Kenyatta ambaye amekuwa akishinikizwa na wadau mbalimbali kukutana na afisa huyo pamoja na mgombea urais wa muungano wa NASA, Raila Odinga, ili kutatua mzozo wa kisiasa unaoendelea kuikabili nchi hiyoAidha, baada ya mkutano huo, Kenyatta ametuma taarifa kwa vyombo vya habari iliyosema kuwa yeye hana masharti yoyote kwa tume hiyo, isipokwa tu kwamba uchaguzi ufanyike siku ya Alhamisi kama ilivyoagizwa na mahakama ya juu
“Msimamo wangu ni ule ule, Wakenya wapewe nafasi ya kushiriki kwenye zoezi la kidemokrasia la kupiga kura kama tu ilivyoagizwa na mahakama ya juu. hatuna masharti yoyote kwa IEBC,” amesema Kenyatta