TUNDAMAN:NILIKUWA KIMYA KWA SABABU...............



Msanii wa muziki wa kizazi kipya Tunda Man, amesema sababu iliyomfanya awe kimya baada ya kuoa ni kutafuta heshima ya ndoa, ambayo alihisi asingeipata kwa mapema angedhalilika.

Akizungumza na eNewz ya East Africa Television, Tunda Man amesema kwamba kitendo cha kutokuwa na mtoto baada ya kuoa kilikuwa kinamnyima raha, hivyo aliamua aache vingine vyote ili kutafuta heshima ya ndoa, lakini sasa anarudi kwenye game rasmi kwani ameshapata alichokuwa akikitafuta.

“Kitu kikubwa ni kwamba sasa niko huru, mwanzo ilikuwa heshima ya ndoa lazima mtoto, kitu kama hiko kilikuwa kinanitia stress kinoma yani, kwa hiyo nimeoa kama miaka miwili iliyopita, na nilikuwa nimekaa kimya ka muda mrefu kutafuta heshima ya ndoa, mnielewe wananchi, nafikiri heshima imekuja tayari, nina mtoto anaitwa Itsal, kwa hiyo kitu kikubwa sasa hvi nadeal na ngoma zangu”, amesema Tunda Man.

Msanii huyo amesema wiki ijayo anatarajia kuachia kazi mpya tatu kwa pamoja, ikiwemo ambayo ametunga baada ya kushuhudia machungu aliyopitia mke wake wakati wa ujauzito.

No comments: