GAIRO:YATIMA WASAIDIWA VIFAA VYA SHULE


Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe akiwaasa watoto yatima wa kituo cha Bethel Wilayani Gairo. Kulia kwake ni baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama walioambatana naye. Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Gairo, Mhe. Andrea Sendeha akitoa salamu kwa watoto yatima.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe akigawa zawadi kwa watoto yatima wa kituo cha Bethel kilichopo wilayani humo.
Watoto wa kituo cha Bethel Wilayani Gairo wakiwa wamejipanga mstari kupokea zawadi.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe (mwenye nguo ya njano), Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Gairo, Mhe. Andrea Sendeha (wa tatu toka kulia) pamoja na kamati ya ulinzi na usalama wakiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima wa kituo cha Bethel wa Gairo.


Katika kujali makundi yenye changamoto za maisha hasa watoto wadogo, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Shaidi Mchembe amegawa sare za shule na madaftari kwa watoto yatima 150 kituo cha Bethel Wilayani Gairo kinachosimamiwa na Mchungaji Chacha.

Hafla hiyo ya ugawaji wa vifaa ulifanyika mapema wiki hii, ambapo Mhe. Mchembe amesema kuwa huo ni utamaduni aliojiwekea kila mwanzo  wa mwaka wa kuwakumbuka watoto yatima na wale waishi katika mazingira magumu.

"Nawakumbusha wananchi kujenga utamaduni wa kusaidiana watu wasiojiweza ili muweze kupata baraka kutoka kwa mwenyezi Mungu, unajua unapokuwa nacho ukatoa kidogo unabarikiwa zaidi," alisema Mhe. Mchembe.

Mhe.  Mchembe aliwakumbusha watoto hao kuzingatia masomo kwani Serikali ya awamu ya tano ya Dr. John Magufuli inatoa elimu bure hivyo hakuna mtoto wa masikini atakayeshindwa kusoma. 

Katika kukua kwao wamtangulize Mungu naye ataendelea kuwabariki na kuwatoa katika hali ya kuhisi unyonge wa kukosa wazazi.

Mwisho aliwaasa waalimu kuwa na moyo wa upendo kwa watoto yatima. Pia kuweka karibu hasa watoto wa kike kuwaepusha na mimba za utotoni.

ELIMU YATOLEWA KWA VIONGOZI WA DINI DHIDI YA KUPINGA NDOA ZA UTOTONI


Mwenyekiti wa Mtandao wa kutokomeza Ndoa za Utotoni Bi. Valeria Msoka akisisitiza jambo katika mkutano uliowakutanisha viongozi wa dini zote lengo likiwa ni kujadili nafasi yao katika kupinga ndoa za utotoni.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia kwa umakini mkutano mapema leo jijini Dar es salaam.

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Al Hadi Mussa Salim akitoa ufafanuzi wa jambo fulani mapema leo katika mkutano uliowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali na kimila katika kujadili nafasi yao katika kupinga ndoa za utotoni.
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Al Hadi Mussa Salim akichangia mada mbele ya wageni walioudhuria mkutano huo mapema leo jijini Dar es salaam.

 Mkurugenzi mtendaji wa RICPT ambaye pia ni muwakilishi wa dini ya kikristo Rev. Canon Thomas Godda akitoa ufafanuzi juu ya siku hiyo, na nini nafasi yao kama viongozi wa dini katika kupinga ndoa za utotoni na ushiriki wao katika kuleta mabadiliko ya sheria ya ndoa inayotumika hivi sasa.
Mwanasheria kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Bw. Godfrey Mpandikizi akitoa presentetion mbele ya wageni waliudhuria mkutano wa kujadili kushinikiza viongozi wa dini na wakimila kupambana ili kuweza kubadilishwa kwa sheria ya ndoa iliyopo hivi sasa.

  • Viongozi wa dini zote hapa nchini wametakiwa kuwa mstari wa mbele kuishinikiza serikali kukubali kubadilisha sheria ndoa ya mwaka 1971.

  • Hayo yamesemwa mapema leo jijini Dar es salaam katika semina iliyoandaliwa na Mtandao wa Kutokomeza Ndoa za Utotoni(TECMN) iliyowakutanisha viongozi wa dini zote mbili pamoja na viongozi wa kimila kutoka mikoa mbalimbali.

  • Akiongea katika semina hiyo Bi. Valeria Msoka alisema kuwa viongozi wa dini ni watu walio karibu sana na jamii, hivyo wanazijua vizuri changamoto wanazokutana nazo wananchi ikiwemo ndoa za utotoni na wanatakiwa wasikae kimya kwani wao ndio msaada pekee kwa jamii yao.

  • Lakini pia viongozi wa dini ni watu wanaopewa nafasi nzuri na kuheshimiwa kwa kiasi kikubwa na serikali hivyo watumie muda huo kuiamba serikali kuwa sheria hii ya mwaka 1971 inayotoa ruhusa kwa mtoto wa kike kuolewa akiwa na miaka 14 haifai na inatakiwa kubadilishwa.

  • Mwenyekiti huyo aliendelea kusema kuwa lengo la kukutana na viongozi wa dini ni kujaribu kushauriana na kuona nini watakifanya kushinikiza kubadilishwa kwa sheria hiyo inayomnyima haki za zake za msingi mtoto wa kike.

  • Akiongea kwa niaba ya dini ya kiislamu Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Al Hadi Mussa Salim alisema kuwa dini zetu zimekuja kwa lengo kuu la kuwasaidia wanadamu na hasa wanawake ambao walikuwa wakinyanyaswa na kunyimwa haki zao katika jamii hususani kwa upande wa ndoa.

  • Aidha Sheikh Mkuu wa Mkoa alisema kuwa cha muhimu tuungane kwa pamoja Waislamu, Wakristo, viongozi wa Kimila pamoja na serikali katika mitazamo na mwazo yetu ili tujue kuwa mtoto wa kike ni nani na haki zake ni zipi anazostahili kupata, kwa njia hiyo tunaweza kufanikiwa kulitokomeza tatizo hili la ndoa za utotoni.

  • Sheikh huyo aliendelea kusema kuwa tusipokuwa na sauti moja hatutaweza kama viongozi wa dini tukisema ndoa za utotoni zikome lakini serikali ikipinga atuwezi kuondoa tatizo hili, cha msingi ni kukubaliana makundi yote kuwa hatuzitaki ndoa za utotoni katika jamii yetu serikali ikubali viongozi wa kimila wakubali, wananchi wakubali na makundi yote yawe tayari kupambana vita hivi.

  • Kwa upande wake kiongozi aliwakilisha dini ya kikristo Rev. Canon Thomas Godda alisema kuwa zama zimebadilika kwani mwanzo sharia hii ilivyotungwa na ilipitishwa kwa urahisi kwa kuwa watu hawakuwa na uelewa, ila kwa sasa watu wameelimika na inapaswa kupingwa kwa nguvu zote swala hili.

  • Bw. Thomas aliendelea kusema kuwa ndoa inayokubalika hata katika vitabu vya dini ni ya watu wazima wote ambao umri wao ni kuanzia miaka 18 na kuendelea, hivyo basi wao kama viongozi wa dini watajaribu kufanya ushawishi kwa kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha swala hili linatokomezwa kabisa na sheria inabadilishwa.

SILAHA ZA KIVITA ZAKAMATWA SHINYANGA


Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata silaha ya kivita aina ya AK-47 iliyotupwa na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi waliokuwa wanataka kuvamia kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd kilichopo Nhelegani katika kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Alhamis Januari 18,2018 Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule amesema walikamata silaha hiyo usiku wa kuamkia leo majira ya saa tano eneo la Tinde wakati majambazi hao wanafuatiliwa na polisi ndipo wakaamua kutupa bunduki hiyo.

“Silaha hii aina ya AK-47 yenye namba 18116428 ilikuwa imefungwa kwenye skafu yenye rangi ya nembo ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ikiwa na risasi 25 ndani ya magazine yake na risasi zingine 8,zikiwa kwenye mfuko mdogo wa nailoni”,alieleza Kamanda Haule.

“Majambazi wawili pia walitelekeza pikipiki aina ya SANLG yenye namba za usajili MC 856 BPF,mafuta ya cherehani ya kulainishia silaha,tochi mbili na koti zito”,aliongeza.

Alisema jeshi la polisi lilipata taarifa za majambazi hao kutaka kuvamia kiwanda hicho kinachomilikiwa na raia wa China tangu tarehe 6.01.2018 kisha kuanza kuwafuatilia na kubaini kuwa baadhi yao ni wakazi wa Kahama na Ushirombo ambapo amewataka kujisalimisha polisi.

Bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 iliyokuwa imefungwa kwenye skafu yenye rangi ya nembo ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliyotelekezwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Wachina mjini Shinyanga- Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Silaha na vifaa vilivyotelekezwa na majambazi
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha skafu iliyotumika kufunga bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 iliyotupwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Jielong
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha silaha aina ya AK-47 yenye namba 18116428 na mafuta ya kulainishia silaha yaliyotupwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Jielong
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule  akionesha risasi zilizotelekezwa na majambazi
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule  akionesha  pikipiki aina ya SANLG yenye namba za usajili MC 856 BPF iliyotelekezwa na majambazi
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule  akionesha koti zito lililotelekezwa na majambazi
Jengo la ofisi za kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd kilichopo Nhelegani katika kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga.
Meneja Mkuu Msaidizi wa kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania),bwana Liu Buhua akilishukuru jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga kwa kuzuia uhalifu uliotaka kufanywa na majambazi
Meneja Mkuu Msaidizi wa kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd ,bwana Liu Buhua akilishukuru na kulipongeza jeshi la polisi kuzuia uhalifu katika kiwanda hicho

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akiwa katika  kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd.

VYAMA VYA SIASA MAREKANI NJIA PANDA



  picha ya Bunge la Marekani.
Huku siku ya mwisho ikiwa imekaribia hapo Ijumaa usiku kabla ya kuwa na uwezekano wa kufungwa kwa shughuli za serikali ya Marekani wabunge wa vyama vya democrat na republican wako njia panda kukubaliana ili shughuli za serikali ziendelee bila ya kuweka hatarini mambo yalio na kipaumbele kwa vyama vyao.
Wademokrat wanataka muswaada wa kujitegemea ili serikali iweze kuendelea kufanya kazi wakati kwa upande wa chama cha republican wanataka muswaada uliounganishwa na usalama wa mipaka na mabadiliko ya uhamiaji.
Warepublikan waliwatumia wademokrat muswaada ambao hauna sera ya kuwalinda wahamiaji laki 7 wasio na vibali walioletwa nchini na wazazi wao wakiwa watoto wadogo lakini inawapa nafasi wademokrat hatua ya kipaumbele cha juu ya kurudisha tena bima ya afya kwa watoto kwa miaka sita. (CHIP).

KAULI YA TRUMP YAFANANISHWA NA UDIKTETA ASEMA SENETA

Seneta afananisha kauli ya Trump na udikteta


Seneta John McCain
Maseneta wawili wa chama cha Republikan Jumatano wamemshutumu Rais Donald Trump kwa kuendelea kuchukizwa na habari zinazokosoa uraisi wake, wakisema kufanya hivyo kunakandamiza misingi ya kidemokrasia katika jamii, uhuru na uwazi wa vyombo vya habari.
Katika maoni yalioandikwa katika gazeti la Washington Post, Seneta wa Republikan kutoka Arizona John McCain amesema kitendo cha Trump kujirudia katika madai ya “habari feki” zinapokuja habari ambazo Trump hazipendi hutumiwa na viongozi wa nchi nyingine kama ni sababu wakati wanavinyamazisha vyombo vya habari, “ambavyo ndio moja ya nguzo za demokrasia.”
Huko katika Bunge la Marekani, Seneta mwengine wa Arizona, Jeff Flake, ambaye amekuwa anamkosoa mara kwa mara Trump, amesema katika hotuba yake kwenye Baraza la Seneti kuwa kitendo cha Trump kukebehi vyombo vya habari ni sawa na kauli za siasa zinazotolewa na madikteta.
“Sio tu mwaka uliopita umeshuhudia rais wa Marekani akitumia lugha ya madikteta kuelezea vyombo huru vya habari, lakini inaokena hivi sasa, amegeuka kuwahamasisha madikteta na watawala wanaotumia mabavu kwa matamko yake. Hili ni jambo la makosa. Hatuko katika zama za habari feki kama anavyoeleza ((Rais wa Syria)) Bashar Assad. Sisi tuko, ukweli ulivyo, katika zama ambazoutashi wa kidikteta unajirudia tena kwa kuwashambulia watu huru na jamii huru kila mahali."

VIONGOZO WA AU WATETA KUHUSU KAULI YA TRUMP



Balozi Arikana Chihombori-Quao,
Balozi wa Umoja wa Afrika (AU) nchini Marekani, Arikana Chihombori-Quao, ameiambia VOA kuwa viongozi wa Afrika wamekasirishwa na tamko la udhalilishaji juu ya wahamiaji kutoka bara la Afrika na Haiti linalodaiwa kutolewa na Rais Donald Trump.
Amesema anategemea hatua zaidi rasmi na juhudi za kidiplomasia kupinga hilo, ikiwa ni pamoja na uwezekano wa mabalozi wa Afrika kususia kuhudhuria hotuba ya rais ya hali ya taifa la Marekani kwenye Bunge la Marekani.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje Heather Nauert amesema Marekani ina uhusiano imara na Waafrika na Haiti, uhusiano imara zaidi kuliko maoni yoyote, ameripoti mwandishi wa VOA.
Wakati hisia hasi zikiendelea kutolewa nchini Marekani na nchi za nje kutokana na kauli ambayo vyanzo kadhaa vimesema kuwa rais alitoa tamko juu ya aina ya wahamiaji anaopendelea waingie nchini Marekani, rais aliulizwa na mwandishi iwapo anataka wahamiaji zaidi watoke kutoka Norway.
Trump alijibu: “Nataka watoke kote ulimwenguni.
Msemaji wa Ikulu ya White House Sarah Huckabee Sanders amekiri kuwa rais alitumia lugha kali wakati wa mkutano wake na wabunge juu ya suala la wahamiaji, na kusema kuwa ni sehemu ya wito wake.
“Nafikiri kuwa hiyo ni moja ya sababu watu wa Marekani wanampenda Trump, sababu mojawapo iliyopelekea kushinda uchaguzi na anaendelea kuwepo katika ofisi yake ya Oval ya ikulu ya White House. Hii ni kwa sababu yeye sio mtu anayetegemea kuandikiwa kila kitu. Yeye ni mtu ambaye anaeleza vitu vile vilivyo mara nyingi, na mara nyingine anatumia lugha kali sana,” amesema Sanders.
Matokeo ya kauli hiyo yenye utata anayodaiwa kuitoa Trump, Botswana, Ghana, Haiti, Namibia, Senegal na Umoja wa Afrika wamepeleka malalamiko yao rasmi ya kidiplomasia kupiga udhalilishaji huo.
Balozi wa Umoja wa Afrika nchini Marekani, Arikana Chihombori-Quao ameiambia VOA kuwa matamko hayo hasi juu ya Afrika na Uongozi wa Trump wa sera ya “Marekani Kwanza” ni kimbingamizi kwa uhusiano wa muda mrefu wa karibu kati ya Marekani na bara la Afrika.

TAFITI:NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI BADO HAZINA UHURU KAMILI



Reipoti ya Freedom House 2017.
Haki za kidemokrasia zimezidi kuonyesha kutoheshimiwa kaitka eneo la Afrika Mashariki ambapo Kenya, Tanzania na Rwanda zimeshuka viwango katika ripoti mpya juu ya hali ya uhuru duniani (global status of freedom).
Kenya
Uhuru Kenyatta akimaliza kukagua gwaride kabla ya kula kiapu kiwanjani Kasarani Nairobi.
Uhuru Kenyatta akimaliza kukagua gwaride kabla ya kula kiapu kiwanjani Kasarani Nairobi.
Utafiti uliofanywa na taasisi binafsi ya Freedom House lenye makazi yake Washington, ambalo sio la kisiasa wala serikali, linaeleza kasoro zilizojitokeza katika mchakato wa uchaguzi wa urais Kenya.
Ripoti hiyo imeeleza kuwa uchaguzi ulikuwa na utata, ambao “marudio ya uchaguzi yalioamrishwa na mahakama yalifanyika bila ya kuwepo mageuzi ya msingi, matukio ya vurugu za kisiasa na kususiwa kwa uchaguzi huo na mgombea mkuu wa upinzani, Raila Odinga.
“Mambo haya yanatia dosari ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta, ambapo alidai kupata kura asilimia 98 ya kura zote pamoja na kuwepo mahudhurio ya chini ya wapiga kura,” ripoti hiyo imesema.
Taasisi hiyo imeipa Kenya asilimia 48 kati ya 100 --- ikionyesha demokrasia imeshuka kutoka asilimia 51 vile ilivyokuwa imeripotiwa mwaka 2017. Hali hiyo inaifanya Kenya kuwa kati ya nchi 58 zinazoelezwa kuwa “hazina uhuru kamili.”
Tanzania
Rais John Magufuli
Rais John Magufuli

Taasisi hiyo ya Freedom House pia imeripoti kushuka kwa haki za kidemokrasia nchini Tanzania, ambayo ilikuwa iko juu kidogo kuliko Kenya.
Tanzania, ambayo imepewa asilimia 52 katika ripoti hiyo mpya na asilimia 58 katika utafiti wa mwaka 2017, imewekwa katika kikundi cha nchi “zisizo na uhuru kamili.”
“Serikali ya Rais John Magufuli – ambaye alichukua madaraka mwaka 2015 kama ni mwanachama pekee wa chama tawala nchini – alianzisha ukandamizaji wa wapinzani, kuwafunga wanasiasa wa upinzani, akifunga vyombo vya habari na kuwakamata wananchi ambao wanatoa maoni yao ya kukosoa katika mitandao ya kijamii,” utafiti huo wa mwaka 2018 umeeleza.
Uganda
Rais Yoweri Museveni
Rais Yoweri Museveni
Uganda imeonyesha mabadiliko kwa kupanda daraja kutoka “kutokuwepo uhuru kabisa” kwenda “zisizo na uhuru kamili” japokuwa hivi sasa imepewa daraja la asilimia 37 ambayo bado iko chini kuliko Kenya na Tanzania.
Taasisi ya Freedom House inafanya tathmini yake ya uhuru nchini Uganda kwa kigezo cha “kuamka kwa sekta ya habari na utayari wa waandishi wa habari, mitandao ya jamii na wananchi kutoa maoni yao.”
Hata hivyo, ripoti hiyo imeongeza kuwa “hali ya kisiasa imeendelea kuwa kandamizi chini ya utawala wa muda mrefu wa Rais Yoweri Museveni.
Rwanda
Rais Paul Kagame
Rais Paul Kagame
Rwanda imeorodheshwa kati ya nchi 49 ambazo “haziko huru.” Imepewa asilimia 23 – ambayo imeshuka kidogo kutoka asilimia 25 ambayo ilipata mwaka jana katika ripoti ya Freedom House. Utafiti mpya hautoi maelezo juu ya daraja waliopewa Rwanda.
Nchi nyingine
Burundi, Somalia na Sudan Kusini pia zimeelezwa kuwa “haziko huru” katika ripoti hiyo.
Sudan Kusini imepewa daraja ya pili kutoka chini—pointi mbili--- kati ya nchi 195 ambazo tafiti hiyo ilifanywa na Freedom House. Somalia inaunafuu kidogo, ambapo inanukta saba. Burundi, pia imegubikwa na migogoro ya ndani lakini sio kwa kiwango ambacho Somalia na Sudan Kusini imeathiriwa na migogoro hiyo, imepata daraja ya asilimia 19.

WANAJESHI WA MAREKANI WATAENDELEA KUWEPO SYRIA ASEMA WAZIRI TELLERSON



Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Rex Tillerson akizungumza kwenye kituo cha Hoover Institute, Stanford, California.
Marekani ina sababu nyingine nyingi kwa Marekani kubaki na kuendelea kujihusisha nchini Syria.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Syria imesema Alhamisi kuwa kuwepo kwa jeshi la Marekani nchini Syria ni kitendo cha uchokozi na ukiukaji wa uhuru.
Maono hayo yamekuja baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Rex Tillerson kuelezea mipango yake katika hotuba aliyoitoa Jumatano akifafanua kwanini Marekani itaendelea kujihusisha kidiplomasia na kijeshi nchini Syria hata baada ya kulishinda kundi lenye msimamo mkali la Islamic State.
Marekani imeongoza ushirika wa kufanya mashambulizi ya anga dhidi ya malengo ya Islamic State nchini Syria na Iraq tangu mwaka 2014, na Pentagon imesema mwezi Desemba kuna takriban wanajeshi 2,000 wa Marekani nchini Syria.
Tillerson alijadili njia za kusonga mbele kwa Marekani nchini Syria katika tukio kituo kinachoelemea upande wa waconservative kwenye Hoover Institute. Aliorodhesha sababu kadhaa kwanini ni muhimu kwa Marekani kubakia katika nchi iliyogubikwa na vurugu, ikiwemo kuzuia kuibuka tena kwa makundi ya kigaidi ya Islamic State na Al-Qaida.
“Hatuwezi kuruhusu historia ijirudie yenyewe nchini Syria,” amesema Tillerson, akizungumzia kile alichokitaja kama makosa yaliyofanywa na utawala wa Obama katika kuondoa wanajeshi wa Marekani mapema mno nchini Iraq na kushindwa kuleta uthabiti nchini Libya baada ya mashambulizi ya anga ya NATO ambayo yamepelekea kuondolewa mamlakani kwa marehemu rais Moammar Gadhafi.
Tillerson amesema kuna sababu nyingine pia kwa Marekani kubaki na kuendelea kujihusisha nchini Syria.
“Kuwaondoa wanajeshi wote wa Marekani nchini Syria kwa wakati huu kutamsaidia Assad. Uthabiti, umoja na uhuru wa Syria hatimaye vitapatikana baada ya uongozi wa Assad ili kupatikana mafanikio. Kuendelea kuwepo kwa marekani kutahakikisha kuishinda ISIS kabisa na pia kufungua njia kwa mamlaka halali za kieneo ili kuendelea utawala wa majimbo kwa maeneo ambayo yatakombolewa,” amesema Tillerson.

MELI ZILIZOAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA ZAFUTIWA USAJILI



Makamu rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa na rais Magufuli.
Serikali ya Tanzania imesema inapitia upya usajili wa meli na kuhakiki taarifa za meli zote zilizosajiliwa nchini humo ili kuondokana na athari za meli zinazopeperusha bendera ya Tanzania zinazopatikana na makosa katika maeneo mbalimbali duniani...
Makamu wa Rais Samia Suluhuu Hassan amezungumzia hatua ya uhakiki wa meli hizo katika mkutano na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam, alipokuwa akitoa taarifa kwa wananchi juu ya maazimio yaliyofikiwa katika mkutano ulioshirikisha wataalamu kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Muungano,kushughulikia meli zinazopeperusha Bendera ya Tanzania,kufuatia hivi karibuni kukamatwa kwa meli za Kaluba iliyokamatwa Jamhuri ya watu wa Dominica,ikiwa na takribani tani 1,600 za dawa za kulevya na Andromeda iliyokamatwa Ugiriki ikisafirisha zana zinazotumika kutengeneza silaha kinyume na sheria za kimataifa kwenda Libya.
Serikali ya Tanzania imesema haihusiki na meli hizo zilizokamatwa licha ya kwamba zimesajiliwa nchini kupitia taasisi ya Mamlaka ya usafiri baharini Zanzibar, yenye mamlaka ya kusajili meli za ndani na nje.
Makamu wa Rais amesema mbali na uhakiki wa meli zilizopata usajili, serikali imeazimia pia kufanyia uchunguzi wa kina meli zitakazoomba usajili pamoja na kufanya mapitio ya sheria za ndani za usajili ili kuepusha nchi kuingizwa tena katika fedheha hizi
Wakati hayo yakiendelea jana wafanyabiashara wawili wakurugenzi wa kampuni tofauti za meli walifikishwa katika mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam wakituhukiwa kupeperusha bendera ya Tanznaia katika meli ya kichina kinyume cha sheria Wafanyabiashara hao ni Issa Haji mkurugenzi wa kampuni ya meli ya Lucky na Abdullah Issa Hanga wa kampuni ya meli ya Saha.

MABALOZI WA ZAMANI WALALAMIA.................



Wahamiaji wa Afrika na Haiti waliokuwa na azma ya kuomba hifadhi nchini Marekani, wakiwa Mexicali, Mexico, Oktoba. 5, 2016.
"Wahamiaji wanaokuja Marekani kutoka Afrika, ni watu wenye mafanikio makubwa.Ninataka kusema kutoka ndani ya moyo wangu, sisi ni sehemu yenu,sisi ni sehemu ya jumuiya ya ulimengu. Hatua cha ziada isipokuwa heshima kwenu," balozi wa Marekani nchini Zimbabwe.
Mabalozi 48 wa Marekani waliokuwa wakihudumu katika nchini mbali mbali barani Afrika wamepeleka barua White House, kuelezea ‘wasi wasi mkubwa’ juu matamshi yaliripotiwa kutolewa na rais Donald Trump akitumia lugha mbaya kuyaita mataifa ya Afrika.
“Sisi mabalozi wa zamani wa Marekani katika nchi 48 za Afrika, tunaandika kuelezea wasi wasi wetu mkubwa sana kuhusiana na ripoti juu ya matamshi yako ya karibuni kuhusu nchi za kiafrika na kuthibitisha umuhimu wa washirika wetu na mataifa takriban 50 ya Afrika,” barua hiyo imesema. “Kama mabalozi wa Marekani wa nje ya nchi tumeona Afrika yenye mambo mengi na utamaduni tajiri sasa, yenye ustahmilivu, na ukarimu mkubwa na huruma.”
Barua iliwapongeza wajasiriamali, wasanii, wanaharakati, wana mazingira, na wasomi barani humo, wakati wakisisitiza umuhimu wa kuendeleza uhusiano mzuri kati ya Marekani na mataifa 54 ya Afrika.
“Tuna matumaini kwamba utatathmini maoni yako kwa Afrika na raia wake, na kutambua umuhimu wa michango ya waafrika na wamarekani weusi ambayo wameitoa na kuendelea kuitoa kwa nchi yetu, historia yetu, na kuendeleza uhusiano wa kudmu ambao siku zote utaiunganisha Afrika na Marekani,” imesema barua.
Jumatano, katika hali ya kupinga matamshi ya Trump yaliyoripotiwa, balozi wa Marekani kwa Zimbabwe, Harry Thomas Jr. amesema kwamba nchi yake imewakaribisha waafrika wote wahamiaji na wageni.
“Ningependa kusema kwa niaba ya ubalozi wetu, serikali yangu, watu wa Marekani, tuna heshima kubwa kwa Zimbabwe, kwa bara la Afrika, watu wake, utamaduni wake, mila zake,” amesema akimuelezea rais Emmerson Mnangagwa na waliohudhuria sherehe za kupokea msaada wa afya mjini Harare.
“Wahamiaji wanaokuja Marekani kutoka Afrika, hasa Zimbabawe ni watu wenye mafanikio makubwa. Ninataka kusema kutoka ndani ya moyo wangu, sisi ni sehemu yenu, sisi ni sehemu ya jumuiya ya ulimwengu. Hatuna chochote zaidi ya heshima kwenu na tunawakaribisha kwetu kama wageni au wakazi, amesema.

AJALI KENYA YAUWA WANNE



Watu wanne wamepoteza maisha Jumapili asubuhi katika ajali ya gari iliyaohusisha basi la abiria na lori katika barabara ya Garrissa -Wajir nchini Kenya.
Ajali hiyo wakati basi lilipo ligonga lori lililokuwa limesimama majira ya saa saba usiku.
Polisi wamesema abiria wengine 10 wamejeruhiwa vibaya sana katika ajali hiyo na wamelazwa hospitalini.
Mkuu wa Polisi katika eneo la Wajir Stephen Ngetich amesema kuwa wanachunguza ni namna gani na kwa nini ajali hiyo ilitokea.
Tunachofahamu ajali hii ilitokea usiku na bado hatujaweza kujua mazingira yaliyopelekea ajali hiyo kutokea.
Basi hilo lilikuwa likielekea Wajir limebeba abiria 50 wakati ajali inatokea kwenye eneo la Habaswen.
Hii ni ajali nyingine ya hivi karibuni kutokea nchini pamoja na kuwepo kampeni ya kuzuia kuendelea kwa janga hili.
Makumi ya watu waliuwawa tangia mwanzoni mwa mwaka huu katika muelekeo ambao unaongopesha. Mnamo mwezi Disemba 2017 peke yake, Zaidi ya watu 360 waliuwawa katika ajali tofauti nchini Kenya.
Hili lilipelekea serikali kupiga marufuku safari za usiku kwa magari yote ya umma ikiwa ni sehemu ya juhudi ya kuzuia ajali hizo za barabarani

RAISI WA LIBERIA AFUKUZWA UANACHAMA



Rais wa LOiberia, Ellen Johnson Sirleaf.
Chama kinachotawala nchini Liberia, Unity party, kimemfukuza rais anayeondoka wa nchi hiyo, Ellen Johnson Sirleaf, kutoka kwa uanachama
Chama hicho kilipiga kura ya kumwondoa siku ya Jumamposi na hatua hiyo ilichukuliwa baada ya tuhuma kwamba hakumuunga mkono makamu wake wa rais Joseph Boakai kama mgombea urais kwenye uchaguzi uliofanyika mwaka jana.
Boakai, ambaye alikuwa makamu wa rais kwa miaka 12, alishindwa na nyota wa zamani wa soka, George Waeh.
Johnson Sirleaf, ambaye ni mshindi wa tuzo la amani la Nobel, hangegombea tena urais kwa sababu haruhusiwi na katiba ya Liberia kufanya hivyo.
Wakosoaji wa Boakai walimshutumu kwa kile walichokiita "kutofanya mengi ya kuimarisha taifa" akiwa makamu wa rais.
Iwapo kila kitu kitaenda shwari, Liberia itashuhudia ubadilishanaji mamlaka kwa njia ya kidemokrasia kwa mara ya kwanza katika kipindi cha Zaidi ya miaka 70.

WAMAREKANI WAMUENZI MARTIN LUTHER JR



Rais Donald Trump akizungumza wakati wa sherehe za kumuenzi Dr Martin Luther King Jr.
Wamarekani Jumatatu wanaadhimisha siku ya kumbukumbu ya Martin Luther King Jr. wakimuenzi kwa kuanzisha harakati za haki za kiraia nchini Marekani.
King alifanya hivyo akizingatia kuwa mafanikio ya harakati hizo zingeweza kufanikiwa tu kwa kufuata misingi ya kuepukana na uvunjifu wa amani.
Kila mwaka Jumatatu ya tatu ya mwezi Januari, Wamarekani wanamuenzi kiongozi wa haki za raia aliyeuwawa ambaye katika miaka ya 1950 na 1960 aliandaa maandamano ya amani dhidi ya ubaguzi, ikiwa ni harakati za kutafuta haki za watu weusi na kuwawezesha kupiga kura.
Wengi nchini wanatumia siku ya mapumziko kumkumbuka King kwa kutokuchoka katika kukomesha ubaguzi kwa kushiriki katika shughuli za huduma za kijamii.
Bunge la Marekani lilimuenzi King kwa ule moyo wake wa kutumikia jamii mwaka 1994 kwa kuifanya siku hiyo ni mapumziko iwe ni siku ya kuhudumia taifa.
Rais Donald Trump amemuenzi King wakati wa sherehe za kuadhimisha kumbukumbu yake mjini Washington Ijumaa, akipongeza hatua yake ya “kupigania haki na usawa kwa amani.”

AFRICA YAENDELEZA MKAKATI WA KUTOKUTEGEMEA WAHISANI



Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat
Tume ya mawaziri kumi wa fedha wanaowakilisha kanda tano za bara la Afrika wamepongeza hatua iliyofikiwa na mataifa ya Kiafrika ya kuendelea kukusanya nguvu kwa ajili ya kujiendeshea mambo yake bila kusubiri tena misaada ya wahisani.
Mawaziri hao kumi wa fedha wameeleza hayo mjini Kigali mwishoni mwa juma walipokutana kutathmini mafanikio ya mkakati huo uliochukuliwa na marais wa Afrika miaka miwili iliyopita.
Mwaka 2016 mwezi Julai ndipo marais wa kiafrika walipokutana Kigali Rwanda na kukubaliana kwamba kila nchi itenge asilimia sifuri nukta mbili kutokana na mapato ya baadhi zinazoingizwa kwenye nchi hiyo kutoka ng’ambo.
Umoja wa Afrika umesema unaachana na kutegemea misaada ya wahisani kwa ajili ya kuendesha mambo yake.
Umesema kuwa ilibainika kuwa zaidi ya asilimia 80% ya bajeti inayotumiwa na kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) ilitegemea pesa za wahisani.
Miaka miwili baadaye mwenyekiti wa kamisheni ya umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat ametoa taswira ya jinsi mataifa hayo ya Kiafrika yanavyoendelea kuchangia kiasi hicho cha mapato kama ilivyokubaliwa na wakuu wa nchi hizo.
"Mataifa 12 yanaendelea na kasi kubwa ya kutenga kiasi hicho kulingana na kiwango kilichokuliwa. Hii ina maana ndani ya muda wa miaka miwili tunakaribia kufikiwa kiwango cha msingi kinachotakiwa," amesema.
Viongozi wa kiafrika kwa nyakati tofauti wametaja kwamba kuendelea kutegemea mataifa wahisani kwa ajili ya kuendeshea mamo yake siyo tu kwamba yanadumaza maendeleo ya bara hilo, lakini pia hii inatoa mwanya wa kuendelea kuwepo kwa ukoloni mambo leo kutoka mataifa makubwa.
Waziri wa fedha wa Rwanda Balozi Claver Gatete amesema mataifa yote ya Kiafrika yataweza kutoa mchango huo kwenye kamisheni ya umoja huo.
Anaeleza kuwa: "Michango hii itaufanya umoja wa Afrika kujitosheleza kwa kiwango cha asilimia 100% ktk kutekeleza mahitaji ya bajeti yake,ikiwa ni pamoja na asilimia 75% kuwekwa kwenye kuendesha miradi mikuwa ya bara hili huku asilimia 25% ikiwekwa kwenye masuala ya ulinzi na usalama.
Sisi hapa kama mawaziri wa fedha hatutachukua nafasi kujadili yale yaliyopitishwa na marais wetu, la hasha tunachokifanya hapa ni kujadiliana utekelezwaji wake."
Hadi mwezi Disemba 2017 kwa ujumla mataifa 21 ya bara la Afrika ndiyo yalikuwa yamekwisha anza kutoa michango hiyo japo kwa viwango tofauti.
Kadhalika mawaziri wa fedha Nigeria, Morocco na Cameroon nao walihudhuria kama wanatume japo awali hawakuwa sehemu ya tume hiyo.

ODINGA KUAPISHWA TAREHE 30 JANUARY



Raila Odinga apiga kura Kibra, Agosti 8, 2017.
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga amesisitiza kuwa ataapishwa, kutwaa madaraka na kuunda baraza lake la mawaziri hata kama ikimlazimu kufanya hivyo akiwa mafichoni.
Katika mahojiano maalum na Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika, Bw. Odinga amefuta uwezekano wa kufanya mazungumzo na rais aliyepo mamlakani Uhuru Kenyatta ili kuweza kupatikana kwa suluhu ya kisiasa kati ya wawili hao.
Bw. Odinga amesema kuapishwa kwake kutafanyika Januari 30 kama ilivyopangwa awali na kila mkenya amealikwa kuhudhuria hafla hiyo na kueleza kuwa huenda ikamlazimu afanye hivyo akiwa mafichoni.
Rais Kenyatta kwa upande wake amekuwa akiuhimiza upinzani wa NASA kuachana na siasa kwani kipindi cha siasa tayari kimekamilika kwa mujibu wa kalenda ya matukio nchini Kenya.
Matamshi ya Bw. Odinga kuwa ataapishwa na kuwa rais wa wananchi yamekuwa yakiibua hisia mbali mbali miongoni mwa wakenya wengi wakijiuliza kule anapoelekea kutekeleza majukumu ya urais wakati ikulu ya Kenya ina mwenyeji ambaye ni Uhuru Kenyatta, Odinga hakubaliani na hilo.
Wachambuzi wa siasa za Kenya wamekuwa wakitofautiana kwa kauli kuwa huenda Odinga na vinara wenzake wanatumia kisingizio cha kuapishwa kama chambo cha kutaka mazungumzo na Bw. Kenyatta na vile vile kujumuishwa katika serikali, lakini Bw. Odinga anasema hilo si kweli hata kidogo.

JESHI LA NIGERIA LAWAACHIA WASHUTUMIWA 244 WA BOKO HARAM



FILE - Boko Haram militants (in camouflage) embrace and shake hands with Boko Haram prisoners, released in exchange for a group of 82 Chibok girls, who were held captive for three years by Islamist militants, near Kumshe, Nigeria, May 6, 2017.
Nigeria's army has released 244 Boko Haram suspects who have denounced their membership in the deadly extremist group.
Nigerian army operation commander Maj. Gen. Rogers Nicholas said Tuesday that those released Monday included 118 adult males, 56 women, 19 teens and 51 children. He said they were freed after they were screened and denounced the Nigeria-based insurgency.
The public release at the Maiduguri military barracks was done to mark Nigeria's Armed Forces Remembrance Day.
Boko Haram has killed more than 20,000 people during its eight-year insurgency. Nigeria has arrested thousands of suspected Boko Haram members in recent years. Human rights groups warn many detainees are arbitrarily arrested.
Nigeria's government established a de-radicalization program in 2016 that offers amnesty for those who repudiated the group.

HAWA HAPA VIJANA WENYE USHAWISHI HAPA BONGO


STRAIKA wa kimataifa wa Tanzania anayesakata kabumbu katika klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Samatta ametajwa kama mshindi wa jumla wa shindano la kutafuta vijana 50 wenye ushawishi zaidi nchini.
Ushindi huo umetokana na kupata kura nyingi kwenye kipengele cha Mwanamichezo mwenye ushawishi zaidi huku mwanamuziki wa Bongo Fleva hapa nchini Ali Kiba akimfunika hasimu wake Diamond Platnumz kwenye kipengele cha Burudani. 
Orodha kamili ya walioshinda ni hii hapa chini.

Kampuni ya Ufaransa yaondoa maboksi milioni 12 ya maziwa sokoni



Ilani ya kuwatadharisha walaji bidhaa ya maziwa ya watoto iliyoondolewa sokoni.
Zaidi ya maboksi milioni 12 ya maziwa ya watoto yanayotengenezwa na kampuni ya maziwa Lactalis ya Ufaransa yameondolewa madukani kutoka nchi 83 kwa hofu ya kuwa yamechafuliwa na vijidudu aina ya salmonella vinayosababisha sumu katika chakula.
Mkuu wa kampuni hiyo ya maziwa nchini Ufaransa Jumapili amethibitisha kuwa bidhaa zake zinarudishwa kiwandani kutoka nchi zote Ulaya, Afrika na Amerika ya Kusini na Asia baada ya Salmonella ilipogunduliwa katika moja ya mitambo yake mwezi wa Disemba 2017. Lakini Marekani, Uingereza na Australia hazikuathirika na tatizo hilo.
Maafisa wa kampuni hiyo wamesema kuwa wanaamini kuwa kuathiriwa kwa bidhaa zao na sumu hiyo kumetokana na matengenezo yaliofanyika katika kiwanda chao cha Celia huko Craon, kaskazini magharibi ya Ufaransa.
Emmanuel Besnier ameliambia gazeti la kila wiki Le Journal du Dimanche kuwa kampuni hiyo ya familia yake, ambayo ni moja ya kiwanda cha maziwa kikubwa kuliko vyote duniani, italipa fidia kwa “kila familia ambayo iliathiriwa na hali hiyo.”
Gazeti hilo limesema kuwa watoto 35 walionekana kuwa na vijidudu hivyo nchini Ufaransa, mmoja nchini Spain na pia kunauwezekano yuko mwengine Ugiriki.

Kwa mujibu wa wataalamu wa afya Salmonella inaweza kusababisha kuharisha kulikopindukia, maumivu ya tumbo, kutapika na kupungukiwa kwa maji mwilini kwa kiwango kikubwa. Pia inaweza kuhatarisha maisha ya mwanadamu, hususan watoto wadogo.
Waziri wa Kilimo wa Ufaransa amesema kuwa bidhaa kutoka katika kiwanda hicho zitaendelea kupigwa marufuku wakati uchunguzi unaendelea.

MIMI SIO MBAGUZI ASEMA TRUMP



Vijana walioingizwa nchini kinyume cha sheria na wazazi wao wakionyesha mshikamano wao kushinikiza programu ya DACA iendelezwe.
Rais Donald Trump amesema yeye sio mbaguzi Jumapili, siku tatu baada ya kuripotiwa kuwa amesema wahamiaji kutoka Haiti, El Salvador na Afrika wanatokea katika nchi alizozifananisha na choo.
“Mimi siyo mbaguzi kabisa ambaye utaweza kunihoji,” alijibu Trump swali la mwandishi katika Jumba lake la Kifahari huko Mar-a-Lago Florida lilioko ufukweni.
Trump amesema kuwa yuko tayari, anania na anauwezo wa kufikia makubaliano ya kuwahami wahamiaji vijana 800,000 wasiondolewe nchini Marekani, chini ya programu ya DACA, ambao miaka kadhaa iliyopita waliletwa na wazazi wao kinyume cha sheria nchini.
“Ukweli ni kuwa, sidhani kama Wademokrati wanataka kufikia makubaliano,” na mapema siku hiyo alisema anafikiria programu hiyo “huenda imeshakufa.”
Trump amedai kuwa wabunge wa chama cha Demokrat “hawataki kuwepo usalama katika mipaka, hawataki kuzuia madawa ya kulevya, wanataka kuondoa fedha kwenye bajeti ya jeshi kitu ambacho hatuwezi kufanya.” Katika ujumbe wake wa Twitter Jumatatu, Trump amesema, Marekani Kwanza na Tuifanye Marekani kuwa bora tena!”
Kauli mbaya inayodaiwa aliitoa Trump kuhusu watu wa Haiti, Salvador na wahamiaji kutoka Afrika imetikisa mazungumzo kuhusu kuwahami wahamiaji vijana kuondolewa chini ya programu ya kuchelewesha kwa muda kuchukuliwa hatua kuwaondoa vijana wanaoingia nchini (DACA) iliyokuwa imeanzishwa na Rais mstaafu Barack Obama.
Mazungumzo kati ya Ikulu ya White House na bunge la Marekani kuhusu programu ya DACA imefungamanishwa na mikutano ya dharura wiki hii juu ya kufadhili operesheni za serikali kuvuka saa sita ya usiku Ijumaa, wakati bajeti ya matumizi ya hivi sasa iliyoidhinishwa ikimalizika muda wake.
Kwa mujibu wa wale waliokuwepo katika ukumbi wa ikulu ya White House wakati wa mkutano huo juu ya wahamiaji wiki iliyopita, Trump alihoji ni kwa nini Marekani inaruhusu wahamiaji kutoka Haiti, El Salvador na Afrika na kusema anataka kuona wahiaji zaidi kutoka nchi kama vile Norway. Pia inavyoelekea ni kuwa anataka kuitoa Haiti katika mpango wa mageuzi ya wahamiaji.
Wakati ikulu ya White House haijakanusha kuwa Trump alitumia lugha chafu kuwaelezea wahamiaji ambao siyo wazungu, Trump alikanusha kwa ubabaishaji. “Lugha niliotumia wakati wa mkutano wa DACA ilikuwa mbaya, lakini hii siyo lugha iliyotumika,” amesema.
Siku ya Jumatatu, Josh Dawsey, mwandishi wa gazeti la The Washington Post aliyeibua habari kuhusu lugha chafu aliotumia Trump, akiwaambia shirika la habari la CNN kuwa maafisa wa ikulu ya White House wanasema kuwa inawezekana Trump alitoa tamko tofauti kidogo la matusi, akihoji ni kwa nini Marekani inawakubali wahamiaji kutoka nchi alizozifananisha na choo.