SABABU ZINAZOWAFANYA VIJANA KUWA TEGEMEZI


ZIJUE  SABABU ZA VIJANA WENGI WA AFRICA KUWA WATEGEMEZI
Makala na; Godson eric
Hii ni dhana ambayo haipingiki kwa asilimia 100%  kuwa vijana wengi wa  Africa ni tegemezi kutoka kwa wazazi wao.jambo ambalo halipingiki kuwa tangia kijana anapotoka kwenye tumbo la mama yake huzaliwa akiwa na dhana ya kusikiliza maagizo pamoja na maelekezo ambayo yanatoka kwa wazazi wao.ni kwel kijan lazima atii na kusikiliza maagizo ambayo yanatoka kwa wazazi wao.
Kutii wazazi sio tatizo kwan wao ndio wanakupa njia iliyo sahihi kuifuata ila vijana wao wenyewe ni waoga kuongea na kuelezea mawazo yao yaweze kuleta tija kwenye jamii inayowazunguka.nakuletea sababu hii ili uweze kuzijia na kuzichukulia hatua kama wewe kijana unataka mabadiliko katika maisha yako na katika jamii inayomzunguka kijana
Sababu hizi hapa za vijana wengi kuwa tegemezi
WAOGA;Amini usiamini kuwa kwa asilimia 89% ya vijana wengi ni waoga kusimama na kutetea hoja zao lakini pia kutoa mawazo ambayo yangeweza kuwa na matokeo chanya kwenye jamii inayomzunguka.ukipita mashule na mavyuo jambo hili halipingiki kwani hata kwenye sehemu ya majadiliano baina yawao wenyewe pia kuna wengine hawawezi kuongea hata baina ya wao wenyewe wanaonea aibu kuongea.kwa asilimia kubwa wasichana ndio waoga a=zana kuongea kwenye mjumuiko wa watu wengi hasa sehemu za majadiliano na sehemu ambazo wao wangepaswa kuwa mstali wa mbele kuelezea adha wanayoipata kwenye matatizo kam vile matatatizo ya maji katika makazi yao,adha wanayoipata kutokana na kushawishiwa  kujihusisha na maswala ya mahusiano.
 Vijana wa kiafrika wengi wao wana ni wazuri sana wa kuongea pembeni na kujisifu kuwa wao ni waongeaji wazuri.kijna wakiafrika ni mwepesi kuongea kwenye watu ambao amewazoea.kama kijna ukitaka uwe na kijana mwenye mabadiliko basi kuwa  jasiri kusimama  na kuelezea mawazo uliyonayo.
HAWAJIAMINI: Jambo linguine ni kuwa vijana wa kiafrika hajiamini kwa mambo ambao wanayafanya huwezi ni pinga  kwa hili kwani ni jambo  ambalo linaonekana kwenye macho ya watu wengi ndani na nje ya  ardhi hii ambayo vijana  wengi bado ni wasikilizaji wa vitu ila wao sio waanzishaji wa mada ambazo zingeweza kuwa na manufaa kwenye maisha yao wenyewe.kwenye muktadha wa kutojiamini ni kuwa ukiangalia kiundani ni kuwa vijana wengi wa kuafrika wanavipaji ambavyo wamezaliwa navyo ukilinganisha na vijana wanaoishi nje ya bara hili la afrika.vijana wan je wengi wao ujuzi wao wamepandikizwa nikimaanisha wao wanafundisha ujuzi Fulani I basi kubla kwa Africa kijana wa kiafrika kipaji alichonacho amezaliwa nacho. Tunaweza kuwa vijana wenye mafanikio  kwa kutoa dhana ya kutokujiamini  na kujenga dhana ya kujiamini katika kutaka kufanya kazi .
WEPESI KUSHAWISHIWA: Nani atanipinga kwa hili hasa hapa kwetu Tanzania kwani vijana wengi ni wepesi kushawishiwa kufanya jambo ambalo linaweza kuleta maafa kwao wenyewe.kijna hasa wa kitanzania ni mwepesi kutoa uhai wake kwa mtu ambaye anaweza kuwa asiye na faida  kwenye maisha yake mwenyewe.urahisi huo wa kuweza kushawishiwa unatokana na haili ambayo inawazunguka.ninakiri kuwa vijana wenyewe umri kuanzia miaka 17-30 ni wepesi kushawishiwa na kufanya jambo ambalo liko tofauti na upeo wao wa kuyadajili mambo kiundani na kujua kuwa jambo ambalo wanalifanya lina mantiki gani kwenye jamii yao.
Kwenye uwanja wa siasa kijana hutumiwa kama dhana ya ushawishi kwenye mazingira yanawazunguka.kwenye mavyuo ,vijana hutumiwa sana katika kuleta ushawishi kwenye siasa ambapo sasa kwa kuangalia baadhi a migomo ambayo imetokea kwenye mavyuo asilimia kubwa vijana hupoteza maisha lakini pia hupoteza viungo vyao kwa watu ambao wamekaa kwenye majamvi wakisubirri nini kitatokea baada ya migomo. USIKUBALI KUSHAWISHIWA KAMA UNAIMANI KUWA UNAA MALENGO MBELENI
SIO WAGUNDUZI WA MAMBO: Wengi wa vijana wa kiafrika sio wagunduzi wa mambo ambayo yanaweza kuwa na faida kubwa kwenye maisha yao.kusema sio wagunduzi wa mambo ni neon lenye taswira ya kuwaelezea vijana ambao wao huwa ni watu wa kuiga mambo amabyo nanaletwa kama utamaduni wa mambo ya nje hasa uvaaji wa mavazi Ambayo sio tamaduni kwa mtoto wa kiafrika ambaye anajua ni mavazi gani ambayo anatakiwa kuvaa hasa anapokuwa kwenye mjumuiko wa watu wengi.ili tuwe kijana mwenye uwezo  basi kubali kuwa kijan mgunduzi uweze kufanikiwa.

No comments: