RONALDO ASHINDA TUZO ZA FIFA AKIWABWAGA MESSI NA NEYMAR JR

Staa wa Ureno, Cristiano Ronaldo amefanikiwa kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Fifa kwa mwaka 2017 kwa mara ya pili mfululizo tangu kureshwa kwa utaratibu wa tuzo huo, mwaka jana.
Ronaldo amekabidhiwa tuzo hiyo jijini London kulipofanyika sherehe za utoaji wa tuzo hiyo ambapo amewapiga bao Lionel Messi wa Barcelona na Neymar PSG.
Tuzo hiyo ambayo iliwepo miaka ya nyuma ilipotea baada ya kuungana na ile ya Ballond’Or lakini mwaka jana Fifa iliamua kujiweka pembeni na kuendelea kuratibu tuzo zake kama zamani huku wale wengine nao wakiendelea na tuzo yao.
Wakati Ronaldo akikabidhiwa tuzo hiyo, kocha wake wa Real Madrid, Zinedine Zidane yeye amepewa tuzo ya Kocha Bora wa Mwaka

No comments: