Ally Hapi: Kinondoni Siyo Wilaya ya Mashamba Tena

UTATUZI MIGOGORO YA ARDHI KINONDONI WASHIKA KASI
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Hapi ameendelea na juhudi za utatuzi wa migogoro mikubwa ya ardhi ambayo inahusisha wananchi wengi na wenye mashamba.
Hapi ameendelea na vikao mbalimbali vya utatuzi ambapo leo amefanya kikao na wananchi wa maeneo ya Kinondo, Dovya na Mbopo na kuwaahidi kuwa serikali imejipanga vema kumaliza mgogoro huo ili wananchi waishi kwa amani.

Hapi ameelezea dira ya wilaya yake kuwa ni kuhakikisha mashamba yote yanapimwa na kuwa viwanja ili kuweka mpango bora wa matumizi ya ardhi na kukomesha uvamizi wa ardhi uliochochewa na wenye mashamba ama kuyatelekeza mashamba yao kwa muda mrefu au kushindwa kumudu kuyaendeleza. Baada ya upimaji kila mwenye viwanja atalazimika kuwa ameviendeleza ndani ya muda maalum ili kuepusha migogoro.
Migogoro mingine mikubwa inayoendelea kutatuliwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ni pamoja na TBA Mabwepande na Nyakasangwe ambao sasa umefikia hatua ya upimaji viwanja.

No comments: