Wasanii maarufu wa Hip-hop, nchini Nigeria Peter na Paul Okoye, wanaounda kundi la Psquare kwa muda mrefu wamekuwa wakifanya vizuri katika muziki wao nchini humo wamevunja mkataba wa kundi hilo mara baada ya Peter Okoye kumtaka mwanasheria wao Festus, Kuvunja kundi hilo.
Peter amesema kuwa inaonekana kuwa ndugu yake Paul hayupo tayari kuendelea kufanya kazi na yeye kwani ameweza kusitisha ziara yao ya US bila ya kuweka sababu yeyote.
Ameongeza kuwa, Paul amekuwa akimtukana mkewe na watoto wake kupitia mitandao ya kijamii na kusema familia yake imekuwa ikitumiwa ujumbe uliokuwa ukiwatishia maisha