Mkwara wa Lipumba wapagawisha wabunge wa CCM | Magazeti ya leo| Tanzania News |Tanzania Today

Mkwara wa Lipumba wapagawisha wabunge wa CCM | Magazeti ya leo| Tanzania News |Tanzania Today

Upelelezi wa kesi ya Halima Mdee wa kumtolea lugha ya matusi Magufuli u...

Leo September 12 2017 upelelezi wa kesi ya kumtolea lugha ya matusi Rais John Magufuli inayomkabili Mbunge wa Kawe Halima Mdee umekamilika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

LOWASSA ATOA SIRI, TUNDU LISSU KUPIGWA RISASI

TUNDU lisu Atamka maneno (12 tu) makali baada ya kufungua macho hospita...

Chadema: Tundu Lissu Apumulia Mipira, Lakini Jasiri, Tuendelee Kumuombea

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimezungumzia maendeleo ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyejeruhiwa vibaya hivi karibuni baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Vincent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema, amesema hali ya Lissu imekuwa ikibadilika mara kwa mara na inaonesha alipigwa zaidi ya risasi tano za kivita kwenye mwili wake, zilizomjeruhi vibaya sana. Viongozi hao wa Kamati Kuu ya Chadema wamesema mbele ya mkutano wa waandishi wa habari katika makao makuu ya ofisi yao iliyoko Kinondoni, jijini Dar es Salaam, kwamba hawana imani na jeshi la polisi na serikali katika kuwatafuta na kuwabaini waliokula njama za kumshambulia mbunge huyo

KANISA KATOLIKI LATOA TAMKO KULAANI VURUGU NA MAUAJI



SeeBait
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu. 

Dar es Salaam. Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), limelaani shambulizi la hivi karibuni lililotekelezwa na watu wasiojulikana dhidi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Mbunge huyo aliyejeruhiwa Septemba 7 kwa kupigwa risasi tano mjini Dodoma, hivi sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan, jijini Nairobi nchini Kenya.

Baraza pia limeungana na Watanzania kulaani kwa nguvu zote matendo yote ya vurugu, mauaji na uvunjifu wa amani nchini.

Tamko la baraza hilo lililosainiwa na Makamu wa Rais wa TEC, Askofu Beatus Kinyaiya limetolewa baada ya kikao cha kawaida cha baraza kilichofanyika kwa siku mbili Septemba 9 na 10 jijini Dar es Salaam.

“Katika Taifa letu sasa tunashuhudia matendo ya mauaji ya watu wasio na hatia kama ilivyokuwa kule Mkuranga, Rufiji na Kibiti, utekwaji wa watu na kuteswa, utekaji wa watoto, ulipuaji wa ofisi za watu na hivi karibuni shambulio la mbunge Lissu,” limesema baraza katika tamko hilo.

Imeelezwa vurugu na mashambulizi ya aina yoyote ile yanalifedhehesha Taifa kwa kuwa matendo hayo ni dhambi, uhalifu na si utamaduni wa Mtanzania, hivyo vyombo vinavyohusika havina budi kuyakomesha mara moja.

BUNGE LAAHIDI KUMPA USHIRIKIANO JAJI MKUU TANZANIA



SeeBait

Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amefunguka na kudai atahakikisha yeye na wabunge wanampa ushirikiano Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma aliyeapishwa leo baada ya kuteuliwa siku ya jana Septemba 10 mwaka huu.


Ndugai ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anatoa salamu za wabunge katika ghafla hiyo ya uapisho iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa bila ya kumsahau Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.


"Sisi kama bunge tunawahakikishia ushirikiano mkubwa sana kwa kuhakikisha kazi za Mahakama zinaendelea kama zilivyo kikatiba na tutaheshimu sana. Yale maneno na makombora moja moja ya bungeni ni vitu vya kawaida, ndiyo utamaduni wa bunge",amesema Ndugai.


Aidha, Ndugai amesema Mahakama inamchango mkubwa kwa wananchi pamoja na taifa kwa ujumla kwa kuwa hicho ndicho chombo pekee kinachoweza kumtetea mnyonge kuweza kupata haki yake kutoka kwa waporaji.


"Kuwepo kwa Mahakama ndiyo usalama wetu, amani, kheri na matumaini ya mnyonge katika sheria na maamuzi ya Mahakama. Kwa hiyo tunakutakia kila la kheri katika kazi yako, tunakuombea kwa Mwenyezi Mungu na tutakusaidia na kuomba msaada wako",amesisitiza Ndugai.


Kwa upande mwingine, Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma ameahidi kufanya kazi katika maadili ya kisheria pamoja na kurudisha imani ya wananchi kuhusiana na kupata misaada ya kisheria inayotolewa katika Mahakama mbalimbali ndani ya Tanzania

LOWASSA AMTEMBELEA TUNDU LISSU HOSPITALIYA ADHA KHAN NCHINI KENYA



SeeBait

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa yupo Nairobi nchini Kenya kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyelazwa katika Hospitali ya Aga Khan, baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana.


Lissu ambaye pia ni mwanasheria wa Chadema alijeruhiwa kwa risasi tano Alhamisi Septemba 7 akiwa ndani ya gari nyumbani kwake Area D mjini Dodoma akitokea bungeni.


Katika akaunti yake ya Twitter, Lowassa ame-tweet akisema, “Earlier today i paid a visit at Nairobi Hospital to see our MP, President of TLS and dear friend @tundulissutz He is recovering well. It is Sad times for Tanzania. Let us all keep praying.”


Kwa tafsiri isiyo rasmi amesema “Mapema leo nilitembelea Hospitali ya Nairobi kumwona mbunge, Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) na rafiki kipenzi Tundu Lissu. Anaendelea vizuri. Ni kipindi cha masikitiko kwa Tanzania. Kwa pamoja tuendelee kuomba.”


Katika tweet hiyo, Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, ameweka picha akiwa pamoja na Alicia ambaye ni mke wa Lissu; Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na dereva wa Lissu Simon Mohamed Bakari.



Earlier today i paid a visit at Nairobi Hospital to see our MP, President of TLS and dear friend @tundulissutz
He is recovering well. 1/2

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO AGOSTI 06,2017


Magazetini leo Jumapili Agosti 06, 2017


MPYA:TCU YATOA MAAGIZO MAZITO KWA WANAFUNZI WANAOTEGEMEA KUOMBA VYUO VIKUU MWAKA HUU 2017/2018


Hapo jana Tume ya vyuo Vikuu Tanzania TCU iliitisha vyombo vya habari na kuamua kuzungumzia swala zima la udahili kwa wanafunzi wa kidato cha sita mwaka huu 2017/2018.

Kaimu katibu Mkuu Nacte alisema Tume imetekeleza agizo  la kuawataka wanafunzi waombe vyuo wanavyotaka wenyewe ambapo hapo nyuma ilibainika kuwamba TCU walikuwa wakiwapangia wanafunzi vyuo.

Jumla ya wanafunzi  70,550 wamepata daraja la kwanza hadi la nne,kati ya hao ,Amema kwamba mwaka huu zaidi ya 50.7% ya wanafunzi waliomaliza kidato cha sita mwaka huu wanatarjiwa kujiunga na elimu ya juu 2017/2018.

Kwa mwaka wa masomo 2017/2018,udahili wa wanafunzi rasimi utaanza tarehe 22 july 2017 kwenye vyuo vyote hapa nchini na maombi yatatumwa moja kwa moja chuoni na sio TCU tena.

TCU IMETOA MAAGIZO YAFUATAYO KWA WANAFUNZI  WANAOTARAJIA KUOMBA

1. WAOMBAJI WATUME MAOMBI MOJA KWA MOJA KWENYE CHUO HUSIKA,VYUO VINA TAARIFA HIYO TAYARI.

2.WAOMBE KUSOMA KTIKA PROGRAMME NA VYUO AMBAVYO VIMEIDHINISHWA NA TCU NA NACTE,ORODHA IPO KWENYE WEBSITE YA TUME TAYARI.

3.WAOMBAJI WANASHAURIWA WAOMBE WENYEWE USIMTUME MTU,KUEPUSHA USUMBUFU BAADAE.

4.ENDSAPO UTACHAGULIWA CHUO ZAIDI YA KIMOJA,UTAPEWA TAARIFA NA UTATAKIWA KUCHAGUA CHUO KIMOJA TU.

5.MNASHAURIWA KUSOMA KWA MAKINI SIFA ZILIZOTANGAZWA 2017/2018.

6.TCU HAITATOZA ADA YOYOTE WAKATI WA UOMBAJI WA VYUO VIKUU,ILA KUTAKUWA NA ADA KATIKA CHUO UNACHOTAKA KUOMBA.

7.MNASHAURIWA NA KUSISITIZWA KUOMBA PROGRAMMES TU ZILIZOIDHINISHWA NA TCU NA NACTE.

8.VYUO VIKUU VINAKUMBUSHWA KUAINISHA ADA YA KILA PROGRAMME WAKATI ZIKITANGAZA KOZI ZAKE.

9.VYUO VINAKUMBUSHWA KUDAHILI WANAFUNZI WENYE SIFA STAHIKI KAMA ZILIVYOAINISHWA NA KUPITISHWA NA TCU AU NACTE.

Diamond na Harmonize wazinguana wakiwa location, Diamond amnyang'anya ng...

HOT NEWS :TRAFIKI AZICHAPA NA DEREVA MORO

Hali ya kushangaza imetokea leo mkoani morogoro pale ambapo askari wa jeshi la polisi alipokuwa anapigana na wenye magari kutoka na askari halo kushindwa kufungua njia kwa ajili ya skari hali kupita na kuendelea na safari.nakuomba endelea kutizama taarifa hii kwa umakini.pia nifuatilie kwenye page yangu ya faceebook ili uwe wa kwanza kupata taarifa zaidi

New:Rais alani kupigwa risasi kwa mheshimiwa Tundu Lissu

Baada ya kupata taarifa ya kupigwa kwa mbunge wa singida mashariki mheshimiwa Tundu Lissu.Mheshiwa Raisi kupitia ukurasa wake wa twitter amelaani vikali tukio hilo.
kwa taarifa mpya za kila muda nikuombe ndugu  mfuatiliaji wa blog hii nikuombe uni follow kwenye account zangu za facebook pia nikuombe ujisajili kwenye account yangu ili uweze kupata latest news

unamjua aliyempiga mheshiwa tundu lissu sikiliza hii

baada ya kusikia taarifa ya kupigwa risasi kwa mheshimiwa Tundu Lissu mtu anayedhaniwa amempiga risasi amegundulika kujulikana baada ya kuandika kwenye ukurasa wake wa facebook huku akiomba ruhusa ya kumuuwa mheshiwa lissu.inasemekana kuwa jamaa huyo alikuwa anaomba ruhusa ya kumuua lissu kutoka na taarifa yake ya kusema kuwa serikali inahumu nchi

full video ya TUNDULISU kilichoendelea baada ya KUPIGWA RISASI |share kw...

ulikuwa hujui nini kilichompata mheshimiwa tundu lissu.nimekusogezea taarifa hii kwa ukaribu zaidi.ilikuwa ni majira ya saa saba mchana ambapo mshimiwa lissu alipokuwa anatoka bungeni.

Kiingereza cha Harmonize, Mzungu kamsaidia?

staa wa nyimbo ya sina na moja kati  ya wanamziki wanaomilikiwa na lebo ya WCB chini ya diamond.harmonize alikutana na moja ya mapresenter  wa vipindi nchini kenya akiwa kwenye moja ya event ambazo alialikwa kuperform.kikubwa zaid ni jinsi alivyokuwa ana flow kingereza

Hii kali ya chid benz

Kama ulikuwa huijui hii saa nakuvutia hii ya chid benz moja kati ya marapa waliokuwa wanafanya vizuri kipindi kile.ila baada ya kitambo kirefu cha kukutana na kasumba nyingi hasa zile za madawa ya kulevya,sasa mpya hii hapa kali yake.Akiwa anojiwa na enewz chid afunguka asema anatarajia kufanya wimbo na rapa ambaye alikuwa anafanya vizuri kipindi cha miaka ya 96 rapa amir shakir

Roma awachana WCB na uongozi

CHADEMA WAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI

Leo hii chama cha demokrasia na maendeleo(chadema) wamekutana na waandishi wa habari kuzungumzia hali inayoendelea kwenyetaifa hasa ya uvunjaji wa sheria.msemaji wa chama hicho pia aliiwatakia wanafunzi wanaelekea kwenye mtihani wao wa mwisho wa elimu ya msingi.pia msemaji huyo azungumziahali inayoendelea katika bunge hili la september

FULL VIDEO: Alivyopokelewa Rayvanny kutoka Marekani



kama kawaida kwanguleo inakuletea taarifa zinazoendelea kujiri kila muda.
mwanamziki anayetokea kwenye lebo ya wassafi classic Rayvanny baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu julius kambarage nyerere alipata mapokezi makubwa sana kutoka kwa mashabiki wake pamoja na bosi wake msanii  diamond platinum.shamrashamra za mapokezi zilianzia kwenye sehemu ya mapokezi kwani watuwalikuwa ni wengi kupita ilivyotarajiwa