VYOMBO VYA DOLA KUWASHUGHULIKIA WANAOTENGENEZA DATA ZA UONGO


Image result for MAGUFULI
Rais John Pombe Magufuli amefunguka na kuvitaka vyombo vya dola nchini viwashungulikiwe watu ambao wamekuwa wakipika data za uongo za serikali na kuzichapisha sehemu mbalimbali na kusema watu hao wanapaswa kufikishwa mahakamani.
Rais Magufuli amesema hayo leo katika hafla ya kuwatunuku vyeti vya pongezi maaalum kwa wajumbe waliohusika kuchunguza kiwango, aina ya madini katika mchanga wa madini ambao ni makinikia. Rais Magufuli amesema kuwa kuna haja Waziri wa Sheria na vyombo vya dola kuangalia namna inavyowezekana kuwashughulikia watu ambao wanapika data.

"Niwaombe Watanzania wengi tofauti na wale wachache wanaopiga kelele muwapuuze, mtu ambaye anabadili data za serikali na kusema kuwa uchumi umeshuka nadhani wanapaswa kuchukuliwa hatua vyombo vya dola na wewe Profesa Kabudi ni Waziri wa Sheria muanze kuangalia watu wa namna hii ambao kwao kubadili Takwimu wanaona kitu kidogo.

"Nafikiri kuna sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 na kunakifungu kinasema mtu anayebadilisha Takwimu za serikali anaweza kufungwa hata miaka 2 jela, kwanini hatuvitumii hivi? Unakuta mtu anazungumza makusanyo ya serikali yameshuka wakati anajua kabisa si kweli" alisema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli aliendelea kusisitiza kuwa mapato ya nchi hayajashuka ndiyo maana Serikali imeweza kununua ndege zaidi ya sita kwa mpigo, serikali imeweza kujenga barabara kwa fedha za ndani, na kusema serikali imeweza kujenga reli kwa kuwa uchumi wake ni mzuri.

HELKOPTA YAUWA WATANO KENYA


WATU watano wanahofi wa kufa akiwemo rubani wa helikopta iliyokuwa ikitoka eneo la Jarika Kaunti ya Nakuru kuelekea Tipis, Mau Narok kwenye kampeni za Rais Uhuru Kenyatta, kuanguka katika Ziwa Nakuru.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini Kenya (KCAA), Gilbert Kibe, helikopta hiyo ilikuwa na watu watano akiwamo rubani wake Bootsy Mutiso.
“Hadi sasa hakuna tena matumaini ya kupata majeruhi kwa sababu helikopta hiyo imezama kwenye ziwa hili na juhudi za uokozi zinaendelea kwa kuleta boti kutoka Ziwa Naivasha, ila sasa ndege zinapita juu kuangalia iwapo wataona chochote na kusaidia,” alisema Kibe.
Alisema katika ziwa hilo la Nakuru hakukuwa na boti karibu hivyo imebidi boti itoke Naivasha ambako ni mbali na hivyo uwezekano wa kuwapata waathirika wakiwa hai ni mdogo.
Kibe alisema katika helikopta hiyo mbali ya rubani, kulikuwa na wanaume watatu na mwanamke mmoja ambao hata hivyo hadi jana jioni majina yao yalikuwa hayajatambuliwa. Alisema helikopta hiyo inamilikiwa na Kampuni ya Flex Air Charters.
Awali Seneta wa Nakuru, Susan Kihika alisema abiria watatu kati ya hao wanne ni watumishi wenzake katika kitengo cha mawasiliano. Alisema helikopta hiyo ilianguka muda mfupi baada ya kuruka kutoka Jarika Kaunti na mashuhuda wengine wanasema waliiona ikiruka umbali wa chini kabla ya kuanguka.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kitengo cha Taifa cha Maafa, Pius Masai alisema wametuma helikopta moja ya Polisi kwenda kusaidia uokozi. “Pia tumetuma wazamiaji kutoka Jeshi la Wanamaji la Kenya wasaidie kutafuta helikopta hiyo iliyozama ziwani,”alisema Masai.
Baada ya kutokea kwa ajali hiyo viongozi mbalimbali walifika kwenye ziwa hilo akiwemo Gavana wa Nakuru, Lee Kinyanjui na viongozi wengine wakiwemo wabunge wa eneo hilo.
Wabunge hao ni Samuel Arama ( Nakuru Magharibi), David Gikaria (Nakuru Mashariki), Jayne Kihara (Naivasha) na Liz Chelule (Mwakilishi wa wanawake). Pia alikuwepo Spika wa Kaunti ya Nakuru, John Kairu.

TETEMEKO LAIKUMBA MPANDA


TETEMEKO lililovikumba vitongoji na viunga vya Mji wa Mpanda mkoani Katavi pamoja na maeneo ya nchi jirani, ni la 5.2 katika kipimo cha richa.
Akizungumza jana mjini Dodoma, Mjiolojia Mwandamizi wa Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), Gabriel Mbogoni alisema kwa kawaida tetemeko la kipimo hicho hugusa eneo kubwa kutokana na ukubwa wake.
Mbogoni alisema tetemko hilo lilitokea kwa takribani sekunde 20 hadi 30. “Eneo hilo lililokumbwa na tetemeko lipo kwenye Bonde la Ufa, kwani ni kawaida kwa maeneo hayo kukumbwa mara kwa mara na matetemeko na kubwa zaidi lililowahi kutokea lilikuwa la mwaka 1969 ambalo hilo ni la mwaka 1982 la 5.0 kipimo cha richa na mengine madogo madogo ya 3.7, 3.8 na 4.0 katika kipimo cha richa.
Alisema tetemeko hilo la Mpanda, lilitokea saa 3.30.12 asubuhi, na kutokana na kutokea kwenye Bonde la Ufa inawezekana pia liligusa eneo kubwa mkoani Katavi, Rukwa na hata maeneo ya mpakani ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na Zambia.
Mbogoni alisema maeneo yaliyokumbwa na tetemeko hilo ni la Kaskazini-Mashariki umbali wa umbali wa kilometa 46 kutoka mji wa Mpanda. “Eneo hilo lipo umbali wa kilometa 16 Kaskazini- Mashariki mwa mji wa Kalambo na umbali wa kilometa 100 Mashariki wa Mbuga ya Mahale iliyopo karibu na Ziwa Tanganyika,” alieleza.
Mbogoni alitoa ushauri kwamba, pale inapotokea kwamba kuna tetemeko, watu wasitoke ndani ya nyumba kama wamo humo kutokana na kasi yake ya kusafiri umbali wa kilometa nane hadi 13 kwa sekunde moja.
Alisema hayo baada ya kuambiwa kuwapo kwa taharuki kubwa kwa wakazi wa Mji wa Mpanda na wengi kuzikimbia nyumba zao. Miongoni mwa wakazi waliokumbwa na taharuki hiyo ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Raphael Muhuga ambaye wakati huo alikuwa kanisani na waumini wenzake.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu, Muhuga alikiri kuwa tetemeko hilo lilikuwa kubwa la kutosha kwamba katika maisha yake hajawahi kushuhudia mtikisiko mkubwa wa ardhi. “Nilikuwa kanisani katika ibada ya misa takatifu ya Jumapili wakati huo.
Hakika lilikuwa kubwa la kutosha niliangalia saa lilianza saa tatu na dakika kumi na kudumu kwa dakika moja hivi, ilisababisha taharuki kubwa kwa waumini kanisani humo hususani watoto walikimbilia nje, sisi watu wazima tulikuwa tukiangalia paa la kanisa kama litatuangukia.
Mungu Mkubwa ibada iliendelea kama kawaida hadi mwisho,” alieleza. Alisema hadi sasa hakuna maafa yoyote ambayo yamesharipotiwa. Mkazi wa Mpanda Mjini, Adamu Juma alieleza kuwa wakati huo alikuwa akihemea sokoni, na alishuhudia wafanyabiashara wakitelekeza maduka yao na kukimbilia walikodhani ni salama kwa maisha yao.
“Wakati huo nilikuwa ndani ndipo ghafla nikahisi kuta za nyumba zikitikisika kwa nguvu nilitaharuki na kukimbilia chini ya uvungu wa meza ya chakula ili hata ukuta ukianguka usiniumize... Nilitetemeka sana kwa hofu,” alisema Mariam Yusufu anayeishi mjini Mpanda.
Katika siku 365 zilizopita, Tanzania imekumbwa na matetemeko ya ardhi manane yenye ukubwa mbalimbali kuanzia 4.4 hadi 5.9. Baadhi ya matetemeko ukiachia lile lililotokea jana Mpanda, Katavi lenye ukubwa wa magnitude 5.2 kina cha kilomita 10, miezi mitano iliyopita lilitokea tetemeko la magnitude 4.4 huko Misasi, Mwanza.
Aidha, miezi 7 iliyopita tetemeko jingine lilitokea Utete kwa kipimo cha Magnitude wa 4.9 na kina cha kilometa 12 huku tetemeko baya kabisa lilikuwa la Nsunga, Kagera Tanzania ambalo lilikuwa na ukubwa wa Magnitude 5.9 na kina cha kilometa 40.4: Pia eneo la Msanga Dodoma lilipatwa na tetemeko la ukubwa wa Magnitude 5.1 na kina cha kilometa 10. Imeandikwa na Magnus Mahenge, Dodoma na Peti Siyame, Mpanda.

TUKO TAYARI KWA MABADILIKO TANZANIA ONE



UONGOZI wa Kampuni ya uchimbaji madini aina ya tanzanite ya TanzaniteOne Mining Limited, umejitokeza na kutangaza wazi kuwa wako tayari kushirikiana na serikali katika kupitia upya makubaliano ya mkataba wa uchimbaji na kuhakikisha kuwa taifa linanufaika na vito hivyo.
“Wakati tunasubiri taratibu za serikali kukamilika kabla ya kuanza majadiliano, tunapenda kumhakikishia Mheshimiwa Rais John Magufuli na Watanzania kwa ujumla kwamba sisi kama TanzaniteOne tutatoa ushirikiano utakaowezesha kuwa na hitimisho lenye tija kwa taifa letu,” ilisema taarifa kutoka kwenye uongozi wa kampuni hiyo.
Taarifa hiyo rasmi kutoka Bodi ya Uongozi wa TanzaniteOne Limited iliyosainiwa na Katibu wa Kampuni, Kisaka Mnzava, inasema kuwa viongozi wake wako tayari kufuata maelekezo yoyote yatakayotolewa na serikali baada ya mazungumzo yanayotarajiwa kufanyika baina ya kampuni hiyo na serikali.
“TanzaniteOne iko tayari kuingia kwenye majadiliano na serikali kwa ajili ya kufanya mapitio ya mkataba husika pamoja na kurekebisha taratibu zote za uchimbaji na biashara ya madini nchini kwa manufaa ya Watanzania wote,” alifafanua Mnzava.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo rasmi, TanzaniteOne itashirikiana bega kwa bega na timu ya serikali itakayoundwa kwa ajili ya kutekeleza wajibu huo, lengo likiwa ni kuwezesha madini ya tanzanite yanayopatikana Tanzania peke yake, kuwa yenye manufaa kwa taifa.
“Tunafanya hivyo kwa sababu mbili: Kwanza ni kutambua juhudi zinazofanywa na Rais John Magufuli na hatua anazochukua kulinda rasilimali za taifa na kuhakikisha kuwa madini yanawanufaisha Watanzania wote kwa ujumla.”
“Pili tunaamini kuwa wabia wa kampuni ya TanzaniteOne, mbao ni Watanzania wazawa wana wajibu wa kushiriki katika mchakato mzima wa kuliwezesha taifa kunufaika na rasilimali za madini nchini,” waliongeza viongozi wa TanzaniteOne katika taarifa yao kutoka Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara.
TanzaniteOne Mining Limited ni kampuni ya ubia baina ya wafanyabiashara wa jijini Arusha, Hussein Gonga na Faisal Shahbhat kupitia Sky Associate wanaomiliki asilimia 50 za hisa na serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (Stamico) lenye hisa 50 pia.
Wakati wa ziara yake ya uzinduzi wa Barabara ya KIA-Mirerani, Septemba 27, mwaka huu, Rais Magufuli aliagiza kupitiwa upya mkataba wa uchimbaji na biashara ya madini hayo ya vito baina ya Sky Associate na Stamico.
Oktoba 19, mwaka huu, baada ya kushuhudia kutiwa saini makubaliano baada ya mazungumzo baina ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya uchimbaji dhahabu ya Barrick Gold Corporation, Rais Magufuli alimuagiza Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi kwamba timu ya serikali ianze kufanyia kazi madini ya tanzanite na almasi.

AGUERO AREJEA UWANJANI

Image result for photo of sergio aguero

Sergio Aguero amefungia Manchester City mabao 176 - amepungukiwa na moja tu kufunga rekodi.
Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero amerejea mazoezini siku 11 baada yake kuvunjika ubavu katika ajali ya barabarani mjini Amsterdam.
Aguero, 29, alikuwa ametarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa wiki kadha
Hata hivyo, alirejea kufanya mazoezi mepesi Jumanne.
City wamesema mchezaji huyo wa Argentina ataendelea "kuimarisha hali yake ya mwili siku zijazo akilenga kurejea kikosini".
Aguero anahitaji bao moja pekee kufikia rekodi ya ufungaji mabao City ya Eric Brook ambayo ni mabao 177.
City wanaongoza Ligi ya Premia kwa wingi wa mabao, mbele ya Manchester United, na watakutana na Stoke siku ya Jumamosi.
Aguero alijeruhiwa akiwa kwenye teksi akisafiri baada ya kuhudhuria tamasha ya muziki. Teksi hiyo iligonga boriti ya taa barabarani.
Alikuwa ameenda Amsterdam kumuona nyota wa muziki kutoka Colombia Maluma akitumbuiza.

BAADA YA SULUHU POVU LAMWAGIKA KATI YA MORINHO NA KLOPP

Image result for photo from the match liverpool vs manchester united 2017
 Baada ya matokeo ya 0-0, Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp ametoa povu akituhumu mbinu za mpinzani wake, Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho kwa kusema kuwa yeye hawezi kutumia mbinu hizo.
Mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Anfield ulishuhudia United ikicheza muda mwingi ikiwa inazuia huku Liverpool ikishindwa kupenga ngome ya wapinzani wao hao.
Klopp amesema kuwa mbinu hizo za kuzuia yeye hawezi kuzitumia kwa kuwa hazimfai.
“Nafikiri sisi tulistahili kupata pointi tatu, tulicheza vizuri, nafikiri Man United walikuja kutafuta pointi hapa na wameipata, sisi tulitaka pointi tatu hatujazipata,” alisema Klopp ambaye alionyesha kutofurahia mbinu za wapinzani wake kupaki basi.

Image result for PHOTO OF SIMON MSUVA IN MOROCCO
Simon Msuva ameendelea kuwa na mwendelezo mzuri katika maisha yake ya soka la kulipwa,  hiyo ni baada ya kutengeneza bao moja katika ushindi wa mabao 2-0 wa timu yake Difaa Hassan El Jadida dhidi ya Chabab Rif Hoceima kwenye Uwanja wa Ben Ahmed El Abdi mjini El Jadida.
Msuva alipiga krosi katika dakika ya 64 katika mchezo wa Kombe la Ligi Morocco ikatua kichwani kwa Adnane El Ouardy akaudondoshea mpira nyavuni kuipatia bao la kwanza Jadida, kabla ya Hamid Ahadad kufunga la pili dakika ya 89.
Hivyo, Jadida metinga Nusu Fainali kwa ushindi wa jumla wa 3-2, baada ya wiki iliyopita kufungwa 2-1 Uwanja wa Mimoun Al Arsi mjini Al Hoceima, siku ambayo Msuva aliifungia timu yake bao muhimu la ugenini.
Katika mchezo huo wa wikiendi hii ya jana, Msuva alipumzishwa dakika ya 92 na nafasi yake kuchukuliwa na Tarik Astati.
Baada ya mchezo huo, Difaa ambayo ina viporo viwili dhidi ya FUS Rabat na Wydad Cassablanca, itamenyana na FAR Rabat Uwanja wa Prince Moulay Abdallah mjini Rabat

VICTOR MOSSES NJE YA UWANJA KWA MWEZ MMOJA

Image result for PHOTO OF VICTOR MOSES

Siku chache tangu wapate kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Crystal Palace, wimbi la majeruhi limeendelea kuitesa Chelsea baada ya Victor Moses naye kuingia kwenye orodha ya majeruhi sambamba na N'Golo Kante na Morata.
Moses ameanza mechi saba katika michuano yote msimu huu, lakini Mnigeria huyo atakuwa nje kwa sababu ya majeraha ya misuli.
Mchezaji huyo alitolewa Chelsea ikichezea kichapo cha 2-1 dhidi ya Crystal Palace wikiendi iliyopita, na kwa mujibu wa The Telegraph, Moses atakuwa nje ya dimba hadi baada ya mapumziko ya kimataifa.
Majeraha ya Moses ni pigo kwa Chelsea kwani tayari wamempoteza N'Golo Kane na Alvaro Morata ambao ni majeruhi pia.
Morata anaweza kurejea kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Roma Jumatano usiku, lakini Kante atakuwa nje hadi mwanzoni mwa mwezi ujao.

MESSI AFIKISHA GOLI LAKE LA 100

Image result for photo of lionel messi


Lionel Messi alifunga bao lake la 100 katika soka la Ulaya akiwa na  Barcelona,Ushindi huo wa barcelona umewafanya wakaribie kufuzu hatua ya makundi ya michuano ya klabu bingwa barani ulaya.
Olympiacos ambayo ilikuwa ugenini imeambulia kipigo cha goli 3 kwa moja kutoka kwa barcelona,katika mchezo huo messi alifikisha idadi ya magoli 100  katika michezo 122 soka la ulaya, Christiano Ronaldo ndiyo mchezaji
mwingine kuwahi kufikisha idadi ya magoli hayo katika michezo 143.

RASHFOD AIBEBA MAN U


 Image result for PHOTO OF MARCUS RASHFORD
Marcus Rashford, jana alifunga bao pekee katika mchezo wa Champions League dhidi ya Benfica na kuiweka United kileleni mwa kundi lao lakini Rashford huyo huyo anaingia kwenye kundi la majeruhi la Paul Pogba, Eric Bailly na Morouane Fellaini.
Chelsea nao jana walikuwa uwanjani wakishuhudia timu yao ikiongoza mabao mawili na baadaye yakarudi yote lakini wakafanikiwa kutoka suluhu ya mabao matatu kwa matatu dhidi ya As Roma.
Chelsea ambao walimkaribisha Alvaro Morata aliyetoka kuwa majeruhi bado wanamkosa kiungo wao mkabaji Ngolo Kante ambaye aliumia wakati akiwa katika majukumu kuitumikia timu yake ya taifa.
Nafasi ya Kante ilichukuliwa na Tiomoue Bakayoko ambaye taarifa zinasema na yeye ameumia baada ya mchezo wa jana huku mlinzi wa kati David Luiz naye akipata majeraha yatakayomuweka nje kwa muda.
Kocha wa klabu hiyo Antonio Conte amesema hawezi kuhatarisha afya za wachezaji wake na kwa kuwa wameumia kidogo atawaacha nje ya uwanja hadi pale watakapokuwa fiti kuanza kucheza.
Wakati huo huo Antonio Conte amemuambia kocha wa Manchester United Jose Mourinho kwamba aangalie timu yake na aache kufuatilia masuala ya klabu ya Chelsea na kushangazwa na kitendo cha Mou kuwafuatilia.
Kauli ya Antonio Conte inakuja baada ya Jose Mourinho kudai kwamba kuna makocha ambao wachezaji wao wakipata maejeraha huwa wanapiga sana kelele kauli ambayo ilionekana kama kijembe kwa Conte.

CAVANI AOMBA KUSAJILIWA MAN CITY

www.kwanguleo.blogspot.com

Mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Edinson Cavani kwa mujibu wa habari ameiomba Manchester City kumsajili.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay mustakabali wake Parc de Princes umekuwa wa mashaka baada ya kuwa na mvutano dimbani baina yake na Neymar mwezi uliopita.
Katika kipidi cha pili cha mechi ambayo PSG walishinda 2-0 dhidi ya Lyon Septemba 17, Cavani na Neymar walikuwa wakigombea kupiga penalti, ambayo hata hivyo Cavani aliikosa.
Kwa mujibu wa Don Balon, mshambuliaji huyo wa zamani wa Napoli anaamini atakuwa tishio mbele ya goli kwa Man City na anaitegemea timu hiyo ya Guardiola kumsajili, lakini pia akiwa anazifikiria Real Madrid, Manchester United au Everton.
Madrid wanataka kusajili mshambuliaji mpya na wanayo machaguzi mengi, kadhalika Cavani atakuwa na wakati mgumu kumpokonya namba Romelu Lukaku Old Trafford.
Everton watahitaji nguvu nyingi kumshawishi Cavani kutua Goodison kutokana na kiwango chao duni cha sasa, wakiwa chini mkiani mwa msimamo wa ligi. Hakuna taarifa zozote kama Manchester City wanafikiria kumsajili Cavani.

KOCHA MPYA MSAIDIZI WA ASIMBA ATAMBULISHWA

Klabu ya Simba imemtangaza Masudi Juma ria wa Burundi kuwa kocha wake msaidizi akichukua nafasi ya Jackson Mayanja.
Kocha huyo mpya aliwasili mchana wa leo nchini kwa ajili ya kusaini mkataba wa kufundisha Simba akisaidiana na Joseph Omog.
Baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) mjini Dar es Salaam, Juma alisema: “Nimekuja kuwa kocha Msaidizi wa Simba chini ya kocha aliopo kwa sasa. Nataka kusaidia Simba ifanikiwe kutwaa mataji zaidi, najua hiyo ndiyo kiu kubwa.”
Kocha huyo ambaye mwaka 1995 aliichezea Burundi katika michuano ya Vijana ya Dunia ya FIFA nchini Qatar alionekana kuwa mchangamfu katika mazungumzo yake.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Prince Louis ya Burundi, Inter Star za Burundi na Rayon Sport ya Rwanda amesema anafurahi kuja kufundisha Simba timu kubwa Afrika na anaamini atajifunza zaidi, hususan akifanya kazi chini ya kocha mzoefu zaidi, Omog.
Masudi Juma amesema atasaini mkataba na Simba kesho Ijumaa.

LIGI KUU BARA INAENDELEA LEO


www.kwanguleo.blogspot.comLigi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), inatarajiwa kuendelea leo Ijumaa Oktoba 20, 2017 kwa mchezo mmoja utakaokutanisha timu za Mwadui na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mwadui mkoani Shinyanga.
Timu hizo zinakutana katika Raundi ya Saba katika duru hili la kwanza la VPL ambalo mbali ya Kampuni ya Simu ya Vodacom - wadhamini wakuu, wadhamini wengine ni Kituo cha Televisheni cha Azam (Azam Tv) na Benki ya KCB ambayo huduma zake za kibenki zinazidi kushamiri nchini.
Wadhamini hao wanachagiza ligi hiyo ambayo itaendelea Jumamosi Oktoba 21 kwa michezo sita  itakayofanyika kwenye viwanja tofauti huku mechi nyingi zikipata fursa ya kuonyeshwa kwenye chaneli mbalimbali za Azam Tv kupitia king’amuzi cha Azam.
Michezo ya Jumamosi itakutanisha timu za Mbao na Azam kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, wakati Lipuli itakuwa mwenyeji wa Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa ilihali Ruvu Shooting watakuwa wageni wa Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Jumamosi hiyo hiyo Simba yenye mabadiliko kidogo kwenye benchi la Ufundi, itawaalika Njombe Mji kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam huku Ndanda ikicheza na Singida United kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Wakati Jumamosi hiyohiyo tena, Mtibwa Sugar wakicheza na Tanzania Prisons ya Mbeya kwenye Uwanja wa Manungu mkoani Morogoro, Jumapili kutakuwa na mchezo mmoja tu - ambao ni kati ya Stand United na mabingwa watetezi, Young Africans ya Dar es Salaam - mchezo utakaopigwa Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

IEBC KAMISHNA AKIMBILIA MAREKANI BAADA YA KUJIUZULU


Roselyn Akombe

KAMISHNA mmoja kati ya makamishna saba wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC), Roselyn Akombe (pichani) amejiuzulu wadhifa wake, ikiwa ni siku saba zimebaki kufikia uchaguzi mpya wa rais utakaofanyika Oktoba 26, mwaka huu.
Ofisa huyo alitoa taarifa ya kujiuzulu kwake akiwa jijini hapa na kusema hawezi kuendelea kufanya kazi katika tume hiyo aliyodai kuwa imegawanyika. Alisema kujiuzulu kwake pia kumechangiwa na hali ya mazingira ya sasa ya kisiasa nchini humo huku akisisitiza kuwa uchaguzi huo ukifanyika Oktoba 26 hautakuwa huru wala wa haki. “Siwezi kuendelea kufanya kazi katika mazingira kama hayo, kuna kila dalili zinazoonesha wazi kuwa uchaguzi hauwezi kuwa huru wala wa haki,” alisema Akombe.
Akombe aliondoka Kenya Oktoba 17 kwenda Dubai kushuhudia uchapishaji wa karatasi za kupigia kura, lakini akaamua kwenda Marekani ambako pia ana uraia wa nchi hiyo. Kujiuzulu kwa Akombe ni pigo kwa tume hiyo ambayo ilikuwa inamtegemea kuzungumza kwa niaba yake na kuitetea mara kwa mara. “Tume ijitokeze wazi, iwe na ujasiri na kusema kuwa uchaguzi huu hauwezi kuwa huru na haki katika mazingira haya,” aliongeza Akombe.
Alisema akiwa Kenya alikuwa anapata vitisho kuhusu maisha yake na huenda asirejee humo kwa muda. Baada ya Akombe kutoa tamko hilo, Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati alizungumza na vyombo vya habari na kusema Akombe alikuwa mmoja wa ofisa bora wa tume hiyo aliyetegemewa na kwamba kujiuzulu kwake kumechangiwa na siasa chafu za wanasiasa nchini Kenya. “Wakenya wenzangu, nchi yetu imebarikiwa kuwa na watu wenye akili duniani na wanaotumia vizuri vipaji vyao kwa manufaa ya nchi zao kama alivyokuwa Akombe, lakini siasa chafu zinazofanywa na wanasiasa wetu zimesababisha ashindwe kufanikisha azma yake kwa taifa hili,” alisema Chebukati.

9 WANG'OKA ACT WAKIMBILIA CCM


ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa chama cha siasa cha ACT Wazalendo, Samson Mwigamba na wenzake tisa, wamejivua uanachama wa chama hicho na kutangaza kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mwigamba alieleza hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, na kuongeza kuwa wamefikia uamuzi huo baada ya kuona uongozi wa sasa wa ACT Wazalendo unachepuka kwa kasi mno nje ya chama tofauti na matarajio yaliyokuwepo. Alisema wameondoka ACT Wazalendo na kujiunga na CCM kwa kuwa ndicho chama kinachoakisi kwa karibu itikadi, falsafa na sera za chama walichotoka.
“Tumejiridhisha kuwa mpangilio wa sasa wa CCM na serikali yake upo katika misingi hii, na Serikali ya Awamu ya Tano ya Dk John Magufuli inaitekeleza misingi hii kwa utashi mkubwa mno,” alieleza Mwigamba na kuongeza: “Tumeamua kujiunga na CCM ili tuendelee kuwa sehemu ya mapambano ya kurudisha nchi katika misingi yake kama ambavyo tulidhamiria ndani ya chama chetu cha zamani.”
Alisema pia wamekwenda CCM kwa kuwa Serikali ya Magufuli ipo katika vitakubwa dhidi ya rushwa na ufisadi, na hivi sasa Tanzania ni kinara wa mapambano dhidi ya rushwa. “Lakini sasa upinzani ambao ndiyo uliasisi vita dhidi ya ufisadi umegeuka kuwa ndiyo watetezi wa mfumo wa kinyonyaji ulioitesa nchi kwa miaka mingi. Sisi tumeamua kujitenga na aina hii ya upinzani,” alifafanua Mwigamba.
Alisema wameamua kujitenga na upinzani unaokerwa na mafanikio ya serikali, kwa kuwa tangu wanachama wenzao Profesa Kitila Mkumbo na Anna Mghwira walipoteuliwa na Rais John Magufuli, kufanya kazi katika utumishi wa umma serikalini, wamekuwa wakikerwa na kutishwa katika utekelezaji wa majukumu yao, hususan wanapoelezea mafanikio ya serikali.
Profesa Mkumbo ambaye alikuwa Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo, aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Aprili 4, mwaka huu, kuchukua nafasi ya Mhandisi Mbogo Futakamba ambaye amestaafu. Kwa upande wake, Anna Mghwira ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho na mgombea urais wa ACT-Wazalendo katika uchaguzi mkuu wa 2015, aliteuliwa Kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Juni mwaka huu, kuchukua nafasi ya Said Mecky Sadiki aliyejiuzulu.
Mwigamba alikuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kuanzisha ACT Wazalendo, na alijiunga nayo mwaka 2014. Alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo ya Katibu Mkuu wa chama, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kampeni na Uchaguzi.
Ofisa Habari wa chama hicho, Abdalah Khamis alisema Mwigamba aliandikiwa barua ya kuitwa leo ili aseme ni sehemu gani ambayo misingi ya chama hicho ilikiukwa. “Aliandikiwa barua aje atoe ufafanuzi nini kimekiukwa na kipi kiboreshwe. Kama kiongozi alitakiwa azungumze. Hatujui analalamikia nini kwa kuwa alikuwa na nafasi ya kueleza hilo kwenye Kamati ya Uongozi,” alisema Khamis, na kusikitishwa na Mwigamba kwa kuwatambulisha wanachama wengine waliohamia CCM kuwa walikuwa viongozi, akidai hawakuwa hivyo.

USHIRIKIANO WA CHINA WAZIDI KUKUA



RAIS wa China, Xi Jinping amefungua Mkutano Mkuu wa 19 wa Chama tawala cha Kikomunisti (CPC) na kuahidi nchi hiyo haitafunga milango ya ushirikiano na nchi nyingine duniani bali kuuendeleza zaidi.
Mkutano huo unaofanyika wakati Rais huyo akimaliza awamu ya kwanza ya kipindi cha utawala cha miaka mitano. Alitumia saa tatu na nusu kuelezea mafanikio aliyopata ikiwemo kuongeza pato la Taifa. Rais JinPing alisema wakati akiingia madarakani mwaka 2012, alikuta Pato la Taifa la China likiwa ni fedha za nchi hiyoYuan trilioni 54 kwa mwaka na sasa pato hilo ni karibu Yuan trilioni 80.
Inaelezwa kuwa kuongezeka kwa pato hilo la taifa kunaashiria nchi hiyo kufikia lengo lake la kuwa taifa lenye uchumi mkubwa duniani. Mbali na kuongeza Pato la Taifa, pia amejivunia kuwaondoa wananchi wa nchi hiyo ya pili kwa uchumi mkubwa duniani zaidi ya milioni 60 katika hali ya umaskini kwa kipindi hicho cha miaka mitano.
Mkutano huo wa siku nne unatarajiwa kutoa mrithi wa nafasi ya urais kama katiba ya chama hicho inavyosema kuwa baada ya miaka mitano, rais aliyepo madarakani anapaswa kumtangaza mrithi wake pamoja na kuchagua viongozi wengine wa ngazi mbalimbali wa chama hicho watakaoongoza nchi hiyo. Katika mkutano huo unaofuatiliwa na watu mbalimbali duniani, mageuzi ya Katiba ya chama hicho yanayolenga kukabiliana na mabadiliko ya mazingira na hali ilivyo kwa sasa yaliwasilishwa rasmi.
“Uzoefu unaonesha kufanya marekebisho ya katiba ya chama kwa maendeleo endelevu na majukumu yaliyopo itasaidia kila mwanachama kuelewa, kutumia na kutekeleza katiba ya chama,” alisema Rais Xi. Katika suala la ushirikiano na nchi mbalimbali duniani, Rais Xi alisema wataendelea kuheshimu uhuru wa mataifa rafiki na kudumisha uadilifu wa mipaka wa mataifa huku wakiandaa mipango ya ushirikiano na kuendeleza miradi ya ushirikiano kwa kutumia majadiliano.
“China itafungua milango ya bidhaa kutoka mataifa rafiki na kulinda haki za kimsingi za wawekezaji wa nje,” alisema. Alisema uchumi wa nchi hiyo umekuwa ukibadilika kutoka kukua kwa kasi hadi kiwango cha ubora wa hali ya juu kimaendeleo kwa kuendeleza uchumi wa kisasa hivyo lazima wazingatia hali halisi ya uchumi wa ndani.
Alisema Serikali yake itawezesha mtaji wa taifa kuwa thabiti, imara na kukua zaidi na kuwezesha kampuni za uwekezaji kutoka China kufikia viwango vya kimataifa na ushindani mkubwa ulimwenguni. “China itazingatia jukumu lake la kutumia bidhaa zinazozalishwa nchini humo na kuboresha mfumo wa usimamizi inayounganishwa na sera ya fedha,”alisema. Katika kukiimarisha chama, alisema kitaendelea kuimarisha vita dhidi ya vitendo vya rushwa na kuhakikisha wanapata ushindi katika vita hivyo.
Alisema katika mfumo wa utawala wa ujamaa, wanazingatia itikadi za Kichina pamoja na kuwa na taifa linalotekeleza mfumo wa kikomunisti. Mkutano huo ulioanza jana, unajumuisha wajumbe zaidi ya 2,307 wanaotoka katika ngazi mbalimbali za kijamii kutoka taaluma na nyanja mbalimbali wakiwemo wachumi, sayansi na teknolojia, ulinzi na usalama, mahakama, elimu, utamaduni, michezo, wakulima na viongozi mbalimbali katika jamii. Pia watachagua viongozi katika kamati mbalimbali za maamuzi za CPC yenye wanachama wanaokadiriwa kuwa milioni 89.44 kwa mujibu wa takwimu zao za mwaka jana.

UVCCM WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI

KASI ya utendaji wa Rais John Magufuli (pichani) imelikuna Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), ambao wamempongeza na kumtaka aendelee na utendaji huo bora.
Akizungumza na wandishi wa habari, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera, Yahaya Kateme alisema Baraza la Vijana limefurahishwa na utendaji wa Rais, hasa katika kuondoa kero za wananchi na hivyo kupunguza maswali.
“Rais amefanya mabadiliko mbalimbali yakiwemo ya kudhibiti utendaji wa watumishi wa umma ofisini, kutoa elimu bure, kutoa mikopo kwa wanafunzi, ukusanyaji kodi, utoaji huduma na kufufua mashirika mbalimbali pamoja na kuanzisha viwanda,” alisema.
Mjumbe wa Baraza Kuu la Vijana (UVCCM), Sylevester Yaredi alimpongeza Rais Magufuli pia kwa kuwaamini vijana na kuwapa nafasi nyingi za uongozi nchini, akaomba vijana nao wafanye kazi vizuri ili kuonesha shukrani kwa kiongozi huyo aliyewateua.

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya na Songwe, Amani Kajuna alisema bado kuna kero chache zikiwemo za maji na umeme vijijini, hivyo wanamwomba Rais ahakikishe wahusika wa wizara sekta hizo wanaondoa kero hizo.

NDALICHAKO ALILIA AJIRA KWA VIJANA




WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema kutokana na ongezeko la ukosefu wa ajira hususani kwa vijana nchini, kuna umuhimu wa kutengeneza mazingira kwa ukuaji wa biashara ili ajira nyingi zipatikane kiurahisi kwa vijana wanaomaliza elimu ya juu ili waweze kujiajiri.
Waziri huyo amebainisha jana Dar es Salaam kuwa kwa sasa Tanzania ina vijana wengi wenye umri wa miaka 15 hadi 34 ambao hawana ajira kutokana na kukosa ujuzi wa kupata ajira ambapo tatizo hilo kwenye miji mikubwa limefikia asilimia 22.3 ikilinganishwa na vijijini ambako ni asilimia 7.1. Alisema hayo wakati akizungumza katika uzinduzi wa Programu za Benki ya Barclays Tanzania zijulikanazo kama Twende Kazi na Balozi Mwanafunzi jijini Dar es Salaam jana.
Profesa Ndalichako alisema tatizo la ukosefu wa ajira linaongezeka kutokana na kutokuwapo kwa uwiano wa ugavi na mahitaji kwenye soko la ajira pamoja na ongezeko la ajira kubakia kwenye sekta isiyo ya kilimo. “Kila mwaka wasichana na wavulana wanaingia kwenye soko la ajira na wanatokana na wahitimu wa sekondari na elimu ya juu ambao wamehama kutoka vijijini kuja mjini kutafuta ajira,” alisema.
Alisema kiwango hicho cha ukosefu wa ajira nchini kinapimwa na idadi ya watu, vijana wasomi wanaotafuta ajira kama asilimia kubwa ya nguvu kazi hali inayosababisha kuwepo na umuhimu wa kutengeneza mazingira mazuri kwa ukuaji wa biashara nchini ili ajira nyingi zipatikane kwa urahisi. Aliishukuru Benki ya Barclays kwa kuwa mstari wa mbele kuisaidia Serikali na jamii katika kuhakikisha tatizo la ukosefu wa ajira linatatuliwa na kupungua kwa kiwango kikubwa kwa kuwawezesha vijana.
Alisema katika miaka 15 ya uwepo wake sokoni, benki hiyo imechukua hatua kupitia mfumo wake wa Shared Growth unaoenda sambamba na Programu ya Twende Kazi, kuwasaidia wahitimu 200 watakaowekwa katika mafunzo ya kujiandaa na soko la ajira katika kampuni mbalimbali nchini kupitia utendaji kazi wa kampuni isiyo ya kiserikali ya Junior Achievement Tanzania ili kupata walio bora zaidi. Alisema pamoja na kutatua tatizo la ajira, benki hiyo pia imesaidia wanafunzi wasio na uwezo wa kujikimu na ada na mahitaji ya chuo kupitia Programu ya Balozi Mwanafunzi ambapo wanafunzi 23 wa mwaka wa kwanza hadi wa nne watasomeshwa miaka mitatu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

MAKUBALIANO YA AWALI KATI YA TANZANIA NA KAMPUNI YA BARRICK GOLD YAONYESHA MWANZO MZURI


RAIS John Magufuli amesema kufikiwa makubaliano kati ya Tanzania na Kampuni ya Barrick Gold Corporation ni mwanzo mzuri, na kwamba Tanzania inaweka mwelekeo ambao haujawahi kuwekwa kokote barani Afrika katika udhibiti wa rasilimali zake.
“Sasa Barrick ni ndugu zetu, msikubali mazungumzo tuliyoyaanza kuingiliwa na watu wengine, tumeweka mwelekeo ambao haujawahi kufanyika popote Afrika, huu ni mwanzo wa kutengeneza Tanzania mpya,” alisema Rais Magufuli. Alitoa kauli hiyo jana Ikulu, Dar es Salaam, wakati wa kutiwa saini kwa makubaliano baada ya Kamati maalumu ya mazungumzo baina ya timu ya wataalamu wa Tanzania na Kampuni ya Barrick Gold Corporation kukamilika.
Katika hafla hiyo iliyofanyika baada ya mazungumzo hayo yaliyochukua takribani miezi mitatu kukamilika, Waziri wa Sheria na Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya mazungumzo aliongozana na baadhi ya wajumbe wake, pamoja na Mwenyekiti Mtendaji wa Barrick, Profesa John Thornton.
Akizungumza baada ya kutiwa saini kwa makubaliano hayo ambayo Kampuni ya Barrick imekubali kulipa Dola za Marekani milioni 300 (zaidi ya Sh bilioni 700), kama malipo ya kuonesha nia njema ya kufidia fedha zilizotokana na upotevu wa mapato kupitia biashara ya kampuni hiyo, Rais Magufuli alisema huo ni mwanzo mzuri.
“Huu ni mwanzo nzuri wa kutengeneza Tanzania mpya na sasa Barrick ni ndugu zetu tumeanza mazungumzo vizuri na tumefikia hatua nzuri ambapo wamekubali kutoa dola milioni 300, wametambua msimamo wetu ndiyo faida ya mazungumzo,” alisema Rais Magufuli. Aidha, Rais Magufuli ameafiki kuundwa kwa kamati ndogo itakayohusisha pande zote mbili za mazungumzo ili kupitia nyaraka zote za malipo na kuangalia maeneo yenye utata ili kuangalia jinsi ya kutafuta suluhu.
“Chochote kinawezekana kinachohitajika ni uaminifu kati ya pande mbili, tutafikia muafaka kwa mazungumzo, ila wamefahamu kuwa hatutaki kuchezewa tena, tumekuwa shamba la bibi kwa muda mrefu, sasa basi,”alisema Rais Magufuli. Mbali na kusifia hatua ya mazungumzo iliyofikiwa na pande zote mbili, Rais Magufuli aliitaka kampuni hiyo ya Barrick kuwasilisha fedha hizo haraka kwa sababu zina kazi ya kufanya na kusisitiza kuwa nchi itaendelea kulinda rasilimali zake zote kwa faida ya Watanzania.
Alisema pamoja na kampuni hiyo kukubali kulipa kianzio cha fidia ya biashara ya madini, pia wamekubali kuanzia sasa Tanzania itakuwa ikipata nusu ya faida ya biashara ya kampuni hiyo ya madini ya dhahabu sambamba na kumiliki hisa kwa asilimia 16. Mbali na kulipa faida na nchi kumiliki hisa hizo, Rais Magufuli alisema kampuni hiyo pia itaendelea kulipa kodi nyingine kama kawaida zikiwemo za halmashauri pamoja na menejimenti ya kampuni hiyo itaundwa kwa kuwahusisha pia Watanzania.
Akizungumzia suala la kuundwa kwa menejimenti ya kampuni hiyo itakayowashirikisha Watanzania, Rais Magufuli alitoa mwito kwa vyombo vitakavyohusika na usaili wa watu wenye sifa, kuangalia kwa makini tabia na mwenendo wao, ili kuhakikisha wanapatikana watu waadilifu na siyo wezi.
“Tumesikia katika makubaliano yao menejimenti mpya ya Kampuni ya Barrick sasa itaundwa kwa kuzingatia watu wa Tanzania, sasa hii ni faida kwetu labda tuweke majizi, ila nitoe rai kwa vyombo vitakavyohusika kutafuta watu wenye sifa, kuhakikisha wanawachunguza kwa undani na kujua tabia zao ili wapatikane watu sahihi kwa faida ya nchi,” alisisitiza Rais Magufuli.
Akiipongeza kamati hiyo, Rais Magufuli alisema imefanya kazi yake kwa weledi mkubwa na uzalendo kwani walikuwa na uwezo wa kupindisha mambo au kula rushwa, lakini wamekuwa waaminifu kwa faida ya taifa.
“Naipongeza kamati, mngeweza kukaa kimya au kula rushwa lakini pamoja na ukubwa wa wajumbe wa Barrick ambao nasikia walifika 25 na nyie mko nane, lakini mmeonesha uwezo wenu mkubwa na nidhamu, na wametambua jambo hili siyo jepesi na mmefikia hatua nzuri, nitaandaa siku ya kuwapongeza hata kwa kuwapa cheti kwa kuwa mmejitolea maisha yenu,” alisema Rais Magufuli.