Haki za kidemokrasia zimezidi kuonyesha kutoheshimiwa kaitka eneo la
Afrika Mashariki ambapo Kenya, Tanzania na Rwanda zimeshuka viwango
katika ripoti mpya juu ya hali ya uhuru duniani (global status of
freedom).
Kenya
Utafiti uliofanywa na taasisi binafsi ya Freedom House lenye
makazi yake Washington, ambalo sio la kisiasa wala serikali, linaeleza
kasoro zilizojitokeza katika mchakato wa uchaguzi wa urais Kenya.
Ripoti hiyo imeeleza kuwa uchaguzi ulikuwa na utata, ambao “marudio
ya uchaguzi yalioamrishwa na mahakama yalifanyika bila ya kuwepo mageuzi
ya msingi, matukio ya vurugu za kisiasa na kususiwa kwa uchaguzi huo na
mgombea mkuu wa upinzani, Raila Odinga.
“Mambo haya yanatia dosari ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta, ambapo
alidai kupata kura asilimia 98 ya kura zote pamoja na kuwepo mahudhurio
ya chini ya wapiga kura,” ripoti hiyo imesema.
Taasisi hiyo imeipa Kenya asilimia 48 kati ya 100 --- ikionyesha
demokrasia imeshuka kutoka asilimia 51 vile ilivyokuwa imeripotiwa mwaka
2017. Hali hiyo inaifanya Kenya kuwa kati ya nchi 58 zinazoelezwa kuwa
“hazina uhuru kamili.”
Tanzania
Taasisi hiyo ya Freedom House pia imeripoti kushuka kwa haki za
kidemokrasia nchini Tanzania, ambayo ilikuwa iko juu kidogo kuliko
Kenya.
Tanzania, ambayo imepewa asilimia 52 katika ripoti hiyo mpya na
asilimia 58 katika utafiti wa mwaka 2017, imewekwa katika kikundi cha
nchi “zisizo na uhuru kamili.”
“Serikali ya Rais John Magufuli – ambaye alichukua madaraka mwaka
2015 kama ni mwanachama pekee wa chama tawala nchini – alianzisha
ukandamizaji wa wapinzani, kuwafunga wanasiasa wa upinzani, akifunga
vyombo vya habari na kuwakamata wananchi ambao wanatoa maoni yao ya
kukosoa katika mitandao ya kijamii,” utafiti huo wa mwaka 2018 umeeleza.
Uganda
Uganda imeonyesha mabadiliko kwa kupanda daraja kutoka
“kutokuwepo uhuru kabisa” kwenda “zisizo na uhuru kamili” japokuwa hivi
sasa imepewa daraja la asilimia 37 ambayo bado iko chini kuliko Kenya na
Tanzania.
Taasisi ya Freedom House inafanya tathmini yake ya uhuru nchini
Uganda kwa kigezo cha “kuamka kwa sekta ya habari na utayari wa
waandishi wa habari, mitandao ya jamii na wananchi kutoa maoni yao.”
Hata hivyo, ripoti hiyo imeongeza kuwa “hali ya kisiasa imeendelea
kuwa kandamizi chini ya utawala wa muda mrefu wa Rais Yoweri Museveni.
Rwanda
Rwanda imeorodheshwa kati ya nchi 49 ambazo “haziko huru.”
Imepewa asilimia 23 – ambayo imeshuka kidogo kutoka asilimia 25 ambayo
ilipata mwaka jana katika ripoti ya Freedom House. Utafiti mpya hautoi
maelezo juu ya daraja waliopewa Rwanda.
Nchi nyingine
Burundi, Somalia na Sudan Kusini pia zimeelezwa kuwa “haziko huru” katika ripoti hiyo.
Sudan Kusini imepewa daraja ya pili kutoka chini—pointi mbili--- kati
ya nchi 195 ambazo tafiti hiyo ilifanywa na Freedom House. Somalia
inaunafuu kidogo, ambapo inanukta saba. Burundi, pia imegubikwa na
migogoro ya ndani lakini sio kwa kiwango ambacho Somalia na Sudan Kusini
imeathiriwa na migogoro hiyo, imepata daraja ya asilimia 19.