SERIKALI YAONGEZA UMRI WA KUSTAAFU



SERIKALI ya Tanzania iko katika mchakato utakaowezesha kuongeza muda wa kustaafu kwa watumishi wenye elimu ya ngazi ya uprofesa, watafi ti na wataalamu wengine ili kuwapa muda zaidi wa kutumia taaluma zao kwa manufaa ya taifa.
Aidha, imesema inalifanyia kazi suala ya watumishi walioondolewa kazini kwa kukosa sifa ikiwemo kutokuwa na vyeti vya kidato cha nne kama ambavyo sheria inavyohitaji na kulipatia suluhu kwa kuwa wengi hawana mshahara.
Imesema watumishi wengi wa umma hulipwa mshahara kwa kufanya kazi kwa kati ya asilimia 30 hadi 50 huku ikiwa ni wachache sana wanaoweza kulipwa kwa kufanya kazi kwa asilimia 100, jambo ambalo litasimamiwa kikamilifu.
Kadhalika imesisitiza itaendelea kuwachukulia hatua za kisheria watu wanaoghushi sifa za kitaaluma na taarifa binafsi wakati wa kuomba kazi, kwa kuwa baadhi ya waomba ajira wameendelea kufanya hivyo.
Waziri wa Nchi, Ofi si ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika alisema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akipokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Ofi si za Sekretarieti ya Ajira katika utumishi wa umma iliyowasilishwa kwake na Katibu wa Sekretarieti hiyo, Xavier Daudi.
Kuhusu wastaafu, Mkuchika alisema katika vyuo vikuu mbalimbali nchini wapo maprofesa na watafi ti wengi ambao umri wao wa kustaafu umefi ka ama unakaribia kufi ka huku wakiwa bado na nguvu ya kuweza kuendelea kulitumikia Taifa.
“Wataalamu hao wanatakiwa kustaafu wakiwa na miaka 60 kwa mujibu wa sheria, lakini serikali iko katika mchakato kuongeza muda wao angalau hadi miaka 65 kwa kuwa yapo maeneo ambayo ni lazima kuongeza muda wa kustaafu,” alisema Mkuchika.
Alitoa mfano wa taaluma hizo kuwa ni pamoja na wasomi wa ngazi ya uprofesa, watafi ti ambao wengi hufi kia kuwa wabobezi katika maeneo hayo wakiwa na miaka kati ya 50 huku wakitakiwa kutumia kwa miaka 10 kabla ya kustaafu, jambo ambalo huonekana bado wakiwa na nguvu.
Nchi nyingine za Afrika Mashariki za Uganda, Rwanda na Burundi wastani wa umri wa kustaafu ni miaka 60, ukiachilia mbali Kenya ambayo ni miaka 55 na ilikuwa imeanzisha mchakato wa kwenda miaka 60.
Mkuchika alisema Serikali imeanzisha vyuo mbalimbali vikuu na suala hilo la kustaafu kwa watumishi hao litaangaliwa ili utaalamu walio nao uweze kuandelea kuangaliwa. Kuhusu watumishi walioondolewa kwa kukosa vyeti vya kidato cha nne, alisema kuanzia mwaka 2004, sheria ya ajira iliainisha mtumishi kuwa na sifa ya cheti ya kidato cha nne, lakini wapo watumishi ambao walikuwa wakitumika kwa bila kuwa na vyeti hivyo wakati wa kukaguliwa kwa vyeti.
Mkuchika alihoji, Ofi si za Sekretarieti ya ajira katika utumishi wa umma iwapo wapo watumishi wa aina hiyo, wanaagwa vipi na kwamba washirikiane kulipatia suala hilo ufumbuzi ama Halmashauri ziwape nauli waweze kurudi makwao kwa kuwa maisha ni magumu na hawana mshahara.
Akijibu suala hilo, Naibu Katibu, Ofi si ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Suzan Mlau aliahidi kulifanyia kazi suala hilo kwa kuwa watumishi hao wanakwenda ofi sini, lakini hakuna wanachokifanya zaidi wanakaa tuu.
Akizungumzia nidhamu kazini, Mkuchika amewataka watumishi wa Ofi si hiyo kwa ujumla kufanya kazi kwa kuwa ni kioo cha serikali, na atasimamia kwa hakika utendaji na muda wa kazi kwa kuwa wapo wananchi wanaofi ka katika ofi si hizo na kushindwa kupata huduma huku jengo hilo likilipiwa pango la Sh milioni 34 kila mwezi.
Awali, akisoma taarifa ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Daudi alisema tangu kuanzishwa kwa ofi si hiyo 2010, imeweza kupokea maombi 472,516 huku ikiwa imewapangia vituo vya kazi waombaji 23,676.
Hata hivyo, alisema ukosefu wa teknolojia za kisasa nchini inawafanya wadau kutumia vibaya mitandao hususani ya kijamii na kuamua kuandaa matangazo ya uongo ya ajira na kujifanya ni sekretarieti imetangaza kwa kutumia mitandao ya kijamii na kupotosha umm

No comments: