MEYA MWANZA AWEKWA NDANI

Related image
Tukio hilo limetokea baada ya kubainika katika salamu za Meya kwa Rais Magufuli, kulikuwa na maelezo ya ufisadi wa kiwanda hicho kilichopo Nyakato Ilemela jijini Mwanza.
Wanaotajwa kufanya ufisadi huo ni mkurugenzi wa Jiji hilo, Kiomoni Kibamba na viongozi wengine wa mkoa huo.
Pia viwanda vya kampuni hiyo vimekuwa vikituhumiwa kuwanyanyasa wafanyakazi wake wengine wakitimuliwa kazi bila kulipwa stahiki zao.
Baada ya kamati ya Ulinzi na usalama mkoa wa Mwanza chini ya John Mongella kubaini kwamba Meya huyo anataka kumwaga ukweli mbele ya rais, inadaiwa aliliagiza jeshi la Polisi kumkamata kiongozi huyo ambaye kwa kipindi kifupi ameonekana akifichua uchafu unaofanyika katika jiji la Mwanza.

VIONGOZI WA DINI WASHAURIWA KUJENGA UZALENDO

Image result for PHOTO OF HARRISON MWAKYEMBE
SERIKALI imewataka viongozi wa madhehebu ya dini nchini, kuwajengea waumini wao moyo wa uzalendo kwa nchi yao kupitia mafundisho na mahubiri yao.Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe alipokutana na viongozi wa madhehebu ya dini nchini, kujadili mada iliyosema ‘Imani na Uzalendo Kuelekea Uchumi wa Viwanda’ ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kujenga uzalendo na utaifa kwa Watanzania.

Mwakyembe aliwakumbusha viongozi hao wa dini kuwa uzalendo ni hali ya mtu kuwa na uchungu na taifa lake katika kuliletea maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kulitetea.Kutokana na dhana hiyo ya uzalendo, Serikali imewasisitiza viongozi wa dini kupitia mafundisho yao kuwakumbusha waumini wao kutekeleza mambo kumi kama sehemu ya imani yao, lakini kwa ustawi na maslahi ya taifa.Mambo hayo kumi ni pamoja na wajibu wa kila muumini kulipa kodi, kuzingatia usafi na utunzaji wa mazingira, kufanya kazi kwa bidii kwa kuwa Watanzania wana sifa nzuri ya kuchapa kazi, wanapokuwa nje ya nchi tofauti na wanapokuwa hapa nchini.
“Mambo mengine ambayo tunawaomba muwakumbushe waumini wenu ni uadilifu, kutii mamlaka, kulinda rasilimali za nchi kwa moyo, nguvu na akili zote, kupinga rushwa na matumizi ya dawa za kulevya pamoja na kuzingatia uaminifu kwa kujieupesha na vitendo vya wizi,” alieleza Dk Mwakyembe.
Waziri Mwakyembe aliwaambia viongozi wa dini kuwa wana jukumu kubwa la kuirejesha jamii ya Watanzania kwenye mstari, kwa kusisitiza uzalendo na utaifa ili taifa liwe na amani na utulivu na liweze kufikia malengo ya kuwa na uchumi wa viwanda.

“Matatizo makubwa katika nchi huanza polepole na tusipoziba ufa tutajenga ukuta. Msichoke kuhubiri amani kwenye nyumba zenu za ibada ili amani tuliyonayo tangu tupate uhuru iendelee kudumu, ,” alieleza Mwakyembe.

WAPINZANI WATAKIWA KUWAACHIA WATU 30 WALIOWAKAMATA CONGO

Umoja wa mataifa umetoa wito wa kuachiwa mara moja kwa watu 30, wa chama kikuu cha upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kutoka korokoroni.Wanachama wa vyama vikuu viwili vya Union for Democracy na wenzao wa Social Progress, walikamatwa siku ya Jumapili katika mji wa Lubumbashi, ulioko Kusini mashariki mwa nchi hiyo, baada ya polisi kuvunja mkutano waliokuwa nao.Utawala wa Rais, Joseph Kabila, umepiga marufuku mkutano wa aina yoyote wa kisiasa, pamoja na maandamano ya upinzani, tangu muda wake wa kuhudumu kama Rais kisheri, ulipomalizika mwaka mmoja uliopita.
Tume ya uchaguzi nchini humo, imesema kuwa, haitakuwa rahisi kuandaa uchaguzi mkuu wa Urais, kabla ya mwezi Aprili mwaka ujao wa 2019.Chama kingine cha upinzani- Union for the Congolese Nation, kimesema kwamba, kitajiondoa katika serikali ya ugawanaji mamlaka, kuhusiana na kucheleweshwa kwa uchaguzi mkuu.Maandamano ya mara kwa mara ya upinzani nchini humo umekabiliwa vikali na utawala wa Rais Joseph Kabila.

WAANDISHI WA HABARI WACHAPWA VIBOKO

Waandishi wa Habari wacharazwa bakora Geita

 Daniel Limbe mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari geita
Waandishi wa habari wanne mkoani Geita wameshambuliwa kwa bakora na kuwekwa sero na askari wa jeshi la polisi mkoani humo wakati wakitekeleza majukumu yao baada ya wanafunzi wa shule ya sekondari Geita kufanya vurugu shuleni.
Inaelezwa kuwa waandishi hao wamekutwa na maswahibu hayo  Oktoba 21,2017 ambapo mbali na kupigwa kamera ya mwandishi wa habari Esther Sumira wa Azam Tv imeharibiwa.
Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Geita Daniel Limbe amewataja miongoni mwa waandishi wa habari waliokumbwa na kadhia hiyo kuwa ni Esther Sumira ( Azam Tv) ,Editha Edward (Mtanzania,Rehema Matowo(Mwananchi) na Emmanuel Ibrahim (Clouds Media).
Taarifa zinasema hakuna uhusiano mzuri baina ya jeshi la polisi mkoa wa Geita na waandishi wa habari.
Chama cha Waandishi wa habari mkoa wa Geita (GPC) kinalaani vikali tukio la waandishi wa habari kushambuliwa kwa kipigo na jeshi la polisi wakati wakitekeleza majukumu yao kwenye vurugu zilizotokea jana kwenye shule ya sekondari Geita(Geseco).Vurugu hizo ambazo wanafunzi walikuwa wakishinikiza Bodi ya shule kuhakikisha inakwenda kufanya mazungumzo ya haraka na jeshi la polisi ili kuwatoa mahabusu wanafunzi watano waliokuwa wakishikiliwa kwa madai ya kumjeruhi kwa kipigo mwanafunzi mwenzao wa kidato cha tano,walitumia mawe kuponda majengo ya shule na kutishia kuichoma moto shule hiyo iwapo hatua za makusudi za wenzao kulejea shuleni hazitafanikiwa.
Baada ya vurugu hizo waandishi walifika eneo la tukio kwa ajili ya kutimiza wajibu wao ambapo Mwandishi wa gazeti Habari Leo,Editha Edward,alikumbana na kichapo cha askari polisi waliofika kutuliza ghasia zilizokuwa zimejitokeza shuleni hapo licha ya kujitambulisha kuwa yeye ni mwandishi wa habari.
Wengine waliokumbana na Kadhia hiyo ni Rehema Matowo, mwandishi wa gazeti la Mwananchi ambaye alinyang’anywa simu yake na kuwekwa chini ya ulinzi kwa muda kwenye chumba cha walinzi wa shule hiyo kabla ya kumrejeshea simu yake na kumwachia huru huku akitakiwa aondoke eneo hilo.
Hata hivyo Mwandishi wa Azam Tv Ester Sumira,alinyang’anywa kamera yake na walimu wa shule hiyo kwa muda wa zaidi ya dakika 20 wakimtaka kutochukua picha za vurugu zilizokuwa zikiendelea eneo hilo.
Na Mwandishi wa Cloud Tv,Emmanuel Ibrahimu alikumbana na msukosuko baada ya polisi kuzuilia pikipiki yake na kusababisha kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kazi.
Kutokana na vitendo hivyo visivyokuwa vya kiungwana ambavyo vinakiuka misingi ya utawala Bora na Haki za Binadamu,Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Geita kinaendelea kulaani vikali na tunaziomba taasisi zingine kama UTPC,MCT, TEF na wadau wote kulaani vitendo hivi vya kihuni ambavyo vinaendelea kutamalaki kila uchwao na kuharibu taswira nzima ya Utawala bora nchini.

MAHAKAMA KENYA YASHIDWA KUSIKILIZA KESHI YA KUIHIRISHWA KWA UCHAGUZI

Mahakama ya Juu Kenya yashindwa kusikiliza kesi ya kuahirishwa kwa uchaguzi kutokana na ukosefu wa majaji wa kutosha mahakamani.Jaji Mkuu David Maraga amesema baadhi ya majaji wapo nje ya nchi na wengine hawangeweza kufika mahakamani kwa sababu mbalimbali.Kesi hiyo ilikuwa imewasilishwa na wapiga kura watatu wakisema Tume ya Uchaguzi haiko tayari kuandaa uchaguzi huru na wa haki kesho.Jaji Mkuu amekuwa mahakamani na Jaji Isaac Lenaola pekee.Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu hakuweza kufika kortini baada ya kupigwa risasi kwa dereva wake jana jioni.Jaji Ibrahim, ambaye amekuwa akiugua, yuko nje ya nchi.Majaji Smokin Wanjala na Jacktone Ojwang hawakuweza kufika kortini pia.Jaji Njoki Ndung’u alikuwa amesafiri nje ya jiji la Nairobi na hakuweza kupata usafiri wa kumuwezesha kufika mahakamani kwa wakati.“Sisi wawili hatuwezi kufikisha idadi inayohitajika ya majaji mahakamani kwa mujibu wa kifungu 162 (2) cha Katiba. Kesi imeahirishwa hadi wakati mwingine,” ametangaza Jaji Maraga.
Wakili wa raia hao watatu waliokuwa wamewasilisha kesi hiyo, Harun Ndubi, ameshutumu hatua ya majaji kukosa kufika kortini akisema ni jambo la kushangaza.“Wakitoweka wakati tunawahitaji kutekeleza jukumu hili muhimu, unashangaa iwapo wanafuata kiapo walichokula,” amesema.Seneta wa Siaya James Orengo aliyewakilisha Raila Odinga mahakamani wakati wa kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa tarehe 8 Agosti amesema kilichotokea leo ni “mapinduzi ya katiba”.“Haya yamekuwa yakifanyika, hata katika tume ya uchaguzi. Stakadhabi zilizowasilishwa na tume kujibu kesi zimewasilishwa na naibu mwenyekiti na wala si mwenyekiti. Ni wazi kwamba tume ya uchaguzi inafanya kazi bila mchango wa mwenyekiti. Wafula Chebukati amekuwa abiria,” amesema.
“Taasisi ambayo imelemazwa na Jubilee kwanza ni IEBC. Na tume iliyosalia haina uwezo wa kuandaa uchaguzi.”Bw Orengo amesema anaamini ukosefu wa majaji wa kutosha mahakamani haufai kushangaza wengi na kudokeza kwamba uamuzi wa kutangaza leo kuwa Siku ya Mapumziko ulilenga kuvuruga shughuli za mahakama.“Kuna jaribio la kuhujumu taasisi za serikali zikiwemo taasisi huru kama vile tume ya uchaguzi na Mahakama ya Juu,” amesema.

TCU YATANGAZA MUDA WA KUANZA MASOMO ELIMY YA JUU

Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Profesa Eleuther Mwageni amesema wanafunzi ambao tayari wamekidhi vigezo na kupitishwa kujiunga na elimu ya juu wanatakiwa kuripoti chuoni ili kuanza masomo ifikapo Oktoba 30
“Tarehe ya Kalenda ya masomo haijabadilika iko palepale ambayo ni Oktoba 30 wanafunzi wanatakiwa kuanza masomo ya elimu ya juu kwa mwaka 2017/2018”, amesema Mwageni.
Aidha Prof. Mwageni ameeleza kuwa zaidi ya wanafunzi 450,000 tayari wameshapata vyuo hivyo kinachosubiriwa katika awamu ya tatu ni kupitisha wanafunzi wengine 12,000 ili kufikia malengo ambayo ni wanafunzi 57,000.
Awamu ya tatu ambayo ilianza Oktoba 18 hadi 22 imefikia hatua nzuri ambapo vyuo vinawasilisha TCU majina ya waombaji ambao vimewapitisha ili tume iweze kujiridhisha kisha wanafunzi waliochaguliwa katika awamu hiyo wajiunge na vyuo na waanze masomo kwa wakati.

Baadhi ya polisi wakiwa katika eneo la tukio Ukonga Mazizini wakidumisha ulinzi ili wananchi wasiendelee kuleta vurugu katika eneo hilo.


Kufuatia sintofahamu iliyokuwa inaendelea maeneo ya Mombasa Gongo la Mboto kati ya wananchi na jeshi la polisi na kupelekea baadhi ya raia kujeruhiwa na polisi kwa kile kinachodaiwa kuwa polisi walikuwa wanalipiza kisasi kufuatia kuuawa kwa askari mmoja wa kikosi cha 'Field Force Unit' (FFU)
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema ametembelea eneo hilo na kusikitishwa na kitendo cha jeshi la polisi kuchukua sheria mkononi na kujeruhi watu ambapo ameagiza wote waliohusika kufanya matukio hayo kuchukuliwa hatua za kisheria.

"Nimeambatana na RPC Salum Hamduni hivyo kwa wale walihusika hatua zitachukuliwa, na wale waliojeruhiwa watatibiwa, pia tumewachukua baadhi ya wananchi ambao wamehaidi kutoa ushirikiano hivyo  tutalifanyia uchunguzi na kutenda haki" Alisema DC Mjema.
Mkuu wa wilaya ya Ilala bi. Sophia Mjema akiongea na wananchi wa eneo la Ukonga Mazizini na kusikiliza kero zao baada ya kudai kupigwa na kupokonywa mali zao na watu wanaodhaniwa kuwa ni askari wa FFU.
DC Mjema amewataka wananchi wote walioharibiwa mali zao wajiorodheshe na serikali ya wilaya italifanyia kazi, huku akisisitiza hakukuwa na sababu ya kuchukua sheria mkononi wakati kulikuwa na mbadala wa kulichunguza suala hilo na kulipatia utatuzi.

Mkuu huyo wa wilaya ya ilala amewaomba wananchi watulie na waendelee na shughuli zao kwani hilo siyo jambo kubwa la kupelekea watu wauane na wavuruge amani ya nchi.

Sintofamhamu hiyo imedumu kwa siku tatu kufuatia kifo cha askari wa kikosi cha FFU ambapo inadaiwa aliuawa na wananchi jambo lililopelekea vurugu hizo, baina ya jeshi la polisi na wananchi.



LOWASA AMTEMBELEA LISSU



Waziri Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edward Lowassa leo Oktoba 24 amemtembelea na kumjulia hali Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Tundu Lissu ambaye anaendelea kupatiwa matibu Nairobi nchini Kenya.
Katika safari hiyo, Lowassa alikuwa ameandamana na mke wake, Mama Reginal Lowassa na wameonekana kwenye picha wakiwa na furaha na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.
Viongozi mbalimbali wa chama hicho wamekuwa wakiendelea kumtembelea na kumjulia hali kiongozi huyo, ambapo hivi karibuni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi

TUNATARAJIA KUPAA ZAIDI MWIJAGE


Image result for PHOTO OF CHARLES MWIJAGE
TANZANIA imesema haiwezi kutegemea ushuru wa forodha pekee kulinda bidhaa za ndani, hivyo ubora ni jambo la msingi ili ziweze kumudu ushindani wa kibiashara ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, kwa kuwa Tanzania ni mwanachama wa EAC na SADC, takribani nchi 22 zina haki ya kuingiza bidhaa nchini bila ukomo na bila kutozwa ushuru wa forodha.
Waziri mwenye dhamana na wizara hiyo, Charles Mwijage amesema, ili Tanzania ifanikwe kwenye masoko ya kimataifa na kufikia lengo la kuwa nchi yenye uchumi wa kati wa viwanda, inapaswa kuingiza matumizi ya viwango katika nyanja zote za uzalishaji, biashara na utoaji huduma.
Alisema, ingawa matumizi ya viwango nchini si ya kiwango cha juu kulinganisha na kasi ya kimataifa, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limetayarisha viwango vya kitaifa kwa lengo la kuchochea ukuaji uchumi na maendeleo ya jamii.
TBS ni miongoni mwa mashirika 162 ya viwango duniani ambayo ni wanachama wa Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO). Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Profesa Egid Mubofu amesema, utayarishaji wa viwango vya kitaifa unazingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, ambayo pamoja na mambo mengine inataka hadi kufikia mwaka 2025 Tanzania iwe nchi ya uchumi wa kati wa viwanda na kiwango kikubwa cha maendeleo ya watu.
Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia viwanda na biashara, Profesa Adolf Mkenda amesema, mbali na TBS viwango pia vinatazamwa na Tume ya Ushindani (FCC) na mamlaka nyingine za udhibiti na usimamizi ikiwemo Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wanapaswa kuhakikisha Tanzania inatekeleza kikamilifu azma ya kujenga uchumi wa viwanda.
FCC ni chombo huru cha serikali kilichoanzishwa kwa Sheria ya Bunge Namba 8 ya Mwaka 2003 ili kuhamasisha usawa kwenye ushindani wa kibishara sanjari na kumlinda mlaji na mtumiaji wa bidhaa.
Aidha TFDA ni wakala wa Serikali chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto wenye wajibu wa kusimamia ubora na usalama wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba ili kulinda afya za wananchi.
Ilianzishwa kupitia kifungu 4(1) cha Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi, na ilianza kazi rasmi Julai Mosi, 2003. Alisema, shughuli za mamlaka hizo ni muhimu zaidi wakati huu kwa sababu Serikali, kupitia Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano, imeamua kujenga uchumi wa viwanda.
Alisema, ili kuuza bidhaa kwenye soko la dunia, suala la usalama na ubora ni lazima lizingatiwe kwa kiwango cha juu. Profesa Mkenda alisema, kama bidhaa za viwandani nchini hazitakidhi viwango vya ubora na usalama, wananchi wataendelea kupenda bidhaa zinazoagizwa kutoka nje ya nchi hivyo kudhoofisha uzalishaji wa ndani.
Profesa Mkenda alisema pia kwamba, kuna haja ya kuzuia uingizwaji wa bidhaa zisizo na viwango na bidhaa bandia kutoka nje ya nchi kwa kuwa zitaleta ushindani usio wa haki kwa wazalishaji wa ndani.
“Bidhaa hizi zisizo na viwango na zile bandia zinapoingia nchini zinadhoofisha sana uzalishaji wa ndani kwa kuleta ushindani usio wa haki na kudhulumu walaji. Lazima tukubali kwamba bidhaa bora, salama na zisizo bandia kutoka nje zitaendelea kuingia nchini.
Baadhi ya bidhaa hizo zitatoka nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na nchi za SADC, na hivyo zitaingia nchini bila kutozwa ushuru wa forodha na bila kuwekewa ukomo”alisema.
Alisema, uzalishaji wa ndani lazima ukukidhi viwango vya kimataifa, hivyo mamlaka za udhibiti na usimamizi zina wajibu wa kufanikisha hilo ili bidha za Tanzania zihimili ushindani ndani na kwenye masoko ya nje.
“Lazima tukubali kuwa ushindani wa haki ni jambo jema. Ushindani wa haki humnufaisha mlaji kwa kumpa bidhaa bora na salama kwa bei ahueni. Ushindani pia hulazimisha wazalishaji wengine kuacha kubweteka na badala yake kuongeza ubunifu na ubora wa bidhaa zao.
Kwa maana hiyo ushindani ni jambo bora sana” alisema Profesa Mkenda. Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora wa TBS, Mhandisi Tumaini Mtitu amesema, bidhaa zisizo na viwango vya ubora husababisha ushindani usio sawa katika soko, zinadhuru afya za walaji au watumiaji wa bidhaa na huchafua mazingira kwa namna tofauti.
“Nembo ya ubora ya TBS ndiyo inayopaswa kutumika kuonesha kuwa bidhaa hii au ile imethibitishwa ubora kwa sababu inatolewa na shirika lenye dhamana ya kudhibiti ubora wa huduma na bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani na ndilo linaloviandaa viwango hivyo kwa ngazi ya taifa” alisema Mtitu. Alisema, hata bidhaa zinazoingizwa katika soko la ndani kutoka nje ya Tanzania hukaguliwa ubora ili kujiridhisha kuwa zinakidhi viwango vya kimataifa.

MHE:LUKUVI ATOLEA UFAFANUZI WA BOMOA BOMOA


Image result for PHOTO OF WILLIAM LUKUVI
SERIKALI imewaondoa hofu wananchi juu ya tishio la bomoabomoa ya nchi nzima kwa waliojenga bila kuwa na vibali vya ujenzi, ikisisitiza si wote watakaohusika, bali `matapeli’ na wavamizi wa maeneo ya watu wengine.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ameongeza kuwa, wananchi waliojengwa kwenye maeneo yasiyopimwa na wasio na vibali vya ujenzi, hawatabolewa nyumba zao, kama umma ulivyopotoshwa.
Lukuvi alisema hayo Ikulu jijini Dar es Salaam jana wakati wa hafla ya kuwatunuku vyeti wajumbe walioteuliwa na Rais John Magufuli kuchunguza biashara ya madini. Kwa mujibu wa Lukuvi, alilazimika kufafanua hivyo baada ya jana baadhi ya vyombo vya habari, hususani magazeti, kumnukuu vibaya kwa kuandika kuwa wananchi waliojenga kwenye maeneo yasiyopimwa na bila kuwa na vibali watabolewa nyumba zao.
“Asilimia 85 ya wananchi wanaishi kwenye makazi holela katika maeneo ambayo hayakupimwa. Serikali hatutabomoa nyumba zao ila tunachokifanya ni kurasimisha makazi yao ili waishi mahali salama, wapate huduma za kijamii na waweze kulipa kodi kwa serikali,” alieleza Waziri Lukuvi.
Lukuvi alisema nyumba zitakazobolewa ni zile zilizojengwa kwenye viwanja walivyoporwa wananchi wanyonge na masikini. Alisema Serikali haitafumbia macho watu wenye nguvu ya pesa, wanaoshirikiana na baadhi ya watumishi wasio waaminifu wizarani na kwenye halmashauri, kunyang’anya viwanja vya wananchi masikini na kubadilisha umiliki wa viwanja hivyo.

MILLION 200 ZAKUSANYWA MNADA WA NG'OMBE


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina akiongea na waandishi wa habari kuhusu opareshei ondoa Mifugo leo katika ofisi za wizara hiyo jijini Dar es Salaam,Pembeni yake ni Naibu Waziri Abdalah ulega, kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo katika sekta ya Mifugo Dkt Maria Mashingo na kushoto ni Katibu Mkuu sekta ya Uvuvi Dkt. Yohana Budeba

Kupitia Amri ya Mahakama iliyoamuru kupigwa mnada kwa ng’ombe waliovamia toka nchi jirani ya Kenya, Serikali imekusanya zaidi ya Shilingi Milioni 200 baada ya ng’ombe hao kupigwa mnada katika wilaya ya Mwanga mwishoni mwa wiki.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpiga amesema Wizara yake imejipanga na kuendelea na Oparesheni maalum ya kukamata na kuondoa mifugo yote inayovamia  kutoka nchi jirani kupitia mikoa ya mipakani kama Katavi, Kigoma, Tanga, Mara,Ruvuma, na Arusha na kuagiza wakuu wa Mikoa na Wilaya hizo kuendesha Opresheni hizo Maalum ndani ya siku saba.
“Mimi , Naibu Waziri wangu, makatibu wakuu na wataalam tunaingia tena katika opareshi hiyo maalum kesho.” Alisisitiza Mpina
Aidha, Mpina alisema kuwa serikali haipo tayari kuingia gharama ya kutibu magonjwa yanayoletwa na mifugo wanaovamia kutoka nchi jirani ambao kwa namna moja au nyingine huleta uharibifu wa mazingira kwa kukata miti ovyo, kusababisha mmomonyoko wa udongo na kuchangia kwa kiasi kikubwa migogoro ya wakulima na wafugaji.
Mpina alisema, watu wenye nia mbaya wasihusishe Opareni hii na mahusiano ya nchi hizi mbili akitolea mfano mahusiano ya Kenya na Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa yapo kisheria.
Akizungumzia suala ya mifugo ya Tanzania kuwa na chapa Mpina alisema, suala hili linashughulikiwa na ifikapo Desemba mwaka huu litakuwa limekamilika na hivyo kurahisha oparesheni hizi za kuondoa mifugo vamizi.