MILLION 200 ZAKUSANYWA MNADA WA NG'OMBE


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina akiongea na waandishi wa habari kuhusu opareshei ondoa Mifugo leo katika ofisi za wizara hiyo jijini Dar es Salaam,Pembeni yake ni Naibu Waziri Abdalah ulega, kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo katika sekta ya Mifugo Dkt Maria Mashingo na kushoto ni Katibu Mkuu sekta ya Uvuvi Dkt. Yohana Budeba

Kupitia Amri ya Mahakama iliyoamuru kupigwa mnada kwa ng’ombe waliovamia toka nchi jirani ya Kenya, Serikali imekusanya zaidi ya Shilingi Milioni 200 baada ya ng’ombe hao kupigwa mnada katika wilaya ya Mwanga mwishoni mwa wiki.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpiga amesema Wizara yake imejipanga na kuendelea na Oparesheni maalum ya kukamata na kuondoa mifugo yote inayovamia  kutoka nchi jirani kupitia mikoa ya mipakani kama Katavi, Kigoma, Tanga, Mara,Ruvuma, na Arusha na kuagiza wakuu wa Mikoa na Wilaya hizo kuendesha Opresheni hizo Maalum ndani ya siku saba.
“Mimi , Naibu Waziri wangu, makatibu wakuu na wataalam tunaingia tena katika opareshi hiyo maalum kesho.” Alisisitiza Mpina
Aidha, Mpina alisema kuwa serikali haipo tayari kuingia gharama ya kutibu magonjwa yanayoletwa na mifugo wanaovamia kutoka nchi jirani ambao kwa namna moja au nyingine huleta uharibifu wa mazingira kwa kukata miti ovyo, kusababisha mmomonyoko wa udongo na kuchangia kwa kiasi kikubwa migogoro ya wakulima na wafugaji.
Mpina alisema, watu wenye nia mbaya wasihusishe Opareni hii na mahusiano ya nchi hizi mbili akitolea mfano mahusiano ya Kenya na Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa yapo kisheria.
Akizungumzia suala ya mifugo ya Tanzania kuwa na chapa Mpina alisema, suala hili linashughulikiwa na ifikapo Desemba mwaka huu litakuwa limekamilika na hivyo kurahisha oparesheni hizi za kuondoa mifugo vamizi.

No comments: