VICTOR MOSSES NJE YA UWANJA KWA MWEZ MMOJA

Image result for PHOTO OF VICTOR MOSES

Siku chache tangu wapate kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Crystal Palace, wimbi la majeruhi limeendelea kuitesa Chelsea baada ya Victor Moses naye kuingia kwenye orodha ya majeruhi sambamba na N'Golo Kante na Morata.
Moses ameanza mechi saba katika michuano yote msimu huu, lakini Mnigeria huyo atakuwa nje kwa sababu ya majeraha ya misuli.
Mchezaji huyo alitolewa Chelsea ikichezea kichapo cha 2-1 dhidi ya Crystal Palace wikiendi iliyopita, na kwa mujibu wa The Telegraph, Moses atakuwa nje ya dimba hadi baada ya mapumziko ya kimataifa.
Majeraha ya Moses ni pigo kwa Chelsea kwani tayari wamempoteza N'Golo Kane na Alvaro Morata ambao ni majeruhi pia.
Morata anaweza kurejea kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Roma Jumatano usiku, lakini Kante atakuwa nje hadi mwanzoni mwa mwezi ujao.

No comments: