Marais watano wa zamani nchini Marekani wamekusanyika katika tamasha la kuchangisha fedha za kuwasaidia waathirika wa janga la kimbunga ambacho kiliyakumba maeneo kadha ya Marekani.
Rais Barack Obama, George W Bush, Bill Clinton, George HW Bush na Jimmy Carter wote walikutana Texas hapo jana kwa lengo la kuwasaidia wale walikumbwa na janga la vimbunga Irma na Maria.
Marais hao wamefanikiwa kuchangisha kiasi cha dola za kimarekani milioni 31 hadi sasa mchango ambao utasaidia jamii za Florida, Puerto Rico na visiwa vya Marekani vya Virgin vilivyopigwa na kibunga.