Kocha Mkuu wa klabu bingwa Tanzania bara Young Aficans, George Lwandamina, amemkabidhi Obrey Chirwa majukumu ya Amissi Tambwe ambaye kwa sasa ni majeruhi.
Chirwa amepewa majukumu hayo kutokana na Tambwe kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu akiuguza majeraha ya goti.
Kutokana na kuuguza majeraha hayo, ilisababisha Tambwe akose michezo mitano za kimashindano ambazo tayari Yanga imecheza ikiwa moja ya Ngao ya Jamii na nne Ligi Kuu Bara.