NILIPEWA KADI NYEKUNDU KIMAKOSA NEYMAR ASEMA


Image result for PHOTO OF NEYMAR JR IN PSG


Mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Neymar amedai kuwa kutolewa dimbani kwa kadi mbili za njano dhidi ya Marseille haikuwa haki.
Zikiwa zimebaki dakika tatu alipewa onyo kwa majibu yake baada ya kufanyiwa faulo na Lucas Ocampos, na Mbrazili huyo aliamrishwa kutoka dimbani timu yake ikiwa nyuma kwa mabao 2-1.
Mpira wa adhabu uliopigwa na Edinson Cavani dakika za majeruhi uliwawezesha miamba hao wa Ligue 1 kupata sare, lakini Neymar amekiri kuwa alikasirishwa na hatua zilizochukuliwa dhidi yake katika uwanja wa Velodrome.
Neymar, 25, amekiambia Esporte Interativo: "Nadhani mambo yalikuzwa, naam. Haikuwa haki. Mchezo wote nimekuwa nikichezewa rafu. Nina alama tele mwilini mwangu.
"Nilijaribu kuendelea kucheza baada ya kufanyiwa faulo. Lakini nilikerwa zaidi na maamuzi ya refa kwa kunitoa nje."
Licha ya sare hiyo, PSG ipo mbele kwa pointi nne dhidi ya timu inayoshika nafasi ya pili Ligue 1

No comments: