BAADA YA SULUHU POVU LAMWAGIKA KATI YA MORINHO NA KLOPP

Image result for photo from the match liverpool vs manchester united 2017
 Baada ya matokeo ya 0-0, Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp ametoa povu akituhumu mbinu za mpinzani wake, Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho kwa kusema kuwa yeye hawezi kutumia mbinu hizo.
Mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Anfield ulishuhudia United ikicheza muda mwingi ikiwa inazuia huku Liverpool ikishindwa kupenga ngome ya wapinzani wao hao.
Klopp amesema kuwa mbinu hizo za kuzuia yeye hawezi kuzitumia kwa kuwa hazimfai.
“Nafikiri sisi tulistahili kupata pointi tatu, tulicheza vizuri, nafikiri Man United walikuja kutafuta pointi hapa na wameipata, sisi tulitaka pointi tatu hatujazipata,” alisema Klopp ambaye alionyesha kutofurahia mbinu za wapinzani wake kupaki basi.

No comments: