Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameidhinisha mswada wa bajeti ndogo ambapo ametenga Kiasi cha shilling za Kenya 12 bilioni (Dola 120 milioni) za kutumiwa na Tume ya Uchagizi katika uchaguzi mkuu mpya tarehe 26 Oktoba.
Kadhalika, kutengwa kwa Kshs 25 bilioni za kutumiwa kufadhili mpango wa elimu ya sekondari bila malipo ambao Rais Kenyatta alikuwa ameahidi kwenye kampeni kwamba utaanza kutekelezwa Januari mwaka ujao.
Aidha, kuna Kshs 6.7 bilioni za kufadhili ununuzi wa mahindi kuhakikisha kuuzwa kwa unga wa bei nafuu.