Beka Afunguka ukweli kuhusu Aslay kuwasaliti, Asema Mkubwa Fella hajawag...

Habari za kuvunjika kwa Bendi ya Yamoto, zinazidi kuzagaa lakini habari mpya ni kwamba, miongoni mwa memba wa kundi hilo, Beka One amefunguka kwa kirefu kuhusu maelezo hayo.
Miongoni mwa mambo aliyoyazungumza Beka One, kama ilivyo kwa memba wengine wa kundi hilo, ameendelea kukataa kwamba bendi hiyo haijafa isipokuwa wameamua kufanya kazi mmojammoja baada ya kujiona wamekua.
Beka amekanusha pia madai kwamba Said Fella amewajengea nyumba na kueleza kuwa kwa sasa wanaishi Tabata jijini Dar wote watatu isipokuwa Aslay.
Kuhusu suala la kwamba walikubaliana waondoke Yamoto band kwa sababu maslahi yalikuwa madogo, amekanusha suala hilo na pia kuhusu suala la mwenzao, Aslay kuwageuka na kurudi kufanya kazi na Mkubwa Fella, kwamba pia si kweli.
Yamekuwepo maneno mengi mitaani kuhusu kusambaratika kwa bendi hiyo kwa kile kilichoelezwa kwamba ni wasanii hao kuchoshwa na unyonyaji wanaofanyiwa na uongozi wao lakini si wanamuziki hao wala viongozi wao waliowahi kutamka hadharani kwamba bendi hiyo imekufa.

No comments: