Mwana FA na Mrisho Mpoto Watoa Neno Zito Kuhusu Ripoti ya Mchanga wa Mad...

Wasanii wa muziki wa Bongo Fleva na filamu, ni miongoni mwa wageni walioalikwa Ikulu wakati mheshimiwa Rais akikabidhiwa ripoti ya kamati ya mchanga wa madini na Tume ya Profesa Ossoro ambapo mbali na kutumbuiza, pia walipata nafasi ya kutoa maoni yao kuhusu ripoti hiyo.
Kwa upande wake, Mwana FA anayesumbua na ngoma yake ya Dume Suruali, alisema ripoti ya kamati ya pili, imetoa mwanga wa nini cha kufanya katika suala zima la kisheria, ikiwa ni mwendelezo wa kile kilichogundulika na kamati ya kwanza.
Mwana FA alisema Watanzania wote tunapaswa kuwa wazalendo na kumuunga mkono mheshimiwa rais badala ya kuendelea kutishana mitaani kwamba nchi itashtakiwa, wafadhili wataacha kuleta misaada.
Kwa upande wa Mrisho Mpoto, naye aliwataka Watanzania kuwa na umoja na uzalendo na kumuunga mkono mheshimiwa rais kwani kama ataendeleza msimamo huu, Tanzania Mpya, ya maziwa na asali ikiwadia hata kama itakuwa watakaofaidi ni vizazi vijavyo.

No comments: