanadamu na hasa wanawake ambao walikuwa wakinyanyaswa na kunyimwa haki zao katika jamii hususani kwa upande wa ndoa.

  • Aidha Sheikh Mkuu wa Mkoa alisema kuwa cha muhimu tuungane kwa pamoja Waislamu, Wakristo, viongozi wa Kimila pamoja na serikali katika mitazamo na mwazo yetu ili tujue kuwa mtoto wa kike ni nani na haki zake ni zipi anazostahili kupata, kwa njia hiyo tunaweza kufanikiwa kulitokomeza tatizo hili la ndoa za utotoni.

  • Sheikh huyo aliendelea kusema kuwa tusipokuwa na sauti moja hatutaweza kama viongozi wa dini tukisema ndoa za utotoni zikome lakini serikali ikipinga atuwezi kuondoa tatizo hili, cha msingi ni kukubaliana makundi yote kuwa hatuzitaki ndoa za utotoni katika jamii yetu serikali ikubali viongozi wa kimila wakubali, wananchi wakubali na makundi yote yawe tayari kupambana vita hivi.

  • Kwa upande wake kiongozi aliwakilisha dini ya kikristo Rev. Canon Thomas Godda alisema kuwa zama zimebadilika kwani mwanzo sharia hii ilivyotungwa na ilipitishwa kwa urahisi kwa kuwa watu hawakuwa na uelewa, ila kwa sasa watu wameelimika na inapaswa kupingwa kwa nguvu zote swala hili.

  • Bw. Thomas aliendelea kusema kuwa ndoa inayokubalika hata katika vitabu vya dini ni ya watu wazima wote ambao umri wao ni kuanzia miaka 18 na kuendelea, hivyo basi wao kama viongozi wa dini watajaribu kufanya ushawishi kwa kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha swala hili linatokomezwa kabisa na sheria inabadilishwa.

SILAHA ZA KIVITA ZAKAMATWA SHINYANGA


Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata silaha ya kivita aina ya AK-47 iliyotupwa na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi waliokuwa wanataka kuvamia kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd kilichopo Nhelegani katika kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Alhamis Januari 18,2018 Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule amesema walikamata silaha hiyo usiku wa kuamkia leo majira ya saa tano eneo la Tinde wakati majambazi hao wanafuatiliwa na polisi ndipo wakaamua kutupa bunduki hiyo.

“Silaha hii aina ya AK-47 yenye namba 18116428 ilikuwa imefungwa kwenye skafu yenye rangi ya nembo ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ikiwa na risasi 25 ndani ya magazine yake na risasi zingine 8,zikiwa kwenye mfuko mdogo wa nailoni”,alieleza Kamanda Haule.

“Majambazi wawili pia walitelekeza pikipiki aina ya SANLG yenye namba za usajili MC 856 BPF,mafuta ya cherehani ya kulainishia silaha,tochi mbili na koti zito”,aliongeza.

Alisema jeshi la polisi lilipata taarifa za majambazi hao kutaka kuvamia kiwanda hicho kinachomilikiwa na raia wa China tangu tarehe 6.01.2018 kisha kuanza kuwafuatilia na kubaini kuwa baadhi yao ni wakazi wa Kahama na Ushirombo ambapo amewataka kujisalimisha polisi.

Bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 iliyokuwa imefungwa kwenye skafu yenye rangi ya nembo ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliyotelekezwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Wachina mjini Shinyanga- Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Silaha na vifaa vilivyotelekezwa na majambazi
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha skafu iliyotumika kufunga bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 iliyotupwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Jielong
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha silaha aina ya AK-47 yenye namba 18116428 na mafuta ya kulainishia silaha yaliyotupwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Jielong
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule  akionesha risasi zilizotelekezwa na majambazi
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule  akionesha  pikipiki aina ya SANLG yenye namba za usajili MC 856 BPF iliyotelekezwa na majambazi
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule  akionesha koti zito lililotelekezwa na majambazi
Jengo la ofisi za kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd kilichopo Nhelegani katika kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga.
Meneja Mkuu Msaidizi wa kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania),bwana Liu Buhua akilishukuru jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga kwa kuzuia uhalifu uliotaka kufanywa na majambazi
Meneja Mkuu Msaidizi wa kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd ,bwana Liu Buhua akilishukuru na kulipongeza jeshi la polisi kuzuia uhalifu katika kiwanda hicho

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akiwa katika  kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd.