ASILIMIA 95 YA MIRADI YA KUBORESHA UMEME YAKAMILIKA JIJINI DAR ES SALAAM



SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO), limesema, tayari asilimia 95 ya uboreshaji miradi ya umeme katika jiji la Dar es Salaam, imekamilika.
Meneja Mwandamizi wa TANESCO Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Mhandisi, Mahende Mgaya, (pichani juu), amewaambia waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Septemba 27, 2017 na kwamba ifikapo Desemba mwaka huu wa 2017, wananchi na wakazi wa Dar es Salaam wataona ile hali ya kukatika kwa umeme, mara kwa mara imebadilika.
“Tulikuwa na jumla ya miradi mipya 18 ya kuboresha vituo vya umeme jijini Dar es Salaam ili viweze kutoa umeme wa kutosha na wa uhakika, hadi sasa, vituo vinane vimekamilika kabisa na vinafanya kazi, vimebaki vituo 10 ambavyo navyo viko katika hatua za mwisho za kukamilika, na ifikapo Desemba, 2017  vituo vyote 18 vitakuwa vinafanya akzi.” Alitoa hakikisho Mhandisi Mgaya.
Alisema, kufuatia kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na idadi ya watu jijini Dar es Salaam, mahitaji ya nishati ya umeme nayo yameongezeka na hivyo Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), iliamua kuchukua hatua za haraka kuboresha vituo vyake vya umeme ikiwa ni pamoja na  kujenga vipya ili kukidhi mahitaji halisi ya umeme.
“Wafadhili kama vile Benki ya Maendeleo ya Afrika, (AfDB, World Bank, Finland, na Japan), walijitokeza na kufadhili miradi hiyo.”Alifafanua.
Kazi hiyo ya kuboresha vituo hivyo ambavyo ni pamoja na  Mbagala, Kurasini, Kigamboni, Ilala Mchikichini, Kisutu, Mikocheni, Gongolamboto, na maeneo mengine imekuwa ikifanyika tangu miaka miwili iliyopita lakini kutokana na matatizo ya hapa na pale, ikiwa ni pamoja na mapingamizi ya wananchi kuzuia utekelezaji wa miradi hiyo, na wakandarasi, kumepelekea ucheleweshaji.
Maeneeo ambayo yamekuwa yakiathirika zaidi na hali hiyo ya kukatika kwa umeme mara kwa mara ni pamoja na Wilaya ya Temeke, Kigamboni, Ubungo na baadhi ya maeneo ya wilaya ya Kinodnoni.
“Nichukue fursa hii kuwaomba radhi wananchi, hususan wateja wetu, kutokana na hali hii ya kukatika kwa umeme, lakini napenda pia waelewe kuwa hali hiyo inatokana na kazi ambayo tumekuwa tukiifanya, na mara nyingi umeme tunakata siku za weekend, kwa vile shunguli nyingi za kiofisi zinakuwa zimepungua na hivyo inakuwa fursa nzuri kwetu kufanya kazi.” Alifafanua Mhandisi Mgaya.
Alisema, wananchi wanataka umeme, tena ulio bora na wa uhakika, ndio maana TANSCO imeamua kuchukua hatua madhubuti za kuboresha na kujenga vituo vipya vya kupoza na kusambaza umeme ikiwa ni pamoja na kujenga lini mpya za kusafirisha umeme.
“Hatu hizi zote lazima ziwe na changamoto za hapa na pale, lakini kwa kiasi kikubwa TANESCO inaelekea kulitatua tatizo hilo la umeme jijini Dares Salaam na Mkuranga.”. Alisisitiza.

 Wakandarasi na mafundi wa TANESCO wakiwa kazini
 Moja ya vituo ambavyo vimefungwa mitambo mipya ili kuboresha upatikanaji wa umeme jijini Dar es Salaam.
 Kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Kisutu.

POUL MAKONDA AELEZA DHAMIRA YAKE YA KUINUA VIWANDA VIDOGO MKOANI DAR-ES-SALAAM

Ili kwenda sambamba na kasi ya serikali ya awamu ya tano ya kuwa na uchumi wa viwanda Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Poul Makonda ameeleza jitihada wanazozifanya ili kufikia malengo hayo.


Akiongea na waandishi wa habari mapema leo mkuu wa mkoa huyo alisema kuwa serikali ya mkoa wa Dar es salaam inafahamu kuwa kuna viwanda zaidi ya 2000 na katika viwanda hivyo kuna makundi 3 ambayo ni viwanda vikubwa, vya kati na viwanda vidogo.

Lakini wao wameamua kuwekeza katika viwanda vidogo ili viweze kuongezeka kufikia kuwa viwanda vya kati na hatimaye kuwa viwanda vikubwa, na ufanikishaji wa hili utaanza hivi karibuni kutokana kwamba wameshaongea na NSSF kuweza kuwekeza katika viwanda hivi.

Na pia Mh Makonda alisema kuwa kila halmashauri imetakiwa kutenga asilimia 10 kwa ajiri ya wazee, wakina mama na vijana, na kwa mkoa wa Dar es salaam ambao una halmashauri 5 hivyo kuna takribani bilioni sita zimetengwa kwa ajiri ya wajasiliamali wadogo na wao wanachotakiwa kukifanya ni kuleta michanganuo ya biashara zao katika ofisi ya mkuu wa mkoa na kupata fedha hizo zenye riba nafuu.

Aidha mkuu wa mkoa huyo aliongeza kwa kusema wajasiriamali wadogo watapata nafasi ya kuuza bidhaa zao katika maonyesho ya biashara yatakayokuwa yakifanyika kwa mwezi mara moja katika viwanja vya mnazi mmoja jijini dar es salaam na zitauzwa bidhaa za ndani peke yake na hakutakuwa na bidhaa toka nje.


Lakini pia wamachinga watatakiwa kuuza bidhaa zinazozalishwa hapa kwetu ambazo zinatoka katika viwanda vyetu kwani hii itasaidia kukuza soko la ndani na kuongeza wigo wa ajira kwa vijana wa hapa nchini kwetu

NASA WATARAJIA KUANDAMANA KESHO






Muungano wa upinzani nchini Kenya NASA umeitisha maandamano leo Jumanne nje ya makao makuu ya tume ya uchaguzi IEBC mjini Nairobi, ikiwa ni hatua ya kushinikiza kujiuzuru kwa baadhi ya maafisa wa juu wa tume hiyo walioshiriki kuandaa uchaguzi mkuu wa August 8 mwaka huu uliobatilishwa na mahakama ya juu nchini.
Tayari rais Uhuru kenyata ametoa onyo kwa wapinzani ambapo amesema kuwa watakumbana na mkono wa sheria iwapo maandamano yao yataingilia shughuli za kiuchumi zaraia wa nchi hiyo.
”Endeleeni na maandamano yenu, mkigusa mboga za mama wanaouza barabarani, tuko na nyinyi. Mkigusa maduka ya watu tuko na nyinyi. Lakini kama hamna lingine lolote la kufanya isipokuwa kutembea – tembeeni. Mimi nawaambia hata mukinitukana mpaka asubuhi, haitabadilisha dunia”, alisema Kenyata.

WATOTO WENYE AFYA NZURI WANAPATIKANA TANZANIA


Watoto wa Tanzania wana afya nzuri ya maungo kuliko wenzao duniani
Taifa la Tanzania ndilo lenye watoto wenye afya nzuri ya maungo duniani, kulingana na utafiti uliofanywa na wanasayansi wa Australia.


Viwango vya afya ya maungo ya watoto milioni 1.1 walio kati ya umri wa miaka tisa hadi 17 kutoka mataifa 50 vilifanyiwa ukaguzi.
Watoto hao walifanyiwa zoezi la kukimbia umbali wa mita 20,ambalo hukagua afya yao ya maungo.
Grant Tomkinson, mmoja ya watafiti wakuu wa chuo cha Kusini mwa Australia ameiambia BBC kwamba watoto wa Tanzania waliibuka washindi kutokana na utendaji wao.

LULU AFUNGUKA BAADA YA KUKUTANA NA JAH PRAYZAH



Mwimbaji staa wa kike Lulu Diva Kutoka Bongoflevani amekutana na mwimbaji staa wa Zimbabwe EXQ ambaye yupo chini ya Label ya Military Touch inayomilikiwa na msanii wa Zimbabwe Jah Prayzah, ambapo amefanikiwa kupata collabo ya kwanza ya kimataifa na msanii huyo.
Lulu diva ameelezea jinsi alivyoipata hiyo collabo ambapo amesema kuwa …>>>”Jah Prayzah najuana nae since naenda south ku-shoot ngoma yangu ya pili ya Usimwache tokea hapo amekuwa akiona kazi zangu Chanel kubwa Kama MTV,Trace na zingine so huwa ananifatilia na kunipongeza kwa juhudi anazoziona nazifanya katika mziki wangu”
“Aliniambia anakuja Tanzania akifika tuonane alipofika alinitafuta na kuniomba nifanye collabo na msanii wake ambaye yupo chini yake akanisikilizisha nyimbo nikaiona ni nzuri na Mimi naweza fanya kitu kizuri kwa hiyo sikusita kutoa jibu nilikubali hapo hapo sababu niliona ntapata faida Kwani ntaongeza mashabiki kutoka Zimbabwe na fanbase yangu itaongezeka” – Lulu Div
a

LIVERPOOL WAKO TAYARI KUMWACHIA COUTINHO ANDE BARCELONA JANARY

Club ya Liverpool ya England katika kipindi cha usajili cha majira ya joto mwaka huu kilikataa kumuuza staa wao raia wa Brazil Philippe Coutinho kwenda katika club ya FC Barcelona ya Hispania licha ya staa huyo kushinikiza.
Wakala wa Coutinho na watu wa karibu na familia ya Coutinho wamekuwa wakishawishi Coutinho ajiunge na FC Barcelona na wawakilishi hao wapo tayari kusikiliza ofa ya Barcelona kwa mara nyingine tena dirisha la usajili la January litakapofunguliwa.
Habari zilizoripotiwa katika mitandao ya kijamii zinaeleza kuwa Liverpool watakuwa radhi kumuachia Coutinhoaende Barcelona mwezi January kama hawatokuwa dalili katika mbio za Ubingwa, licha ya staa huyo kushinikiz
a

NEW:RAIS AMWGA AJIRA MPYA 3000 JWTZ KUHAMIA DODOMA

   RAIS John Magufuli amesisitiza azma yake ya kujenga Tanzania mpya, kwa kutangaza ajira 3,000 katika Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ujenzi wa reli ya kisasa ya umeme kipande cha Morogoro hadi Dodoma na yeye kuhamia Dodoma mwakani.

Alisema hayo kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha jana, baada ya kutunuku Kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wapya 422 wa jeshi wa cheo cha Luteni Usu wa Kundi la 61/16. Miongoni mwa maafisa haowapya, 32 ni wanawake na wanaume ni 390. Wanafunzi waliotunukiwa vyeo hivyo, wanatoka Shule ya Anga, Shule ya Ubaharia na Chuo cha Kijeshi cha Monduli. Baada ya kutunukiwa vyeo vipya, maafisa hao wapya walivaa vyeo hivyo, kisha kutoa salamu huku wananchi, ndugu, jamaa na marafiki wakishangilia kwa nguvu.
Pia, walikula kiapo cha utii mbele ya Rais Magufuli na baada ya hapo ofisa mpya, Sikujua Peter alivalishwa bawa kwa niaba ya marubani wenzake. Awali, Rais Magufuli alitoa zawadi kwa mwanafunzi aliyefanya vizuri Shule ya Kijeshi ya Kibaharia, Jacob Soka, waliofanya vizuri darasani ni Ally Kitawala na Hamza Msuya, huku Benjamin Fanuel alipata zawadi kutokana na kufanya vyema katika masuala ya urukaji katika anga. Waliofanya vizuri zaidi katika Shule ya Kijeshi ya Monduli ni Hamis Mwantega, aliyefanya vizuri darasani ni Haji Kimaro.
Wanafunzi hao waliotunukiwa vyeo hivyo vipya, walipita mbele ya Rais kwa gwaride la mwendo wa pole na kasi, huku wakishangiliwa na watu mbalimbali waliofika uwanjani hapo kushuhudia kutunukiwa kwa kamisheni zao. Ajira mpya jeshini Rais alieleza kuwa amefurahi kutoa kamisheni kwa maafisa hao wapya 422, lakini pia jeshi ni lazima liwe pia na wanajeshi wa kawaida.
“Kwa kutambua hilo natangaza rasmi nafasi 3,000 za kuajiri wanajeshi wapya. Na hao watakaoajiriwa wawe wamemaliza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). Lengo ni tuwe na maaskari wa kutosha na jeshi la kisasa zaidi,” alisema Rais Magufuli, ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu. Alipongeza JWTZ, Polisi, Zimamoto, Uhamiaji, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, kwa kazi nzuri ya kulinda amani ya nchi. Alitaka wananchi kuendelea kuunga mkono vyombo hivyo.
Kuhusu suala la ajira, Rais alisema katika mwaka huu wa fedha, serikali inatarajia kuajiri jumla ya watumishi 50,000 wa sekta mbalimbali, ikiwemo wanajeshi, madaktari na walimu. Kuhamia Dodoma Rais alisema uamuzi wa kuhamia Dodoma kutoka Dar es Salaam, ulitolewa na Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1973, lakini kwamba tangu wakati huo utekelezaji wake ulikuwa mgumu. Lakini, alisema serikali yake imedhamiria kuhamia Dodoma na kwamba hadi sasa watumishi 3,000 wamehamia Dodoma akiwemo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Alitangaza kuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan atahamia baadaye mwaka huu na yeye mwaka kesho. “Mwaka huu atahamia Makamu wa Rais na mwaka kesho nahamia mimi. Yule ambaye hatahamia huko na kukaa Dar kazi hana,” alisema Mkuu huyo wa Nchi. Ndege, reli ya umeme Rais alisema hatua mbalimbali ambazo Serikali ya Awamu ya Tano, imechukua kudhibiti matumizi ya serikali, zimeiwezesha kupata fedha za kutosha, hivyo kuiwezesha kujenga miradi mikubwa mbalimbali, mfano kununua ndege za kisasa sita, zitakazoboresha usafiri wa abiria wa kawaida na watalii.
Mradi mwingine ni ujenzi wa reli ya kisasa ya umeme (standard gauge). “Tumeanza kujenga reli ya kisasa kilometa 300 kutoka Dar hadi Morogoro. Na wiki ijayo tunatarajia mkataba mwingine mpya utasainiwa kwa ajili ya ujenzi wa kipande cha reli kutoka Morogoro kwenda Dodoma,” alitangaza. Madeni ya wanajeshi Rais Magufuli alisema juzi alikutana na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Venance Mabeyo na makamanda wa juu jeshini, kujadili madeni na maslahi mbalimbali ya wanajeshi, ambapo walikubaliana wataanza kulipa madeni hayo kuanzia wiki ijayo.
Umeme Bonde la Rufiji Magufuli alisema serikali yake itatimiza ndoto ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ya mwaka 1975, ambapo alitaka kujenga bwawa la kufua umeme la Stiegler’s Gorge katika Bonde la Mto Rufiji mkoani Pwani, kwa lengo la kuondoa kero ya umeme nchini. Alisema mradi huo wa Stiegler, utazalisha megawati 2,100 za umeme na kumaliza tatizo la umeme nchini. Alisema umeme unaozalishwa nchini kwa sasa ni megawati 1,460 tu ambazo hazitoshi, hasa wakati huu serikali inajenga uchumi wa viwanda na kukaribisha wawekezaji mbalimbali.
“Tumetangaza tenda ya kujenga Stieglers na tayari makampuni 50 ya kimataifa yameomba tenda hiyo,” alisema Rais na kuongeza kuwa fedha za kutekeleza mradi huo mkubwa zipo. Uchumi wapaa Rais alisema uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi na Tanzania ni moja ya nchi tatu barani Afrika, zinazoongoza kwa uchumi kukua, ya kwanza ikiwa ni Ethiopia.
Uchumi wa Ethiopia unakua kwa asilimia 8, wakati wa Tanzania unakua kwa asilimia 7.1 na mwakani utakua kwa asilimia 7.2 sawa na wa India. Urais mateso Magufuli alisema urais ni msalaba, kazi ngumu mno na ya kujitoa msalaba. Alisema yeye amejitoa sadaka ili kunyoosha nchi na mafisadi. “Urais ni mateso. Ni shida kubwa kuwa Rais. Nayaona mateso.
Niliomba urais kwa kujaribu, nikasukumiziwa huko, hata hivyo nimejitoa sadaka kwa ajili ya nchi yangu na Watanzania,” alisema. Alisisitiza, “Niliingia bila kutoa rushwa. Hakuna aliyenichangia wakati nagombea urais, hivyo nitaendelea kunyoosha nchi. Hili la kutumbua, watu watatumbuka kweli kweli, nataka mafisadi watubu, nataka Tanzania mpya.” Mialiko safari za nje Rais alisema amepata jumla ya mialiko 60 ya kwenda nje ya nchi, lakini hakwenda, kwa sababu bado anasafisha nchi. “Nimeacha mialiko 60. Wengi tu wanaomba uje.
Nije kufanya nini? Nasafisha kwanza nyumba yangu. Niliomba urais si wa kutembelea nchi nyingi. Kwanza mimi nilishatembelea nchi nyingi kabla sijawa rais. Huu sasa ni wakati wangu wa kuchapa kazi,” alisema Rais. Viongozi walioshuhudia wanajeshi hao wapya wakitunukiwa vyeo ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Jaji Mkuu mstaafu, Augustino Ramadhani, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Hussein Mwinyi, Mbunge wa Ngorongoro William ole Nasha, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, wakuu wa wilaya za Arusha, wakurugenzi wa wilaya.

MPOTO AIWAKILISHA TANZANIA UTALII WA KIMATAIFA NCHINI CHINA





Msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto amewasili nchini China kwaajili ya kuiwakilisha Tanzania katika Tamasha la Utalii Duaniani. 
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Kitendawili’, aliondoka nchini Tanzania siku ya Jumatatu akiwa ameambatana na kikundi chache cha ngoma kikiwa na jumla ya watu sita pamoja na yeye mwenyewe.
Akiongea na mwandishi wetu akiwa nchini humo baada ya kuwasili katika eneo ambalo litafanyika tamasha hilo, Mpoto amesema Alhamisi hii wataanza kufanya maonyesha hayo katika tamasho hilo ambalo linayakutanisha mataifa mbalimbali duniani.

MPOTO AIWAKILISHA TANZANIA UTALII WA KIMATAIFA NCHINI CHINA





Msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto amewasili nchini China kwaajili ya kuiwakilisha Tanzania katika Tamasha la Utalii Duaniani. 
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Kitendawili’, aliondoka nchini Tanzania siku ya Jumatatu akiwa ameambatana na kikundi chache cha ngoma kikiwa na jumla ya watu sita pamoja na yeye mwenyewe.
Akiongea na mwandishi wetu akiwa nchini humo baada ya kuwasili katika eneo ambalo litafanyika tamasha hilo, Mpoto amesema Alhamisi hii wataanza kufanya maonyesha hayo katika tamasho hilo ambalo linayakutanisha mataifa mbalimbali duniani.





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemaliza ziara yake ya kikazi ya siku 6 Mkoani Arusha leo Septemba 25, 2017 ambapo tayari amewasili Jijini Dar es salaam mara baada ya kumaliza ziara yake.
3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda pamoja na viongozi wengine wa Mkoa wa Dar es Salaam mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam wakati akitokea Mkoani Arusha.
2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam wakati akitokea Mkoani Arusha.
4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda pamoja na viongozi wengine mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam wakati akitokea Mkoani Arusha.

MAGAZETI YA LEO TAREHE 23 SEPTEMBER 2017

Magazeti ya Tanzania leo Septemba 26, 2017

21 mins ago Comments Off on Magazeti ya Tanzania leo Septemba 26, 2017
Fahamu yote yaliyojiri