WASIRA AIKOSOA SERIKALI

Aliyekuwa Mbunge wa Bunda na waziri wa serikali za awamu zilizopita mhe Stephen Wasira amesema si kosa la jinai kuikosoa Serikali bali kuitukana serikali ndio kosa kwa mujibu wa sheria za nchi.


Hata hivyo Wasira amesema watu waikosoe Serikali kwa hoja na sio kutukana hivyo haoni sababu yeyote ya watu kuikosoa Serikali tena kwa hoja alafu wakamatwe,ameongeza kuwa ipo tofauti kubwa kati ya kukosoa na kutukana.

Amezungumzia pia kuhusu viongozi wa upinzani wanaokamatwa ara kwa mara na vyombo vya dola pale wanapoikosoa Serikali, ameongeza kuwa ni sawa wakamatwe lakini wapelekwe mahakamani , mahakama ndio inaweza kuamua haki kwa mujibu wa sheria kuwa kama kuna kosa au hakuna kosawww.kwanguleo.blogspot.com/mpya

No comments: