FUNGUA LINK HII UONE MAAJABU

http://MyWorkingHour.com/?userid=512046
Je!unapenda kutengeneza pesa basi link hii ni free unajiunga ukishamaliza subiri majibu ndani ya masaa 24

BILIONI MOJA YAWAPONZA POLISI SABA



1. E.4948 CPL Dani Isack Kasala
2. F.1331 CPL Matete Maiga Misana
3. G.1876 PC Japhet Emmanuel Lukiko
4. G.5080 PC Maingu Baithaman Sorrah
5. G.6885 PC Alex Elias Nkali
6. G.7244 PC Timoth Nzumbi Paul
7. H.4060 PC David Kadama Ngelela.

Aidha, kuhusu Afisa SSP: Moris Okinda ambaye alikuwa kiongozi wa askari hao walioomba na kupokea rushwa ya kiasi hicho cha fedha, mamlaka yake ya kinidhamu tayari imemsimamisha kazi na tayari amefikishwa mahakamani pamoja na askari hao.
Pamoja na askari hao, pia wamefikishwa mahakamani watuhumiwa wengine wa nne waliokamatwa huko Kigongo feri Wilayani Misungwi wakitorosha madini hayo ya dhahabu kutoka Tanzania kwenda Nchi jirani ya Rwanda.

Watuhumiwa waliokamatwa wakitorosha madini hayo ya dhahabu ni;
1. Sajid Abadalah Hassan, miaka 28, mfanyabiashara wa dhahabu, mkazi wa Ilala Dar es Salaam na Mwanza mtaa wa pamba ‘A’.
2. Kisabo Kija  Mkinda , miaka 55, mfanyabiashara wa dhahabu, mkazi wa mwatulole –Geita
3.Emmanuel Ntemi, miaka 63, dereva, mkazi wa kijiji cha mwatulole –Geita
4. Hassan Sadiq Hassan, miaka 28, Mhindi, Raia wa Pakistani, mkazi wa Mwanza mtaa wa Pamba ‘A’, Mfanyakazi wa duka la kuuza vito.
Kufuatia sakata hili, Jeshi la Polisi Tanzania kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na wanaendelea na uchunguzi wa kina ili tuweze kuwakamata watuhumiwa wote waliohusika kwa namna moja au nyingine katika sakata hili.

WAZIRI MHAGAMA ATINGA KIWANDA CHA VIATU.............ATOA AGIZO KWA VITENDAJI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama amewataka watendaji wa kiwanda cha Viatu na bidhaa za ngozi cha Karanga Wilaya ya Moshi kuzalisha bidhaa zenye ubora na kuendana na Soko lililopo nchini.
Ametoa kauli hiyo alipotembelea kiwanda hicho mwishoni mwa wiki ili kukagua shughuli za uendeshaji wa kiwanda hicho na kujiridhisha na ubora wa bidhaa zinazozalishwa.

“Niwatake watendaji kuweka mikakati madhubuti ya kuendelea kutengeneza bidhaa zenye ubora kwa kuzingatia viwango vinavyotatiwa”, Mhagama
Aidha Waziri aliwaasa watendaji wa kiwanda hicho kuendelea kutatua changamoto zinazowazunguka za kimfumo kwa kuzingatia sheria na taratibu za uendeshaji wa kiwanda hicho ili kuendana na ukuaji wa teknolojia na ushindani ulipo.

“Nisingependa kuona kiwanda kinakwama kuzalisha bidhaa zenye ubora, hivyo ni vyema kuzingatia sheria na kanuni za uendeshaji wa kiwanda katika ufanisi wa hali ya juu”,alisisitiza mhagama.
Kiwanda cha viatu cha Gereza Kuu Karanga, Moshi kilizinduliwa rasmi Juni 3, 1977 na Rais wa awamu ya kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Baba wa Taifa Mwalimu, Julius Kambarage Nyerere.Awali kilikuwa na ubia na Mfuko wa hifadhi ya jamii wa PPF ambapo baada ya mabadiliko ya kuunganishwa kwa mifuko hiyo , kwa sasa kina ubia na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF.

UHABA WA MADARASA TATIZO WANAFUNZI 1266 WAKOSA MASOMO



Wanafunzi 1266 waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2018/2019 mkoani Lindi wameshindwa kujiunga na kuanza masomo kutokana na ukosefu wa vyumba vya madarasa.
Hayo yalibainishwa jana na katibu tawala(RAS) wa  mkoa wa Lindi, Rehema Madenge alipozungumza kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa(RCC) kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa,iliyopo katika manispaa ya Lindi.
Madenge alisema katika zoezi la uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2019, wanafunzi 11808 walichaguliwa na kupangiwa shule watakazo jiunganazo kwa ajili ya masomo.Ambapo kati ya wanafunzi hao waliochaguliwa ni wasichana 6124 na wavulana 5684.
Alisema kati ya wanafunzi hao waliochaguliwa,bado wanafunzi 1266 hawajajiunga kwenye shule walizopangiwa kutokana na kukosekana kwa vyumba vya madarasa.Huku akibainisha kwamba wanafunzi hao ni wasichana 602 na wavulana 664.

Madenge alizitaja halmashauri ambazo baadhi ya wanafunzi waliochaguliwa wameshindwa kuanza masomo kutokana na tatizo hilo kuwa ni,majina na idadi ya wanafunzi kwenye mabano ni Kilwa(434),Lindi(443),Nachingwea(127) na Ruangwa wanafunzi 262.

Katibu tawala huyo wa mkoa wa Lindi alisema kushindwa kujiunga kwa wanafunzi hao mapema kumesababishwa na upungufu wa vyumba vya madarasa 39 ambavyo vingeweza kukidhi mahitaji.

"Wilaya inayoongoza kwakuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa ni Kilwa ambayo inaupungufu wa vyumba kumi nanne hadi sasa.Ruangwa vyumba kumi na moja,Lindi vyumba kumi na wilaya ya Nachingwea ni vyumba vinne,"alisema Madenge.

Alisema kufuatia hali hiyo,mkuu wa mkoa wa Lindi,Godfrey Zambi ameziagiza halmashauri ambazo wanafunzi waliochaguliwa wameshindwa kuanza masomo zikamilishe ujenzi wa vyumba vya madarasa.Ambapo amezitaka ifikapo tarehe 15,mwezi Februari,mwaka huu ziwe zimekamilisha ujenzi huo.

Kufuatia hali hiyo baadhi ya wadau wa elimu mkoani humu walitoa maoni yao yanini kifanyike.Miongoni mwa wadau hao ni Mohammed Mussa anaeishi katika manispaa ya Lindi.Ambae alisema wazazi na walezi hawanabudi kuungana ili kutatua changamoto zilizopo kwenye sekta ya elimu.Badala ya jukumu hilo kuachiwa serikali peke yake.

Mohammed alisema alitoa ushauri huo wa jumla kutokana na mkoa wa Lindi kuendelea kupata matokeo mabovu ya kiwanga cha ufaulu.Ambao matokeo ya mtihani wa kidato cha pili umeshika nafasi ya 24 kati ya 26 iliyopo Tanzania bara.