Alvaro Morata alifunga mabao matatu katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza uliopigwa hapo jana wakati Chelsea ikiibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Stoke City.
Morata alifunga bao la kwanza dakika ya 2 baada ya mchezo kuanza akipokea pasi nzuri kutoka kwa Cesar Azpilicueta kabla ya Pedro kufunga bao la pili dakika ya 30 kisha Morata akafunga dakika ya 70 na 82.
Hii ni hat-trick ya kwanza kwa Morata tangu ajiunge na Chelsea kwa ada ya pauni milioni 60 akitokea Real Madrid, mshambuliaji huyo anaonekana kuanza kuonyesha uwezo mkubwa ikiwa ni siku chache baada ya Chelsea kukubali kumuuza Diego Costa.