Showing posts with label mchezo. Show all posts
Showing posts with label mchezo. Show all posts

KANUMBA ALINITOLEA PANGA LULU ANENA

Image result for PHOTO OF ELIZABETH MICHAEL


MSANII wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu ameanza kujitetea katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam akieleza alichokuwa akifanyiwa na marehemu Steven Kanumba.
Akitoa utetezi wake katika kesi hiyo ya kuua bila kukusudia, Lulu amesema Kanumba alikuwa akilewa na kumpiga na kwamba Kanumba aliwahi alimpiga kwa panga mapajani na akapelekwa Hospitali ya Mwananyamala.
“Sijasababisha kifo cha Kanumba kwa namna yoyote ile. Umbo langu lilikuwa dogo hivyo mimi ndiyo nilikuwa nashambuliwa. Kama marehemu asingeanguka labda angenidhuru. Kanumba alikuwa kama mlezi wangu, tulianza mahusiano miezi minne kabla ya kifo chake,” amesema Lulu.
“Nilikuwa nataka kutoka ila marehemu (Kanumba) alinikataza, alikuwa hataki nitoke, nilipomwambia natoka na marafiki zangu alinikimbiza na taulo na mimi nilikuwa naogopa kupigwa, mara nyingi alikuwa ananipiga kila akilewa na sio kwa akili zake.  Alipoona simu yangu inaita akahisi ni simu ya mwanaume akasema kwa nini naongea na simu ya mwanaume mbele yake? Marehemu akaingia uvunguni akatoa panga akasema leo nakuua huku akinipiga na panga kwenye mapaja”, ameelezea Lulu.
Lulu ameendelea kusimulia…. “Marehemu alianguka mwenyewe na kujigonga kwa nguvu na kuinuka akitapatapa, nilimwambia Seth kuwa Kanumba amedondoka na akajaribu kumuamsha hakuamka,  akasema anaenda kumuita daktari, alivyosema anaenda kumuita daktari na mimi nikaondoka nikiogopa anaweza akaamka akaanza kunipiga.  Niliondoka nikawasha gari kuelekea Coco Beach kutuliza akili”.
Muigizaji huyo ameendelea kusimulia kwamba … “Nilivyofika Coco Beach meseji zilianza kusambaa kuniuliza kuwa nasikia Kanumba amefariki, nikampigia Kidume ambaye ni rafiki yake Kanumba kumuuliza Kanumba yupo hospitali gani niende kumuona, akaniambia wewe usije hospitali, niambie uko wapi, tukakubaliana tuonane Bamaga.  Tulivyokutana Bamaga alikuwa kama anataka kuongea na mimi ghafla wakaja askari kunikamata,” ameeleza Lulu.
Baada YA Muigizaji, Elizabeth Michael ‘Lulu’kuanza kujitetea katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar, kwa tuhuma za kusababisha kifo cha Steven Kanumba bila kukusudia, msanii huyo amekana kuhusika na kifo hicho.
Lulu ameeleza siku ya tukio, Kanumba alikuwa amelewa na yeye Lulu alitaka kutoka na marafiki zake lakini alimkataza, baada ya Kanumba kuona simu ya Lulu imeita alizani anaongea na mwanamme mwingine huku ambapo alichukua panga na kumkimbiza nalo. Kanumba alianguka na Lulu kuchukua gari na kukimbilia Coco Beach ambapo baadaye alikamatwa na polisi maeneo ya Bamaga.
Jaji wa Mahakama Kuu, Samu Rumanyika amemtwanga maswali Lulu kama ifuatavyo;
Jaji Sam Rumanyika: Kipindi unaendesha gari ulikuwa na leseni halali?
Lulu: Ndiyo.
Jaji: Tufafanulie uhalali wake.
Lulu: Nilikuwa sina.
Lulu: Baada ya kukamatwa nilipelekwa kituo cha polisi Oysterbay nilikuwa nikihojiwa nikiwa sijui kama Kanumba amefariki.
Lulu ameeleza hayo leo Jumatatu akijitetea katika kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili.

VIINGILIO VYA MECHI YA SIMBA NA YANGA HIVI APA

Image result for PHOTO OF SIMBA FC VS YANGA FC

Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Young Africans na Simba utafanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kama ilivyotangazwa awali. Hakuna mabadiliko.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetangaza viingilio katika mchezo huo kwamba watazamaji watakaohitaji kukaa katika Jukwaa Kuu watalipia Sh 20,000 na Mzunguko ni Sh 10,000.

RONALDO ASHINDA TUZO ZA FIFA AKIWABWAGA MESSI NA NEYMAR JR

Staa wa Ureno, Cristiano Ronaldo amefanikiwa kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Fifa kwa mwaka 2017 kwa mara ya pili mfululizo tangu kureshwa kwa utaratibu wa tuzo huo, mwaka jana.
Ronaldo amekabidhiwa tuzo hiyo jijini London kulipofanyika sherehe za utoaji wa tuzo hiyo ambapo amewapiga bao Lionel Messi wa Barcelona na Neymar PSG.
Tuzo hiyo ambayo iliwepo miaka ya nyuma ilipotea baada ya kuungana na ile ya Ballond’Or lakini mwaka jana Fifa iliamua kujiweka pembeni na kuendelea kuratibu tuzo zake kama zamani huku wale wengine nao wakiendelea na tuzo yao.
Wakati Ronaldo akikabidhiwa tuzo hiyo, kocha wake wa Real Madrid, Zinedine Zidane yeye amepewa tuzo ya Kocha Bora wa Mwaka

HELKOPTA YAUWA WATANO KENYA


WATU watano wanahofi wa kufa akiwemo rubani wa helikopta iliyokuwa ikitoka eneo la Jarika Kaunti ya Nakuru kuelekea Tipis, Mau Narok kwenye kampeni za Rais Uhuru Kenyatta, kuanguka katika Ziwa Nakuru.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini Kenya (KCAA), Gilbert Kibe, helikopta hiyo ilikuwa na watu watano akiwamo rubani wake Bootsy Mutiso.
“Hadi sasa hakuna tena matumaini ya kupata majeruhi kwa sababu helikopta hiyo imezama kwenye ziwa hili na juhudi za uokozi zinaendelea kwa kuleta boti kutoka Ziwa Naivasha, ila sasa ndege zinapita juu kuangalia iwapo wataona chochote na kusaidia,” alisema Kibe.
Alisema katika ziwa hilo la Nakuru hakukuwa na boti karibu hivyo imebidi boti itoke Naivasha ambako ni mbali na hivyo uwezekano wa kuwapata waathirika wakiwa hai ni mdogo.
Kibe alisema katika helikopta hiyo mbali ya rubani, kulikuwa na wanaume watatu na mwanamke mmoja ambao hata hivyo hadi jana jioni majina yao yalikuwa hayajatambuliwa. Alisema helikopta hiyo inamilikiwa na Kampuni ya Flex Air Charters.
Awali Seneta wa Nakuru, Susan Kihika alisema abiria watatu kati ya hao wanne ni watumishi wenzake katika kitengo cha mawasiliano. Alisema helikopta hiyo ilianguka muda mfupi baada ya kuruka kutoka Jarika Kaunti na mashuhuda wengine wanasema waliiona ikiruka umbali wa chini kabla ya kuanguka.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kitengo cha Taifa cha Maafa, Pius Masai alisema wametuma helikopta moja ya Polisi kwenda kusaidia uokozi. “Pia tumetuma wazamiaji kutoka Jeshi la Wanamaji la Kenya wasaidie kutafuta helikopta hiyo iliyozama ziwani,”alisema Masai.
Baada ya kutokea kwa ajali hiyo viongozi mbalimbali walifika kwenye ziwa hilo akiwemo Gavana wa Nakuru, Lee Kinyanjui na viongozi wengine wakiwemo wabunge wa eneo hilo.
Wabunge hao ni Samuel Arama ( Nakuru Magharibi), David Gikaria (Nakuru Mashariki), Jayne Kihara (Naivasha) na Liz Chelule (Mwakilishi wa wanawake). Pia alikuwepo Spika wa Kaunti ya Nakuru, John Kairu.

AGUERO AREJEA UWANJANI

Image result for photo of sergio aguero

Sergio Aguero amefungia Manchester City mabao 176 - amepungukiwa na moja tu kufunga rekodi.
Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero amerejea mazoezini siku 11 baada yake kuvunjika ubavu katika ajali ya barabarani mjini Amsterdam.
Aguero, 29, alikuwa ametarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa wiki kadha
Hata hivyo, alirejea kufanya mazoezi mepesi Jumanne.
City wamesema mchezaji huyo wa Argentina ataendelea "kuimarisha hali yake ya mwili siku zijazo akilenga kurejea kikosini".
Aguero anahitaji bao moja pekee kufikia rekodi ya ufungaji mabao City ya Eric Brook ambayo ni mabao 177.
City wanaongoza Ligi ya Premia kwa wingi wa mabao, mbele ya Manchester United, na watakutana na Stoke siku ya Jumamosi.
Aguero alijeruhiwa akiwa kwenye teksi akisafiri baada ya kuhudhuria tamasha ya muziki. Teksi hiyo iligonga boriti ya taa barabarani.
Alikuwa ameenda Amsterdam kumuona nyota wa muziki kutoka Colombia Maluma akitumbuiza.

BAADA YA SULUHU POVU LAMWAGIKA KATI YA MORINHO NA KLOPP

Image result for photo from the match liverpool vs manchester united 2017
 Baada ya matokeo ya 0-0, Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp ametoa povu akituhumu mbinu za mpinzani wake, Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho kwa kusema kuwa yeye hawezi kutumia mbinu hizo.
Mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Anfield ulishuhudia United ikicheza muda mwingi ikiwa inazuia huku Liverpool ikishindwa kupenga ngome ya wapinzani wao hao.
Klopp amesema kuwa mbinu hizo za kuzuia yeye hawezi kuzitumia kwa kuwa hazimfai.
“Nafikiri sisi tulistahili kupata pointi tatu, tulicheza vizuri, nafikiri Man United walikuja kutafuta pointi hapa na wameipata, sisi tulitaka pointi tatu hatujazipata,” alisema Klopp ambaye alionyesha kutofurahia mbinu za wapinzani wake kupaki basi.

Image result for PHOTO OF SIMON MSUVA IN MOROCCO
Simon Msuva ameendelea kuwa na mwendelezo mzuri katika maisha yake ya soka la kulipwa,  hiyo ni baada ya kutengeneza bao moja katika ushindi wa mabao 2-0 wa timu yake Difaa Hassan El Jadida dhidi ya Chabab Rif Hoceima kwenye Uwanja wa Ben Ahmed El Abdi mjini El Jadida.
Msuva alipiga krosi katika dakika ya 64 katika mchezo wa Kombe la Ligi Morocco ikatua kichwani kwa Adnane El Ouardy akaudondoshea mpira nyavuni kuipatia bao la kwanza Jadida, kabla ya Hamid Ahadad kufunga la pili dakika ya 89.
Hivyo, Jadida metinga Nusu Fainali kwa ushindi wa jumla wa 3-2, baada ya wiki iliyopita kufungwa 2-1 Uwanja wa Mimoun Al Arsi mjini Al Hoceima, siku ambayo Msuva aliifungia timu yake bao muhimu la ugenini.
Katika mchezo huo wa wikiendi hii ya jana, Msuva alipumzishwa dakika ya 92 na nafasi yake kuchukuliwa na Tarik Astati.
Baada ya mchezo huo, Difaa ambayo ina viporo viwili dhidi ya FUS Rabat na Wydad Cassablanca, itamenyana na FAR Rabat Uwanja wa Prince Moulay Abdallah mjini Rabat

VICTOR MOSSES NJE YA UWANJA KWA MWEZ MMOJA

Image result for PHOTO OF VICTOR MOSES

Siku chache tangu wapate kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Crystal Palace, wimbi la majeruhi limeendelea kuitesa Chelsea baada ya Victor Moses naye kuingia kwenye orodha ya majeruhi sambamba na N'Golo Kante na Morata.
Moses ameanza mechi saba katika michuano yote msimu huu, lakini Mnigeria huyo atakuwa nje kwa sababu ya majeraha ya misuli.
Mchezaji huyo alitolewa Chelsea ikichezea kichapo cha 2-1 dhidi ya Crystal Palace wikiendi iliyopita, na kwa mujibu wa The Telegraph, Moses atakuwa nje ya dimba hadi baada ya mapumziko ya kimataifa.
Majeraha ya Moses ni pigo kwa Chelsea kwani tayari wamempoteza N'Golo Kane na Alvaro Morata ambao ni majeruhi pia.
Morata anaweza kurejea kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Roma Jumatano usiku, lakini Kante atakuwa nje hadi mwanzoni mwa mwezi ujao.

CAVANI AOMBA KUSAJILIWA MAN CITY

www.kwanguleo.blogspot.com

Mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Edinson Cavani kwa mujibu wa habari ameiomba Manchester City kumsajili.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay mustakabali wake Parc de Princes umekuwa wa mashaka baada ya kuwa na mvutano dimbani baina yake na Neymar mwezi uliopita.
Katika kipidi cha pili cha mechi ambayo PSG walishinda 2-0 dhidi ya Lyon Septemba 17, Cavani na Neymar walikuwa wakigombea kupiga penalti, ambayo hata hivyo Cavani aliikosa.
Kwa mujibu wa Don Balon, mshambuliaji huyo wa zamani wa Napoli anaamini atakuwa tishio mbele ya goli kwa Man City na anaitegemea timu hiyo ya Guardiola kumsajili, lakini pia akiwa anazifikiria Real Madrid, Manchester United au Everton.
Madrid wanataka kusajili mshambuliaji mpya na wanayo machaguzi mengi, kadhalika Cavani atakuwa na wakati mgumu kumpokonya namba Romelu Lukaku Old Trafford.
Everton watahitaji nguvu nyingi kumshawishi Cavani kutua Goodison kutokana na kiwango chao duni cha sasa, wakiwa chini mkiani mwa msimamo wa ligi. Hakuna taarifa zozote kama Manchester City wanafikiria kumsajili Cavani.

KOCHA MPYA MSAIDIZI WA ASIMBA ATAMBULISHWA

Klabu ya Simba imemtangaza Masudi Juma ria wa Burundi kuwa kocha wake msaidizi akichukua nafasi ya Jackson Mayanja.
Kocha huyo mpya aliwasili mchana wa leo nchini kwa ajili ya kusaini mkataba wa kufundisha Simba akisaidiana na Joseph Omog.
Baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) mjini Dar es Salaam, Juma alisema: “Nimekuja kuwa kocha Msaidizi wa Simba chini ya kocha aliopo kwa sasa. Nataka kusaidia Simba ifanikiwe kutwaa mataji zaidi, najua hiyo ndiyo kiu kubwa.”
Kocha huyo ambaye mwaka 1995 aliichezea Burundi katika michuano ya Vijana ya Dunia ya FIFA nchini Qatar alionekana kuwa mchangamfu katika mazungumzo yake.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Prince Louis ya Burundi, Inter Star za Burundi na Rayon Sport ya Rwanda amesema anafurahi kuja kufundisha Simba timu kubwa Afrika na anaamini atajifunza zaidi, hususan akifanya kazi chini ya kocha mzoefu zaidi, Omog.
Masudi Juma amesema atasaini mkataba na Simba kesho Ijumaa.

LIGI KUU BARA INAENDELEA LEO


www.kwanguleo.blogspot.comLigi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), inatarajiwa kuendelea leo Ijumaa Oktoba 20, 2017 kwa mchezo mmoja utakaokutanisha timu za Mwadui na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mwadui mkoani Shinyanga.
Timu hizo zinakutana katika Raundi ya Saba katika duru hili la kwanza la VPL ambalo mbali ya Kampuni ya Simu ya Vodacom - wadhamini wakuu, wadhamini wengine ni Kituo cha Televisheni cha Azam (Azam Tv) na Benki ya KCB ambayo huduma zake za kibenki zinazidi kushamiri nchini.
Wadhamini hao wanachagiza ligi hiyo ambayo itaendelea Jumamosi Oktoba 21 kwa michezo sita  itakayofanyika kwenye viwanja tofauti huku mechi nyingi zikipata fursa ya kuonyeshwa kwenye chaneli mbalimbali za Azam Tv kupitia king’amuzi cha Azam.
Michezo ya Jumamosi itakutanisha timu za Mbao na Azam kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, wakati Lipuli itakuwa mwenyeji wa Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa ilihali Ruvu Shooting watakuwa wageni wa Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Jumamosi hiyo hiyo Simba yenye mabadiliko kidogo kwenye benchi la Ufundi, itawaalika Njombe Mji kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam huku Ndanda ikicheza na Singida United kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Wakati Jumamosi hiyohiyo tena, Mtibwa Sugar wakicheza na Tanzania Prisons ya Mbeya kwenye Uwanja wa Manungu mkoani Morogoro, Jumapili kutakuwa na mchezo mmoja tu - ambao ni kati ya Stand United na mabingwa watetezi, Young Africans ya Dar es Salaam - mchezo utakaopigwa Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

9 WANG'OKA ACT WAKIMBILIA CCM


ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa chama cha siasa cha ACT Wazalendo, Samson Mwigamba na wenzake tisa, wamejivua uanachama wa chama hicho na kutangaza kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mwigamba alieleza hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, na kuongeza kuwa wamefikia uamuzi huo baada ya kuona uongozi wa sasa wa ACT Wazalendo unachepuka kwa kasi mno nje ya chama tofauti na matarajio yaliyokuwepo. Alisema wameondoka ACT Wazalendo na kujiunga na CCM kwa kuwa ndicho chama kinachoakisi kwa karibu itikadi, falsafa na sera za chama walichotoka.
“Tumejiridhisha kuwa mpangilio wa sasa wa CCM na serikali yake upo katika misingi hii, na Serikali ya Awamu ya Tano ya Dk John Magufuli inaitekeleza misingi hii kwa utashi mkubwa mno,” alieleza Mwigamba na kuongeza: “Tumeamua kujiunga na CCM ili tuendelee kuwa sehemu ya mapambano ya kurudisha nchi katika misingi yake kama ambavyo tulidhamiria ndani ya chama chetu cha zamani.”
Alisema pia wamekwenda CCM kwa kuwa Serikali ya Magufuli ipo katika vitakubwa dhidi ya rushwa na ufisadi, na hivi sasa Tanzania ni kinara wa mapambano dhidi ya rushwa. “Lakini sasa upinzani ambao ndiyo uliasisi vita dhidi ya ufisadi umegeuka kuwa ndiyo watetezi wa mfumo wa kinyonyaji ulioitesa nchi kwa miaka mingi. Sisi tumeamua kujitenga na aina hii ya upinzani,” alifafanua Mwigamba.
Alisema wameamua kujitenga na upinzani unaokerwa na mafanikio ya serikali, kwa kuwa tangu wanachama wenzao Profesa Kitila Mkumbo na Anna Mghwira walipoteuliwa na Rais John Magufuli, kufanya kazi katika utumishi wa umma serikalini, wamekuwa wakikerwa na kutishwa katika utekelezaji wa majukumu yao, hususan wanapoelezea mafanikio ya serikali.
Profesa Mkumbo ambaye alikuwa Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo, aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Aprili 4, mwaka huu, kuchukua nafasi ya Mhandisi Mbogo Futakamba ambaye amestaafu. Kwa upande wake, Anna Mghwira ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho na mgombea urais wa ACT-Wazalendo katika uchaguzi mkuu wa 2015, aliteuliwa Kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Juni mwaka huu, kuchukua nafasi ya Said Mecky Sadiki aliyejiuzulu.
Mwigamba alikuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kuanzisha ACT Wazalendo, na alijiunga nayo mwaka 2014. Alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo ya Katibu Mkuu wa chama, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kampeni na Uchaguzi.
Ofisa Habari wa chama hicho, Abdalah Khamis alisema Mwigamba aliandikiwa barua ya kuitwa leo ili aseme ni sehemu gani ambayo misingi ya chama hicho ilikiukwa. “Aliandikiwa barua aje atoe ufafanuzi nini kimekiukwa na kipi kiboreshwe. Kama kiongozi alitakiwa azungumze. Hatujui analalamikia nini kwa kuwa alikuwa na nafasi ya kueleza hilo kwenye Kamati ya Uongozi,” alisema Khamis, na kusikitishwa na Mwigamba kwa kuwatambulisha wanachama wengine waliohamia CCM kuwa walikuwa viongozi, akidai hawakuwa hivyo.

USHIRIKIANO WA CHINA WAZIDI KUKUA



RAIS wa China, Xi Jinping amefungua Mkutano Mkuu wa 19 wa Chama tawala cha Kikomunisti (CPC) na kuahidi nchi hiyo haitafunga milango ya ushirikiano na nchi nyingine duniani bali kuuendeleza zaidi.
Mkutano huo unaofanyika wakati Rais huyo akimaliza awamu ya kwanza ya kipindi cha utawala cha miaka mitano. Alitumia saa tatu na nusu kuelezea mafanikio aliyopata ikiwemo kuongeza pato la Taifa. Rais JinPing alisema wakati akiingia madarakani mwaka 2012, alikuta Pato la Taifa la China likiwa ni fedha za nchi hiyoYuan trilioni 54 kwa mwaka na sasa pato hilo ni karibu Yuan trilioni 80.
Inaelezwa kuwa kuongezeka kwa pato hilo la taifa kunaashiria nchi hiyo kufikia lengo lake la kuwa taifa lenye uchumi mkubwa duniani. Mbali na kuongeza Pato la Taifa, pia amejivunia kuwaondoa wananchi wa nchi hiyo ya pili kwa uchumi mkubwa duniani zaidi ya milioni 60 katika hali ya umaskini kwa kipindi hicho cha miaka mitano.
Mkutano huo wa siku nne unatarajiwa kutoa mrithi wa nafasi ya urais kama katiba ya chama hicho inavyosema kuwa baada ya miaka mitano, rais aliyepo madarakani anapaswa kumtangaza mrithi wake pamoja na kuchagua viongozi wengine wa ngazi mbalimbali wa chama hicho watakaoongoza nchi hiyo. Katika mkutano huo unaofuatiliwa na watu mbalimbali duniani, mageuzi ya Katiba ya chama hicho yanayolenga kukabiliana na mabadiliko ya mazingira na hali ilivyo kwa sasa yaliwasilishwa rasmi.
“Uzoefu unaonesha kufanya marekebisho ya katiba ya chama kwa maendeleo endelevu na majukumu yaliyopo itasaidia kila mwanachama kuelewa, kutumia na kutekeleza katiba ya chama,” alisema Rais Xi. Katika suala la ushirikiano na nchi mbalimbali duniani, Rais Xi alisema wataendelea kuheshimu uhuru wa mataifa rafiki na kudumisha uadilifu wa mipaka wa mataifa huku wakiandaa mipango ya ushirikiano na kuendeleza miradi ya ushirikiano kwa kutumia majadiliano.
“China itafungua milango ya bidhaa kutoka mataifa rafiki na kulinda haki za kimsingi za wawekezaji wa nje,” alisema. Alisema uchumi wa nchi hiyo umekuwa ukibadilika kutoka kukua kwa kasi hadi kiwango cha ubora wa hali ya juu kimaendeleo kwa kuendeleza uchumi wa kisasa hivyo lazima wazingatia hali halisi ya uchumi wa ndani.
Alisema Serikali yake itawezesha mtaji wa taifa kuwa thabiti, imara na kukua zaidi na kuwezesha kampuni za uwekezaji kutoka China kufikia viwango vya kimataifa na ushindani mkubwa ulimwenguni. “China itazingatia jukumu lake la kutumia bidhaa zinazozalishwa nchini humo na kuboresha mfumo wa usimamizi inayounganishwa na sera ya fedha,”alisema. Katika kukiimarisha chama, alisema kitaendelea kuimarisha vita dhidi ya vitendo vya rushwa na kuhakikisha wanapata ushindi katika vita hivyo.
Alisema katika mfumo wa utawala wa ujamaa, wanazingatia itikadi za Kichina pamoja na kuwa na taifa linalotekeleza mfumo wa kikomunisti. Mkutano huo ulioanza jana, unajumuisha wajumbe zaidi ya 2,307 wanaotoka katika ngazi mbalimbali za kijamii kutoka taaluma na nyanja mbalimbali wakiwemo wachumi, sayansi na teknolojia, ulinzi na usalama, mahakama, elimu, utamaduni, michezo, wakulima na viongozi mbalimbali katika jamii. Pia watachagua viongozi katika kamati mbalimbali za maamuzi za CPC yenye wanachama wanaokadiriwa kuwa milioni 89.44 kwa mujibu wa takwimu zao za mwaka jana.

NDALICHAKO ALILIA AJIRA KWA VIJANA




WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema kutokana na ongezeko la ukosefu wa ajira hususani kwa vijana nchini, kuna umuhimu wa kutengeneza mazingira kwa ukuaji wa biashara ili ajira nyingi zipatikane kiurahisi kwa vijana wanaomaliza elimu ya juu ili waweze kujiajiri.
Waziri huyo amebainisha jana Dar es Salaam kuwa kwa sasa Tanzania ina vijana wengi wenye umri wa miaka 15 hadi 34 ambao hawana ajira kutokana na kukosa ujuzi wa kupata ajira ambapo tatizo hilo kwenye miji mikubwa limefikia asilimia 22.3 ikilinganishwa na vijijini ambako ni asilimia 7.1. Alisema hayo wakati akizungumza katika uzinduzi wa Programu za Benki ya Barclays Tanzania zijulikanazo kama Twende Kazi na Balozi Mwanafunzi jijini Dar es Salaam jana.
Profesa Ndalichako alisema tatizo la ukosefu wa ajira linaongezeka kutokana na kutokuwapo kwa uwiano wa ugavi na mahitaji kwenye soko la ajira pamoja na ongezeko la ajira kubakia kwenye sekta isiyo ya kilimo. “Kila mwaka wasichana na wavulana wanaingia kwenye soko la ajira na wanatokana na wahitimu wa sekondari na elimu ya juu ambao wamehama kutoka vijijini kuja mjini kutafuta ajira,” alisema.
Alisema kiwango hicho cha ukosefu wa ajira nchini kinapimwa na idadi ya watu, vijana wasomi wanaotafuta ajira kama asilimia kubwa ya nguvu kazi hali inayosababisha kuwepo na umuhimu wa kutengeneza mazingira mazuri kwa ukuaji wa biashara nchini ili ajira nyingi zipatikane kwa urahisi. Aliishukuru Benki ya Barclays kwa kuwa mstari wa mbele kuisaidia Serikali na jamii katika kuhakikisha tatizo la ukosefu wa ajira linatatuliwa na kupungua kwa kiwango kikubwa kwa kuwawezesha vijana.
Alisema katika miaka 15 ya uwepo wake sokoni, benki hiyo imechukua hatua kupitia mfumo wake wa Shared Growth unaoenda sambamba na Programu ya Twende Kazi, kuwasaidia wahitimu 200 watakaowekwa katika mafunzo ya kujiandaa na soko la ajira katika kampuni mbalimbali nchini kupitia utendaji kazi wa kampuni isiyo ya kiserikali ya Junior Achievement Tanzania ili kupata walio bora zaidi. Alisema pamoja na kutatua tatizo la ajira, benki hiyo pia imesaidia wanafunzi wasio na uwezo wa kujikimu na ada na mahitaji ya chuo kupitia Programu ya Balozi Mwanafunzi ambapo wanafunzi 23 wa mwaka wa kwanza hadi wa nne watasomeshwa miaka mitatu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

MAKUBALIANO YA AWALI KATI YA TANZANIA NA KAMPUNI YA BARRICK GOLD YAONYESHA MWANZO MZURI


RAIS John Magufuli amesema kufikiwa makubaliano kati ya Tanzania na Kampuni ya Barrick Gold Corporation ni mwanzo mzuri, na kwamba Tanzania inaweka mwelekeo ambao haujawahi kuwekwa kokote barani Afrika katika udhibiti wa rasilimali zake.
“Sasa Barrick ni ndugu zetu, msikubali mazungumzo tuliyoyaanza kuingiliwa na watu wengine, tumeweka mwelekeo ambao haujawahi kufanyika popote Afrika, huu ni mwanzo wa kutengeneza Tanzania mpya,” alisema Rais Magufuli. Alitoa kauli hiyo jana Ikulu, Dar es Salaam, wakati wa kutiwa saini kwa makubaliano baada ya Kamati maalumu ya mazungumzo baina ya timu ya wataalamu wa Tanzania na Kampuni ya Barrick Gold Corporation kukamilika.
Katika hafla hiyo iliyofanyika baada ya mazungumzo hayo yaliyochukua takribani miezi mitatu kukamilika, Waziri wa Sheria na Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya mazungumzo aliongozana na baadhi ya wajumbe wake, pamoja na Mwenyekiti Mtendaji wa Barrick, Profesa John Thornton.
Akizungumza baada ya kutiwa saini kwa makubaliano hayo ambayo Kampuni ya Barrick imekubali kulipa Dola za Marekani milioni 300 (zaidi ya Sh bilioni 700), kama malipo ya kuonesha nia njema ya kufidia fedha zilizotokana na upotevu wa mapato kupitia biashara ya kampuni hiyo, Rais Magufuli alisema huo ni mwanzo mzuri.
“Huu ni mwanzo nzuri wa kutengeneza Tanzania mpya na sasa Barrick ni ndugu zetu tumeanza mazungumzo vizuri na tumefikia hatua nzuri ambapo wamekubali kutoa dola milioni 300, wametambua msimamo wetu ndiyo faida ya mazungumzo,” alisema Rais Magufuli. Aidha, Rais Magufuli ameafiki kuundwa kwa kamati ndogo itakayohusisha pande zote mbili za mazungumzo ili kupitia nyaraka zote za malipo na kuangalia maeneo yenye utata ili kuangalia jinsi ya kutafuta suluhu.
“Chochote kinawezekana kinachohitajika ni uaminifu kati ya pande mbili, tutafikia muafaka kwa mazungumzo, ila wamefahamu kuwa hatutaki kuchezewa tena, tumekuwa shamba la bibi kwa muda mrefu, sasa basi,”alisema Rais Magufuli. Mbali na kusifia hatua ya mazungumzo iliyofikiwa na pande zote mbili, Rais Magufuli aliitaka kampuni hiyo ya Barrick kuwasilisha fedha hizo haraka kwa sababu zina kazi ya kufanya na kusisitiza kuwa nchi itaendelea kulinda rasilimali zake zote kwa faida ya Watanzania.
Alisema pamoja na kampuni hiyo kukubali kulipa kianzio cha fidia ya biashara ya madini, pia wamekubali kuanzia sasa Tanzania itakuwa ikipata nusu ya faida ya biashara ya kampuni hiyo ya madini ya dhahabu sambamba na kumiliki hisa kwa asilimia 16. Mbali na kulipa faida na nchi kumiliki hisa hizo, Rais Magufuli alisema kampuni hiyo pia itaendelea kulipa kodi nyingine kama kawaida zikiwemo za halmashauri pamoja na menejimenti ya kampuni hiyo itaundwa kwa kuwahusisha pia Watanzania.
Akizungumzia suala la kuundwa kwa menejimenti ya kampuni hiyo itakayowashirikisha Watanzania, Rais Magufuli alitoa mwito kwa vyombo vitakavyohusika na usaili wa watu wenye sifa, kuangalia kwa makini tabia na mwenendo wao, ili kuhakikisha wanapatikana watu waadilifu na siyo wezi.
“Tumesikia katika makubaliano yao menejimenti mpya ya Kampuni ya Barrick sasa itaundwa kwa kuzingatia watu wa Tanzania, sasa hii ni faida kwetu labda tuweke majizi, ila nitoe rai kwa vyombo vitakavyohusika kutafuta watu wenye sifa, kuhakikisha wanawachunguza kwa undani na kujua tabia zao ili wapatikane watu sahihi kwa faida ya nchi,” alisisitiza Rais Magufuli.
Akiipongeza kamati hiyo, Rais Magufuli alisema imefanya kazi yake kwa weledi mkubwa na uzalendo kwani walikuwa na uwezo wa kupindisha mambo au kula rushwa, lakini wamekuwa waaminifu kwa faida ya taifa.
“Naipongeza kamati, mngeweza kukaa kimya au kula rushwa lakini pamoja na ukubwa wa wajumbe wa Barrick ambao nasikia walifika 25 na nyie mko nane, lakini mmeonesha uwezo wenu mkubwa na nidhamu, na wametambua jambo hili siyo jepesi na mmefikia hatua nzuri, nitaandaa siku ya kuwapongeza hata kwa kuwapa cheti kwa kuwa mmejitolea maisha yenu,” alisema Rais Magufuli.

WAZIRI ATOA PONGEZI KWA NSSF NA PPF KWA UWEKEZAJI


WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa (pichani) amepongeza hatua ya mifuko ya hifadhi ya jamii nchini kuwekeza kwenye sekta ya viwanda huku akitoa mwito kwa jamii hususani vijana kuhakikisha wanaonesha uzalendo kwa kujitolea kwa vitendo kuunga mkono jitihada hizo zinazolenga kutatua tatizo la ajira na kuinua uchumi wa taifa.
Majaliwa alitoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki mkoani hapa baada ya kuongoza upandaji wa miwa ikiwa ni ishara ya kuunga mkono mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha sukari unaofahamika kama Mkulazi II, unaotekelezwa kwa ubia kati ya mifuko ya hifadhi ya jamii ya NSSF na PPF kupitia Kampuni Hodhi ya Mkulazi Holding unaofanyika katika Gereza la Mbigiri, Dakawa wilayani Mvomero mkoani Morogoro.
“Pamoja na kutoa pongezi kwa mifuko yetu ya hifadhi ya jamii hapa nchini kwa kuitikia vema wito wa Serikali ya Awamu ya Tano katika uwekezaji wa viwanda vyenye tija kwa taifa, kipekee nitoe wito kwa jamii hususani vijana kuhakikisha wanaunga mkono jitihada hizi kwa kujitolea ujuzi na maarifa katika kufanikisha azma hii ya serikali inayolenga kuwanasua kutoka kwenye uhaba wa ajira,” alieleza


MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imepanga Oktoba 19 hadi 23 mwaka huu kuanza kusikiliza kesi ya mauaji bila kukusudia ya aliyekuwa nguli wa fi lamu nchini, Steven Kanumba inayomkabili mwigizaji wa fi lamu maarufu nchini, Elizabeth Michael “Lulu” (pichani).
Lulu aliye nje kwa dhamana atapanda kizimbani mahakamani hapo baada ya kusomewa maelezo ya awali karibu miaka miwili na nusu iliyopita. Msanii huyo anakabiliwa na kesi hiyo akidaiwa kumuua Kanumba bila kukusudia kinyume cha Kifungu cha 195 cha Kanuni za Adhabu.
Inadaiwa Lulu alimuua Kanumba bila ya kukusudia Aprili 7, 2012 nyumbani kwa marehemu huyo Sinza Vatican, Dar es Salaam. Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya kesi za mauaji ya bila kukusudia iliyotolewa na Mahakama Kuu Dar es Salaam jana, kesi hiyo itasikilizwa siku hizo na Jaji Sam Rumanyika. Kesi hiyo inaanza kusikilizwa baada ya kupangiwa Jaji kufuatia upelelezi kukamilika.
Mara ya kwanza Lulu alipandishwa kizimbani Aprili 11, 2012 mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Jijini Dar es Salaam wakati huo, Augustina Mbando ambapo alisomewa mashitaka ya mauaji.
Hata hivyo, Februari 18, 2014 akisomewa maelezo ya awali Lulu alikiri mahakamani kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kanumba na pia kusema kulikuwepo ugomvi baina yao siku ya tukio la kifo cha mwigizaji huyo.
Lulu aliachiwa kwa dhamana Januari 29, 2013 baada ya kesi hiyo kubadilishwa hati ya mashitaka kutoka kwenye kesi ya mauaji kwenda mauaji ya bila kukusudia ambapo badiliko hilo lilimpa nafasi ya kupata dhamana.
Katika kesi ya msingi namba 125 ya mwaka 2012, inadaiwa Aprili 7, 2012 Sinza Vatican Lulu alimuua Kanumba bila kukusudia. Lulu alipelekwa rumande gereza la Segerea hadi mashitaka yalipobadilishwa akapata dhamana.